Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Hamida Mohamedi Abdallah

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH: Mheshimiwa Spika, ninaunga mkono hoja na ninampongeza Waziri Mkuu kwa namna ambavyo anachapa kazi yeye na wasaidizi wake wote katika kutekeleza mipango mbalimbali ya kibajeti ya maendeleo katika sekta mbalimbali.

Mheshimiwa Spika, mvua zilizonyesha zimeathiri kwa kiasi kikubwa na uharibifu mkubwa wa barabara nyingi,mashamba na mifugo.

Mheshimiwa Spika, ninaiomba Serikali kuona namna ya kusaidia kwa haraka sana kuhakikisha wananchi wanapata chakula. Kupimiwa viwanja bure, kuwafanya wananchi kuwa na makazi na kujenga maeneo salama.

Mheshimiwa Spika, Serikali iongeze fedha upande wa ujenzi, barabara zimeathiriwa sana, sasa shughuli za usafiri na usafirishaji zimekuwa ngumu sana.

Mheshimiwa Spika, ninaunga mkono hoja, ahsante sana.