Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Dr. Charles John Tizeba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. DKT. CHARLES J. TIZEBA: Mheshimiwa Spika, awali ya yote niipongeze Serikali kwa kazi kubwa na nzuri sana inayofanyika ya kutuletea maendeleo Watanzania. Nimpongeze Rais wetu mpendwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa uongozi wa kizalendo usio mfano wa kuiongoza nchi yetu. Nimpongeze pia Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa uongozi wake uliotukuka.

Mheshimiwa Spika, nimshukuru na kumpongeza sana rafiki na kiongozi wangu, Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kazi nzuri ya kusimamia shughuli za Serikali. Kazi inaonekana, huduma zinaonekana, maendeleo yanaonekana na hilo hakuna ubishi.

Mheshimiwa Spika, Niipongeze sana Serikali kwa maendeleo makubwa ambayo yamepatikana katika jimbo langu la Buchosa. Mambo ni mengi haina sababu ya kuyataja katika mchango wangu.

Mheshimiwa Spika, jambo ambalo ningependa kutoa ushauri kwa Serikali ni kuhusu urahisishaji wa namna ya kufanya biashara hapa nchini. Katika eneo hilo bado yako mambo ambayo yanasumbua wafanyabiashara. Blue print inabidi ifanyiwe kazi kwa nguvu zaidi. Kuna taasisi za udhibiti bado zinasumbua wafanyabiashara badala ya kuwawezesha na kuwasimamia.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.