Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi na mimi nichangie kwa kifupi hoja iliyoko mezani.

Naomba nitangulie kwanza kuwa kumpongeza sana Waziri Mkuu na Waziri na Naibu Waziri walioko chini yake pamoja na watendaji wote kwa wasilisho zuri na kazi nzuri inayofanyika Wizarani.

Mheshimiwa Spika, kipekee niruhusu kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa kazi nzuri anayofanyia Watanzania tangu walivyomchagua mwaka 2015. Lakini pia nichukue nafasi hii kukupongeza kwa dhati kabisa kwa jinsi ambavyo umeliongoza Bunge letu tukufu kwa umahiri mkubwa.

Mheshimiwa Spika, nitajikita kwenye maliasili na utalii na afya kwenye mchango wangu huu.

Mheshimiwa Spika, kwanza naomba Waziri Mkuu atusaidie mgogoro wa mpaka kati ya wananchi wa Kitongoji cha Momela na Hifadhi ya ANAPA utatuliwe kwa hekima kama ilivyo dhamira ya Mheshimiwa Rais kwa kuunda jopo la mawaziri nane. Historia inaonesha wananchi wa eneo hilo wamekuwa victim wa kuchomewa nyumba na kutaka kuhamishwa tangu mwaka 1951.

Mheshimiwa Spika, Kituo cha Afya cha Momela kiko katika hatari ya kufungwa kwa sababu ya tatizo dogo sana la ownership. Tulikwenda pale na Naibu Waziri wa Afya akatoa maelekezo isainiwe MOU ya PPP ili status quo ya kituo iwe maintained pamoja na kupandisha hadhi kituo kiwe charitable hospital. Hayo hayajafanyika mpaka sasa na matunda yake wananchi wa eneo hilo ambalo liko mbali na Hospitali ya Wilaya wanakosa huduma muhimu ya afya bila sababu za msingi.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana na naunga mkono hoja kwa 100%.