Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kupata nafasi ya kuchangia hotuba ya bajeti ya Waziri Mkuu.

Mheshimiwa Spika, napenda kumpongeza Mheshimiwa, Dkt. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Rais na Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa, Waziri Mkuu pamoja na watendaji wote kwa kazi nzuri yenye mafanikio kwenye sekta zote.

Mheshimiwa Spika, awamu hii imeweka historia ya nchi hii kwa ujenzi wa reli ya kisasa SGR, ujenzi wa mradi wa kuzalisha umeme wa Mwalimu Nyerere, ununuzi wa ndege na kufufua shirika la ndege, uboreshaji wa huduma ya afya ikiwemo ujenzi wa vituo vya afya na hospitali za Wilaya, ujenzi wa maboma ya shule za msingi na sekondari na msingi, mafanikio ya usambazaji umeme vijijini na pia miradi mikubwa ya maji.

Mheshimiwa Spika, pamoja na hotuba nzuri ya bajeti, napendekeza Serikali iendelee kuimarisha Kamati ya kudhibiti kuenea kwa ugonjwa wa virusi vya corona (covid-19) ikiwa ni pamoja na kuwezesha kuwepo kwa coronavirus contingency plan kwa sekta zote. Hii itasaidia kuimarisha utambuzi wa changamoto za kiafya na za kiuchumi lakini kutambua pia fursa zilizopo na ambazo zinaweza kupunguza athari za kiuchumi.

Mheshimiwa Spika, napendekeza kuchukua hatua za kuchochea ubunifu katika kukabiliana na changamoto zinazotukabili ikiwemo hata watalaam wetu kushiriki uvumbuzi wa chanjo ya covid-19'.

Mheshimiwa Spika, napendekeza Serikali iangalie fursa kwenye sekta ya kilimo na madini na kuongeza uwekezaji na hata kuvutia wawekezaji kwenye uzalishaji wa mazao ya chakula.

Mheshimiwa Spika, napendekeza mpango wa haraka kuvutia wawekezaji katika madini ya chuma, bati na Niobium. Pia Serikali iongeze mtaji wa Benki ya Kilimo (TADB) na Benki ya Rasilimali (TIB).

Mheshimiwa Spika, katika kipindi hiki tunaposhuhudia mtikisiko wa uchumi kidunia, napendekeza Serikali kuangalia jinsi ya kusaidia mabenki na hata uwekezaji kwenye kilimo kuwezesha kuwepo kwa stimulus package. Kuna fursa kwenye uzalishaji wa mazao ya chakula na hata mazao ya mifugo. Katika kipindi hiki Serikali iendelee kusisitiza kuimarisha matumizi ya teknolojia kwenye masoko ya mazao (TMX) na mfumo wa stakabadhi ghalani.

Mheshimiwa Spika naunga mkono hoja.