Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Ali Salim Khamis

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mwanakwerekwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. ALI SALIM KHAMIS: Mheshimiwa Spika, nachukua fursa hii na mimi kutoa mchango wangu wa maandishi kama ifuatavyo:-

Kwanza nianze na maradhi ya Corona. Ili kudhbiti ugonjwa huu mambo yafuatayo yazingatiwe:-

Mosi, kama Serikali imeamua shughuli za kijamii waendelee kama masoko, maeneo ya usafiri wa umma na kadhalika, wakati umefika sasa nikuzuia watu kutoka nje ya nchi, pia maeneo yaliyopatikana maambukizi yazuiliwe watu kutoka na pia kuingia.

Jambo la pili ni muhimu kuangalia upatikanaji wa vifaa vya uchunguzi pamoja na vifaa kwa ajili ya wauguzi na madaktari kuweza kujikinga na maambukizi wakati wa kutoa huduma kwa wagonjwa.

Tatu, katika Ofisi ya Waziri Mkuu iko haja ya kutenga bajeti ya dharura ili kukabiliana na janga hili kwani dharura inaweza kutokea wakati wowote.

Mheshimiwa Spika, nnem mwaka 2017 tulipitisha sheria ya mgawanyo wa wafanyakazi katika taasisi za Muungano asilimia 72 kwa 28 likiwemo Bunge la Jamhuri ya Muungano hadi sasa marekebisho ya wafanyakazi bado, naomba lifanyiwe kazi ili uwiano upatikane.

Tano, kutokana na janga la Corona Serikali iangalie ni namna gani kuangalia kuondoa kodi kwa biashara zote zilizoathirika kutokana na janga hili walau kwa miezi mitatu.

Mheshimiwa Spika, ni matumaini yangu kuwa ushauri wangu utafanyiwa kazi.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.