Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Zainab Mndolwa Amir

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. ZAINAB M. AMIRI: Mheshimiwa Spika, awali ya yote namshukuru Mungu kwa kunipa afya njema ili niweze kuchangia katika hotuba ya Waziri Mkuu.

Mheshimiwa Spika, ili kufikia Tanzania ya viwanda nashauri fedha zinazotengwa katika bajeti zipelekwe kwa wakati ili kuharakisha miradi iliyopangwa itekelezwe ipasavyo.

Nashauri kwa wamiliki wa viwanda vinavyotumia sukari ya viwandani walipwe kwa wakati fedha zao ambazo wanadai sasa takriban miaka minne hawajalipwa asilimia 15 withholding tax ambayo inapelekea wamiliki wa viwanda kupunguza uzalishaji pamoja na kupunguza wafanyakazi sababu mitaji yao imeshikiliwa na Serikali. nashauri walipwe ili uzalishaji uongezeke na kupata pato la Taifa.

Mheshimiwa Spika, nashauri askari wa usalama barabarani wasiwabambikizie makosa madereva, watumie weledi wao kubaini makosa mbalimbali, maana utakuta trafiki anatumia kifaa cha kumulikia speed maarufu tochi, badala ya kupiga picha namba ya gari wanapiga picha bodi ya gari na kutumia picha hiyo kukamata magari yote ya kampuni husika maana jina na rangi za magari zinafanana. Hivyo nashauri askari wapatiwe mafunzo ya kutosha kuondoa kero.