Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Spika, natoa pongezi kwa Waziri Mkuu na Waziri kwa kazi nzuri ya kujenga Taifa letu.

Mheshimiwa Spika, Serikali imeongeza huduma za afya kwa nchi nzima hii hatua nzuri kwa wananchi kupata huduma kwa urahisi. Ujenzi wa Hospitali kwa Halmashauri 67 katika Halmashauri mpya. Halmashauri ya Mufindi Hospitali imejengwa na itanisaidia sana katika majimbo ya Mufindi Kusini na Kaskazini.

Mheshimiwa Spika, kuhusu ujenzi wa sekondari ya Mbalamaziwa, Mgololo na Idete, wanafunzi wameanza kusoma katika sekondari ya Idete, nashukuru sana Serikali kwa kukamilisha ujenzi huo. kuhusu umeme vijijini kata 15 umeme umeshafika bado kata moja tu ya Idunda, naomba Serikali kupeleka umeme katika kata ya Idunda.

Mheshimiwa Spika, maji ni tatizo kubwa sana katika Kata ya Mtwango, Igowole, Nyololo na kata ya Itandula na Mtambula bado hatujapata maji ya bomba. Naomba sana Serikali kukamilisha miradi ya maji katika kata hizo.

Mheshimiwa Spika, barabara ni tatizo kubwa, barabara ya Mafinga hadi Mgololo bado ujenzi wa kiwango cha Lami. Kuna barabara ya Nyololo, Kasanga, Luhunga na Kilolo barabara hizi ni mbovu sana. Naiomba sana Serikali kujenga barabara hizo.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha na naunga mkono hoja. Ahsante.