Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Eng. Christopher Kajoro Chizza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buyungu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. ENG. CHRISTOPHER K. CHIZA: Mheshimiwa Spika, napenda kumpongeza Mheshimiwa Waziri Mkuu, Waheshimiwa Mawaziri wa Nchi, Makatibu Wakuu na watendaji wote katika Taasisi zilizo chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa hotuba nzuri iliyosheheni mafanikio katika sekta mbalimbali.

Mheshimiwa Spika, mimi niko katika Kamati ya LAAC, katika ziara nyingi tulizofanya kukagua utekelezaji wa miradi mikoani, nilijikita sana kuchunguza miradi ya ujenzi wa madarasa, zahanati, vituo vya afya, stendi za mabasi, masoko, miradi ya maji na umwagiliaji na kadhalika. Ninapongeza juhudi kubwa inayofanywa na Serikali kutekeleza miradi hiyo kwa gharama nafuu na mahali pengine kwa kutumia mtindo wa force account na ushirikishaji wa wananchi.

Napenda kushauri mambo yafuatayo; kwanza mara kadhaa tumeshuhudia radi zikiharibu majengo, yakiwemo madarasa na hata kujeruhi na kuua walimu na wanafunzi. Nashauri suala la kuweka mitego ya radi katika public buildings zote zikiwemo nyumba za ibada hasa katika maeneo yenye radi liwe la lazima ili kuokoa maisha ya watu na fedha za umma.

Pili, baadhi ya majengo yanalalamikiwa kwa kujengwa chini ya kiwango. Naishauri Serikali iajiri wahandisi wachache na mafundi sanifu wengi katika Halmashauri zetu ili wazisaidie Kamati za Ujenzi kudhibiti ubora wa kazi katika majengo ya umma. Hali ilivyo sasa ni uchache mkubwa wa wataalamu hasa katika Halmashauri na TARURA. Bado kuna udhaifu mkubwa katika kusimamia ubora wa kazi na usimamizi wa mikataba ya ujenzi.

Mheshimiwa Spika, tatu, mafuriko yanayoendelea sasa kuharibu miundombinu yetu tuyatumie kama changamoto. Trend and periodicity ya miaka mingi ya ukame na mafuriko inaonesha kwamba kila baada ya miaka takribani minne huwa nchi yetu inapata ukame na upungufu wa chakula. Tutumie fursa hii sasa kuyavuna maji yanayopotea na kuyahifadhi katika mabwawa ili baadaye tuyatumie kwa kilimo cha umwagiliaji na matumizi mengine.

Mheshimiwa Spika, hali ilivyo sasa ni kwamba tunatumia fedha nyingi sana kukarabati miundombinu iliyoharibiwa na mafuriko huku tukiyaachia maji hayo hayo kutiririka hadi baharini bila kutunufaisha.

Mheshimiwa Spika, mara nyingi tunakumbuka jambo hili tunapopata ukame, njaa na upungufu wa chakula. Mifano hai ni mafuriko ya El-nino yaliyotokea katika miaka ya 1990 na njaa ya mwaka1974. Rejea pia Azimio la Moshi la Kilimo cha Umwagiliaji, Kilimo cha Kufa na Kupona na maazimio mengine yaliyohusu kupambana na ukame.Naunga mkono hoja.