Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Abdallah Majurah Bulembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. ALHAJI ABDALLAH M. BULEMBO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuchangia kwenye hotuba hii ya Mheshimiwa Waziri Mkuu. Kwanza nichukue nafasi kumpongeza sana Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano kuweza kuniona kwenye wateule wake 10 kuja Bungeni kujifunza Bunge linaishije. Pili, nimpongeze Mheshimiwa Makamu wa Rais nina imani walishirikiana na Mheshimiwa Rais kuweza kufanya uteuzi huu akiwemo na Mheshimiwa Waziri Mkuu.

Mheshimiwa Spika, mimi leo sina mengi sana nataka kusema machache kidogo. Kwanza ni pongezi kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano. Waziri Mkuu ni mfano wa Mawaziri wachache ambao watu walishaonekana. Kwanza ni mvumilivu, pili mstahimilivu, tatu Mheshimiwa Serukamba amesema kumuona ni rahisi lakini hata ukiwa unajadiliana naya huwezi kujua kama ni Mheshimiwa Waziri Mkuu. Hajakilewa kile cheo, hakijambeba kama Mheshimiwa Waziri Mkuu, kwa hali hiyo, nasema na mimi ni mmojawapo ninayeaga kwamba sitarudi Bungeni, sitegemei kugombea chochote, ni mstaafu kwa sababu nimeshiriki siasa zaidi ya miaka 30, sijawahi kufanya kazi kwenye ofisi yoyote ya Serikali, nimefanya ujasiriamali na siasa miaka 30. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mwaka 1995 nilikuwa nagombe Ubunge na mtu alikuwa anaitwa Joseph Rwegasira, Waziri wa Mambo za Nchi za Nje, wengine walikuwa wananyonya, wengine walikuwa darasani hapa, ni wachache waliokuwepo. Kwa hiyo nina imani nimejifunza Bungeni kuna nini, watu wanafanya nini, sasa kipindi cha kung’atuka kimefika.

Kwa hiyo Mheshimiwa Waziri Mkuu nina imani Wanaruangwa watakupitisha bila kupingwa, lakini ikiwa amejitokeza yoyote kwa kukupinga kwa sababu mimi ni mstaafu, gari yangu nitakuwa nayo mpya, mafuta yapo, nitakuja kupiga kambi kwako nihakikishe unashinda na nina imani kwa ushindi wako matunda haya tunayoyaona kwa awamu ya tano si jukumu langu kusema huyo uliyenayo kwa sababu Mheshimiwa Pombe Magufuli atakuwa Rais na wewe unaweza kuendelea kuwa Waziri Mkuu, nitakuombea dua. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa nihamie kwako, mimi tulikuwa tunafahamiana kidogo si sana, lakini umenilea sana hapa Bungeni na nimejifunza mambo mengi kwako kwamba hoja sio Uspika, busara ndio kitu muhimu sana. Umejawa na busara, umejawa na huruma, yako mambo makubwa sana yanafanyika Bungeni huku kama hujawahi kukaa Bungeni itakuwa hatari, kwa maana ukiwa Spika leo umekuja jana Bunge hili haliwezi kutawalika, lakini uzoefu wako wa kuwa Mbunge ukaja ukawa Spika na wewe dua yangu naihamishia kwako kwamba nina uhakika Wanakongwa watakupitisha bila kupingwa, lakini wasipokupitisha bila kupingwa ni siku 60 nitakaa 30 kwa Mheshimiwa Majaliwa, nitahamia 30 Kongwa kuhakikisha unashinda. Ahadi zangu mara nyingi hazikai chini, ziko moja kwa moja, lakini nina uhakika na ukiwa Spika basi uendelee kipindi kingine kuwa Spika ndani ya Bunge hili. Uspika ni busara tu, ni hekima, yaani mafanikio ya miaka mitano Mhimili huu umeshiriki. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niende kwenye lile alilosema Mheshimiwa Nape. Nilibahatika kidogo wakati wa kampeni kwenye kusimamia Ilani nilikuwa natembea na bwana mkubwa aliyekuwa anagombea akakabidhiwa kijiti, yalikuwa yanasemwa yaliyo kwenye Ilani, lakini tukipata nafasi ya kukaa sehemu moja namuuliza mzee mbona umetwishwa mzigo, haya yatawezekana? Ananiambia hivi nakuahidi tena ndani mwaka mmoja yatawezekana, kweli anasema yatawezekana lakini sasa wenzangu wa Upinzani mnajua wanasema mwenye macho haambiwi tazama, reli tunajenga, meli tunajenga, maji yapo, barabara zipo, viwanda vinafanya kazi, nidhamu imerudi ndani ya ofisi zetu, nidhamu hii haikuja bure, ukipita kijijini unakuta mama yuko kwenye zahanati na chemli hakuna umeme anakesha pale kwa ajili ya kuhudumia wananchi. Hii haiji yenyewe, ni kwa sababu Mheshimiwa John Pombe amefanya kazi yake. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa niwaombe, wote tunalia corona hapa, mkakati ni nini? Mimi nakuja na mkakati wa corona, mkakati wa corona niwaombe wenzangu wa Vyama vya Upinzani wamwache Mheshimiwa Magufuli apite bila kupingwa tusiwe na uchaguzi wa Rais, pamoja na Katiba inasema kwa nini, kwa vyovyote vile nina uhakika Upinzani hawana Mgombea Urais, sasa kwa nini tutumie gharama kubwa kufanya uchaguzi wakati mshindi tunaye. Utekelezaji unaonekana, aliyoyafanya yako wazi, kipindi kile kidogo tulipata kutoka jasho alikuwa Lowassa ameenda upambe ule, sasa yuko huku? Sioni, kwa hiyo wavumilie, tusitumie hela nyingi ili zibaki tukasaidie corona, tugombee Wabunge na Madiwani. Kikubwa wakipata Wabunge wengi au wachache si wanaongeza pato, pato linatokana na Ubunge halitokani na Urais. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hawa ni rafiki zangu lakini katika hili tukubaliane tu kwamba Vyama vyote vya Upinzani nani atamshinda Mheshimiwa Magufuli, yupo jamani?

WABUNGE FULANI: Hakuna.

MHE. ALHAJI ABADALLAH M. BULEMBO: Sasa kwa nini tupoteze pesa ambapo wanaenda kushindana na jiwe, haina sababu, tuje humu tuwekeane utaratibu Mheshimiwa Magufuli aapishwe, tufanye uchaguzi wa Wabunge na Madiwani ili tupate pesa za kuwahudumia wananchi wetu katika janga la corona. Uchaguzi ni gharama kubwa, Serikali inaumia, unapofanya uchaguzi wa Rais gharama yake inatisha.

Kwa hiyo, nasema haya kwa dhati, lakini kuna wenzangu wa Upinzani watachukia, lakini siku ya mwisho atakuwa ameshinda Mheshimiwa Magufuli kwa asilimia 85 au 90, sasa ni kwa nini tupoteze muda huo? Kwa hiyo nina imani tutaungana nao tu, tunaweza tukaleta hoja tukaungana nao humu ndani, Rais tukamuacha tukaenda Wabunge na Madiwani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nikushukuru na niseme kwamba nashukuru kwa ushirikiano wa Waheshimiwa Wabunge wote, Mawaziri nimepata marafiki, nimepata maadui humu, lakini ndio maisha yanavyokwenda. Naomba kuunga mkono hoja, ahsante sana. (Makofi)