Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Freeman Aikaeli Mbowe

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Hai

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. FREEMAN A. MBOWE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuwa mchangiaji mchana huu, nami nitazungumza mambo mawili tu ya msingi.

Mheshimiwa Spika, mwaka huu au kwa kipindi hiki tunakabiliwa na mambo mawili makubwa sana katika nchi yetu, janga la maambukizi ya virusi vya Corona na baadaye mwaka huu Uchaguzi Mkuu na haya ni mambo mawili makuu sana katika Taifa.

Mheshimiwa Spika, kwanza nizungumze suala la Corona. Nazungumza kama mtu ambaye kwa bahati mbaya nime-experience tatizo hili katika familia yangu. Kwa hiyo, nalizungumza kama mtu ambaye nina uhakika na ninachokizungumza ni nini. Kwa sababu nilikuwa katika isolation mpaka leo nilipotoka rasmi, namshukuru Mungu kwa hilo, ninapenda nishirikishe viongozi na Waheshimiwa Wabunge wenzangu kitu ambacho nafikiri pengine hatujakipa uzito wa kutosha katika kukabiliana na janga la Corona.

Mheshimiwa Spika, hili tatizo ni realy, wala Watanzania wasifikiri kwamba hili tatizo linaweza likazuiwa na mipaka ya nchi yetu. Kwa hiyo, ni wajibu kabisa wa Serikali na wadau wengine wote kushirikiana katika kuhakikisha jambo hili linapewa uzito unaostahili kama ambavyo Mataifa mengine ambayo yame-experience tatizo hili yanavyopitia.

Mheshimiwa Spika, mbali na tahadhari mbalimbali ambazo zimetolewa na Serikali bado kuna uzembe mkubwa sana miongoni mwetu, aidha kwa kujua ama kutokujua, ama kufikiri tatizo liko mbali na haliko mikononi mwetu. Kwa upande wa Serikali, naomba nishauri kitu kimoja; itakuwa ni dhana ya bahati mbaya sana kufikiria jambo hili ni kazi ya Serikali peke yake. Jambo hili ni lazima lishirikishe wadau wote, lakini kwa vyovyote itakavyokuwa, lazima Serikali i-take a leading role na Serikali nina hakika ina wajibu wa ku-take a leading role. Hili ni jambo ambalo linahusu taasisi binafsi, sekta binafsi, Mashirika ya Umma, nyumba zetu za imani na ibada, tunahitaji effort ya Kitaifa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ushauri mkubwa ambao napenda kuutoa katika Bunge lako ni kuunda a National Taskforce ambayo itasimamia masuala yote yanayohusu Corona. Serikali iongeze hii taskforce, lakini ishirikishe wadau wengine, wanazuoni, madaktari, hospitali binafsi na taasisi mbalimbali za nchi ili jambo hili lipewe uzito wa Kitaifa. Lisiachiwe Serikali peke yake kwa sababu Serikali ni sehemu ya uongozi, lakini kuna wadau wengine huku nje ambao ili nao wakielimika wanaweza wakajua na wakaisaidia Serikali katika kufikia malengo yake. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hili tatizo la Corona ni kubwa sana na watu wengine mpaka sasa hivi wanaliona kwamba kwetu halijawa kubwa kwa sababu pengine watu wengi wakaathirika na wakapata maafa, lakini ukweli maafa ya Corona tayari yameshaingia katika uchumi wetu. Nilitegemea sana katika bajeti ya mwaka huu Serikali ingekuja na mpango maalum kabisa wa kibajeti na kutoa taarifa katika Bunge hili kwamba hivi tuna athari kiasi gani za kiuchumi zinazotokana na janga la Corona? Ukiangalia mipango ya Serikali mpaka sasa hivi, labda yatabadilika baadaye, bado mipango iko kama business as usual, bajeti ziko pale pale, hatuja-foresee kushuka kwa mapato makubwa sana ya Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa mfano, Sekta ya Utalii ambayo ni sekta inayoingiza mapato makubwa ya fedha za kigeni, hii sekta imeanguka kabisa, yaani hii kwa asilimia 99. Hoteli zimefungwa, kampuni za tour zimefungwa, facilities zote za kitalii zimefungwa, mashirika ya ndege ya Kitaifa na Kimataifa haya-operate. Hali hii haita-recover baada ya wiki mbili, hili anguko la kibiashara kwenye upande wa utalii, impact yake ni mwaka mzima, kwa sababu wageni wame- cancel booking mpaka Desemba, mpaka new year. Kwa hiyo hili siyo jambo la leo au kesho. Ni lazima Serikali iweze ku- foresee haya mambo.

Mheshimiwa Spika, tunapojadiliana bajeti hapa, mpaka sasa hivi katika bajeti za nchi utaona kwa kiwango kikubwa sana utekelezaji wa mipango mingi ya Serikali ulikwama njiani kwa sababu ya mapato kuwa kidogo. Sasa bado tunakwenda kuangusha mapato zaidi.

Mheshimiwa Spika, biashara zinaanguka, foreign direct investments sasa hivi zitakuwa almost suspended kwa mwaka mwingine mmoja, misaada kutoka nchi mbalimbali ambazo zilikuwa zinatusaidia nina hakika zitapunguza misaada kwa sababu ya hali yao wenyewe katika nchi zao; uwekezaji wa ndani vilevile sasa hivi umeingia katika mashaka makubwa; uagizaji wa bidhaa kutoka nchi za nje ambao unachangia kwa kiwango kikubwa sana mapato ya Serikali, unaanguka; mashirika na makampuni mengi yatafunga kazi na wafanyakazi watakuwa retrenched, lakini sijaona hili jambo likichukuliwa uzito wa kutosha kwenye bajeti yetu ya nchi.

Mheshimiwa Spika, kama tunaendelea na kufanya mipango yetu ya bajeti vile vile kama vile hakuna tatizo lililotokea, wakati tuna-expect mapato ya Serikali yataweza kupungua almost by 40% katika kipindi cha miezi sita ijayo, tunawezaje kutekeleza bajeti zetu za kiserikali? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hili ni jambo ambalo nilitamani sana Mheshimiwa Waziri Mkuu atusaidie, Mheshimiwa Waziri wa Fedha atusaidie tuwe na mipango ya pamoja na wala tusione aibu katika kukabiliana na janga la Corona. Ni vyema tukajiandaa mapema kwa kutafuta mitigation factors gani zifanyike ili kujaribu kupunguza hili tatizo.

Mheshimiwa Spika, inawezekana tukalazimika kuacha baadhi ya miradi yetu mikubwa ambayo tunaipenda. Tunaipenda sana na tungetamani ikamilike, lakini inawezekana kabisa kabisa tukashindwa ku-fund miradi hii kwa sababu mapato ya Serikali ni lazima yatashuka. Kama tunadanganyana kwamba mapato ya Serikali hayatashuka, siyo kosa la mtu yeyote, ni kosa la ugonjwa huu na ni lazima tukabiliane na hali hiyo.

Mheshimiwa Spika, wakati huo huo tukichukua tahadhari hizo, ni lazima tuongeze fungu kubwa la fedha kwenda katika facilities mbalimbali zinazotoa huduma kwa wananchi hasa mambo ya kiafya. Kuwaambia watu wanawe tu mikono; tunaona information ambazo ni contradictory. Wakuu wa Mikoa wanatoa matamko mbalimbali na maelekezo mbalimbali, watu waendelee kukusanyika na kufanya kazi.

Mheshimiwa Spika, sasa tunajiuliza, Serikali mbona inakuwa na kauli mbili mbili! Kuna mikusanyiko tunaiona kwamba haifai, siyo ya lazima kwa tafsiri ya Serikali, lakini kuna mikusanyiko ya ghafla, Wakuu wa Mikoa wenyewe wanafanya majumuiko ya watu, wanakusanya watu, wanahutubia watu, wanawaambia watu Corona iko mbali. Haya ni mambo ya hatari. Sasa Serikali inasema nini? Tumsikilize nani?

Mheshimiwa Spika, natamani tumsikilize Mheshimiwa Rais wa nchi, ningetamani tumsikilieze Mheshimiwa Waziri Mkuu na Mheshimiwa Waziri wa Afya. Hawa ndio mamlaka ambazo tumeambiwa zitatoa kauli kuhusiana na ugonjwa wa Corona. Sasa kila Mkuu wa Mkoa na kila Mkuu wa Wilaya anakazana kutafuta kutoa maelezo katika maeneo yake. Mimi nafikiri hii nchi tukienda hivi huu ugonjwa utatupeleka mahali pabaya sana.

Mheshimwa Spika, katika hili la Corona, ni bora tujiandae hata kama tunaona janga liko mbali ili janga likifika tukute tumejiandaa kuliko kutokujiandaa tukafikiri liko mbali halafu likafika, litakuwa fedhea kwa nchi. Na lazima tujifunze kwa nchi za wenzetu, jamani sisi hatuishi wkenye mipaka na siyo vibaya kujifunza kwa wenzetu siyo siri hili tatizo limekumba dunia, hebu angalieni wenzetu wa Rwanda wanafanya nini, tuangalie wenzetu wa Kenya wanafanya nini, hawa wenzetu siyo wajinga na mipaka yetu sisi ni ya jamiii hiyo moja Kenya na Tanzania jamii ni hiyo hiyo moja na Uganda na Rwanda. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa nitake nisisite kwamba hili jambo linahitajiwa kuundiwa national task force tuanze kuangalia athari za kiuchumi, athari za kijamii, tufanye nini tuache nini, hatuwezi kuendelea na mipango yote kama tunavyofanya siku zote hiki ni kipindi cha prioritize, yaani tuamue priority za Taifa katika kipindi hiki cha corona ni nini, lazima tu suspend baadhi ya mipango ya Serikali ili kuwezesha kukabaliana na tatizo ambalo linajitokeza.

Mheshimwa Spika, jambo la pili ningependa nizungumze kuhusiana na uchaguzi, leo tuna kama miezi tu actual process za uchaguzi zimeasha, lakini ukiangalia tumekuwa tunadai kwa muda mrefu sana, jamani tutengenezeeni maridhiano katika nchi tutengeneze Tume huru ya Uchaguzi. Uchaguzi ni process na hii process ni ndefu, uwandikishaji ni sehemu ya process, upatikanaji vifaa ni sehemu ya process, kurekebisha Sheria bali tunavyokidhi na matatizo ni sehemu ya process, lakini siye umekuwa tunadai minimum reform kwa sababu moja tu, kwamba tunaamini kwamba ili nchi iweze kuendelea vizuri, lazima ipate viongozi wanaopatikana kwa misingi ya kidemokrasia, tunaimani kwamba wawakilishi wananchi lazima wapatikane kwa misingi ya kidemokrasia. Ili jambo linahitaji political will wala siyo kushindana kupiga kelele. (Makofi)

Mheshimwa Spika, nimemwandikia Mheshimiwa Rais, tumesema mara nyingi tumezungumza mara nyingi katika forum mbalimbali, kwamba jamani tunaposema tunataka minimum reforms, marekebisho machache ya Sheria kwa sababu mtakumbuka 2015 wakati mchakato huu wa Katiba mpya unashindikana makubaliano na Mheshimiwa Rais wakati ule Mheshimiwa Jakaya Kikwete yalikuwa tuende basi angalau kwenye minimum reform mpaka tutakapomaliza mchakato mzima wa Katiba. Bahati mbaya ile process haijarudia mpaka leo.

Kifungu namba 74 na namba 75 katika Katiba yetu vinahitaji marekebisho machache, na haya mambo kama kuna political will upande wa Serikali haya mambo yanawezekana, tukaenda kwenye uchaguzi watu tumeridhiana, tumekubaliana, uchaguzi haki akichaguliwa huyo, akichaguliwa yule basi tupate viongozi ambao wamepatikana kwa ridhaa ya wananchi na siyo kwa giliba za mifumo ya kiuchaguzi. (Makofi)

Mheshimwa Spika, sasa Katiba ina matatizo yake mapungufu, ambayo marekebisho yake ya kufanya kwa sabau zamani minimum reforms ni machache, kifungu cha 74 na 75, halafu kuna masuala ya Sheria za uchaguzi tumeainisha Sheria mbalimbali tumeshapeleka taarifa hizi Serikalini bwana mkubwa mwenyewe kwamba kuna maeneo mbalimbali yana criminalize process zima ya uchaguzi. Kuna watu wengine wanaenguliwa kwenye process ya uchaguzi kwa sababu tu eti amekosea kuweka nukta hapa vitu kama hivyo ambavyo vinavuruga ile dhana ya kupaya viongozi bora.

Mheshimwa Spika, kwa hiyo, tunachosema sisi ni kama tunahitaji hizi minimum reform zifanyike, na nina hakika bado huo muda tunao, hata Bunge hili kabla halijaifa, kama kuna willingness na political will ya kutafuta mwafaka katika Taifa, kutafuta amani ya kudumu na maridhiano katika Taifa haya mambo bado yanaweza kufanya siyo mambo magumu ya kuhitaji bajeti maalum hapana, ni mambo ambayo yanawezekana, tumeainisha mambo chungu mzima katika Sheria ya uchaguzi na Katiba ambayo yanafaa kufanyiwa reforms ili kuwezesha jambo hili kufanyika, ahsante sana. (Makofi)