Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Peter Ambrose Lijualikali

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Kilombero

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. PETER A. P. LIJUALIKALI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa tena dakika zangu.

Mheshimiwa Spika, nilikuwa kwenye issue ya barabara ingawa ndugu yangu Kibajaji pale anasema huu siyo muda wa barabara na kwamba muda umeisha. Mimi nataka nimwambie tu kwamba mimi ni Mbunge kwa miaka mitano na nimeapa kukaa hapa mpaka nitakapofika mwisho.

Kwa hiyo, mimi nitasema mambo ya Kilombero mpaka siku ya mwisho. Mimi kazi yangu ni kusema mambo ya Kilombero. Ninyi Serikali ya CCM na Rais Magufuli kazi yenu ni kutenda yale mimi nayoyasema kuhusu Kilombero. Kwa hiyo, mimi hapa nitafanya kazi yangu mpaka siku ya mwisho. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ifike hatua kule kwenye sheria ya sifa za kuingia Bungeni kidogo zibadilike, shule pia inatakiwa itumike angalau hata form four hivi. Mambo mengine ni kutokana na shule inawezekana ikawa watu hawaelewi mazingira ya humu ndani. Kwa hiyo, niombe ifike hatua shule pia iingizwe, mtindo wa kusema kwamba tu mtu ajue kusoma na kuandika kama Taifa sasa hii issue ifike mwisho, shule itajwe form four, form six. Kama dereva wa Serikali anaambiwa lazima awe form four…

SPIKA: Dakika tatu zinaisha…

MHE. PETER A. P. LIJUALIKALI: Mheshimiwa Spika, ni bora ziishe lakini nchi ijue ukweli. Kwa sababu kama kuna Mbunge anakambia eti bwana wewe muda umeisha wakati anajua kabisa tumeapa miaka mitano…

T A A R I F A

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Spika, taarifa.

MHE. PETER A. P. LIJUALIKALI: Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, tuzingatie elimu kwenye kuchagua Wabunge.

SPIKA: Taarifa, Mheshimiwa Lijualikali naomba ukae upokee taarifa. Mheshimiwa Deo Sanga.

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Spika, naomba nimpe taarifa mzungumzaji ajue hata waliomaliza form four na wenye degree wapo failures. Kwa hiyo, form four siyo maana yake ndiyo inayokuingiza hapa. Wapo watu hawana form four lakini vichwa vyao ni sawa na mtu mwenye PhD. (Makofi)

SPIKA: Na huo ni ukweli wa maisha. Mheshimiwa Lijualikali pokea taarifa.

MHE. PETER A. P. LIJUALIKALI: Mheshimiwa Spika, issue siyo kufeli au kufaulu; kama tunasema madaktari wawe na level fulani, kama madereva wetu tu lazima wawe na form four, wewe unakaa hapa upitishe sheria za nchi, uisimamie Serikali halafu uwe tu darasa la pili au shule huna kabisa. Lazima tuitendee haki nchi yetu. Huyu nimwambie kabisa mimi sijakimbia shule, kwa hiyo, lazima tubadilishe twende kwa style hiyo, shule itumike. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, barabara ya Kilombero iwe ni mwaka huu au mwakani kwa sababu wahisani wameshatoa fedha na fedha mnazo, mimi kama Mbunge wa Kilombero nawataka mfanye kazi yenu ya kutuletea barabara yetu. Haiwezekani mmepewa fedha za bure kabisa, fedha mnazo mmekalia hamtaki kazi ifanyike kwa sababu zozote zile. Halafu Mheshimiwa Waziri alikuwa anasema suala la VAT ni suala la kitaalam tu wakati mmeshikilia mitambo ya mwekezaji, mmeshikilia mitambo ya mkandarasi asifanye kazi leo hii unasema kwamba hili suala ni la kawaida tu, maana yake nini?

Mheshimiwa Spika, nimtake Waziri iwe kesho, keshokutwa ama mwakani Kilombero tunataka barabara yetu tuliyopewa na mabeberu. (Makofi)