Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 – Ofisi ya Waziri Mkuu

Hon. Musa Rashid Ntimizi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 – Ofisi ya Waziri Mkuu

MHE. MUSA R. NTIMIZI: Mheshimiwa Spika, naashukuru mimi Musa Rashid Ntimizi huyu Ahangazi wa Tanga huko. Nashukuru kwa kupata nafasi niweze kutao mchango wangu kidogo, katika hotuba ya bajeti ya Mheshimiwa Waziri Mkuu.

Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa nianze kwa pongezi za dhati kwa hotuba nzuri na kazi nzuri ambazo zinafanywa na Ofisi ya Waziri Mkuu. Nimpongee dada Mheshimiwa Jenista Mhagama kwa kuwa kiungo kizuri sana kati serikali na Bunge letu tukufu kwa kazi zuri ambazo zinafanyika pale. Waziri wa Uwekezaji, dada yangu Mheshimiwa Ikupa na mdogo wangu Mheshimiwa Mavunde kwa kazi nzuri ambazo anafanya kumsaidia Mheshimiwa Waziri Mkuu katika kutekeleza majukumu yake mazuri kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba na mimi nichukue nafasi kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Igalula kupongeza kazi nzuri ya Serikali hii ya Awamu ya Tano waliyoifanya katika kipindi chote na sasa wanaelekea kumaliza na sasa tunaelekea kumaliaz miaka mitano. Nampongeza sana Mheshimiwa Rais kwa kazi nzuri aliyoifanya Mheshimiwa Rais amesimamia kauli zake, Mheshimiwa Rais amesimamia ahadi zake ambazo alituahidi wana Igalula ambacho kipindi chote ambacho amekuwa katika uongozi wake.

Mheshimiwa Spika, naomba nichukue nafasi hii fupi nikupongeze wewe na Bunge lako tukufu kwa kazi kubwa ambazo umezifanya mafanikio mazuri ya serikali yetu ya Awamu ya Tano yanatokana na kuungwa mkono na Bunge lako na kutekeleza na yanastahili kulifanya. Nakuongeza sana na pia nawapongeza Wabunge wote. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu amezungumzia miradi iliyotekelezwa kimkakati katika nchi yetu katika kipindi cha miaka mitano, ikiwemo bwawa na ufuaji la umeme la Mwalimu Nyerere Mradi mkubwa wa Standard Gauge, mradi wa REA, ununuzi wa ndege sisi kwa tabora maji ya kutoka Ziwa Victoria, ujenzi wa wilaya na vituo vya afya, elimu bure na kadhalika.

Mheshimiwa Spika, naomba hii miradi yote ambayo imezungumzwa hapa imeleta impart katika uchumi wetu na kuongeza ajira kubwa sana rasmi na zisizo rasmi kwa nchi yetu, watu wengi wanasema Serikali haitakangazi ajira lakini miradi hii katika utekelezaji wake kama alivyosema Mheshimiwa Waziri Mkuu imeleta ajira nyingi sana zilizo rasmi na zisizo rasmi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba nigusie miradi ambayo ni ya kimkakati aliyozungumzia Mheshimiwa Waziri Mkuu katika kutoa ushauri ili iweze kuboresha huko tunakokwenda mbele. Nikianzia katika eneo la kilimo kwa haraka haraka pamoja na kwamba tunaporesha miundombinu yote hii yote ambayo tumeitaja ya reli, kutengeneza mradi wa umeme, REA na kadhalika inaenda ku-effect kwenye kilimo chetu. Lakini yapo mambo ambayo tunatakiwa tuyafanya ili kusaidia kilimo ambacho kinachangia wa asilimia 29 ya GDP ya nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, ukiangalia suala la miundombinu la umwagiliaji ni eneo ambalo hatujaliwekea msisitizo sana.

Niombe Wizara ya Kilimo iliangalie hili eneo ili tutakapoboresha miradi hii ya umwagiliaji itaenda kusaidia uchumi kama onavyoona eneo hili la kilimo linasaidia katika asimilia 29 katika GDP. Tukirekebisha miundombinu ya uwagiliaji na hakika tutaongeza upatikanaji wa chakula na mwisho wa siku wananchi wetu wakulima tutawasaidia.

Mheshimiwa Spika, lakini hapo hapo tuangalie masoko ya mazao yetu ya kimkakati ikiwepo Tumbaku, Kahawa, Korosho, na Pamba. Tuangalie bei ya mazao haya, tuangalie soko la mazao haya tuangalie upatikanaji wa pembejeo ya mazao haya hapa nazungumizia tupate mbolea kwa wakati mbolea ya kupandia ije wakati wa kupanda, mbolea ya kukuzia ije wakati wa kukuzia. Lakini pia tuongeze ruzuku kwenye mbolea ili kushusha bei ya mbolea iweze kumsaidia mkulima. Lakini vile vile usimamizi wa vyama vya msingi ushirika ili mwisho wa siku mkulima aweze kupata tija.

Mheshimiwa Spika, naomba nizungumzie suala la miundombinu ya barabara, unapozungumzia ukuaji wa kilimo unazungumizia masoko yake unazungumzia na bei yake. Kama barabara zetu za kijiji hazipitiki mwisho wa siku bei ya mazao haya bei inakuwa ndogo au itakuwa kubwa mwisho wa siku mkulima hatopata faidi. Gharama za usafirishaji zitaongeza na mwisho wa siku hata mazao yanaweza fika sokoni yakiwa yameharibika. Niombe tuiongezee TARURA uwezo wa kifedha ili mwisho wa siku tuweze kutengeneza barabara hizi zisaidie mkulima huko kijijini. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba naomba kidogo nizungumzie kidogo REA, REA inafanya vizuri nipongeze kwa kazi nzuri inayofanyika. Maeneo yetu ni makubwa changamoto zake ni nyingi lakini wanajitahidi wanafika maeneo mengi kwa hili kabisa naomba nitoe shukrani za dhati kwa miradi ya rea inayofanyika. Lakini ninachotaka ni shauri hapa zipo changamoto ndogo ndogo. Vipo baadhi ya vijiji ambavyo vinarukwa, vipo baadhi ya vitongoji ambavyo vinarukwa basi haya mapungufu yaweze kufanyiwa kazi, na serikali iweze kutoa fedha kwa REA kutekeleza miradi yake.

Mheshimiwa Spika, kwenye eneo la afya nipongeze kazi kubwa ya ujenzi wa hospitali za wilaya nipongeze kazi kubwa ya ujenzi wa vituo vya afya, nipongeze kazi kubwa inayofanya ya kuleta madawa n.k. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, katika hili eneo nataka nishauri kitu kimoja tusisahau ujenzi wa zahanati, wananchi wamechangia kujenga zahanati lakini mwisho wa siku hatujawasidia vya kutosha. Rufaa yakutoka zahanati inaenda kituo cha afya, kituo cha afya inayo hospitali ya wilaya then hospitali ya mkoa. Tusiporekebisha huku kwenye zahanati tunakapatikana zahanati za kutosha na huduma zikawa nzuri tutakuwa tuna mapungufu kidogo katika utoaji wa huduma za afya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, yapo mambo mengine nitazungumza kwenye sekta husika lakini nataka nimalizie moja, la watendaji wetu wa vijiji na kata. Hawa ndio wasimamizi wakubwa wa maeneo yetu ya maendeleo katika maeneo ya vijiji. Nilikuwa nashauri la kwanza tuwatafutie usafiri wa ukakika wa kufanya shughuli zao ikiwe hata pikipiki. Lakini na pili watendaji wa vijiji wanajenga nyumba za waganga lakini wao hawana nyumba za kuishi. Watendaji wa kata wanajenga nyumba za waganga lakini wao hawana nyumba za kuishi. Tujenge nyumba za watendaji hawa tuwapatie usafiri mwisho siku wasimamie vizuri miradi katika maeneo yao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nilitaka nichangie hayo naunga mkono hoja ahsante sana. (Makofi)