Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue fursa hii kwanza kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijalia uhai na kuweza kuchangia bajeti hii. Katika hatua hii nipende kuwapongeza Waheshimiwa Mawaziri wote pamoja na watendaji wote kwenye wizara hii kwa kazi kubwa wanayiofanya kwa kufanya uchumi wa nchi yetu uweze kukua vyema na huduma za jamii kuimarika. Mawaziri kwa utendaji wao uliotukuka ndiyo sababu ya Mheshimiwa Rais kuwaamini kuendelea kuhudumu kwenye Wizara hii muhimu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kusema kweli bajeti hii kwa kaisi kikubwa imekwenda kujibu changamoto mbalimbali kwenye jamii yetu, kwani hakuna bajeti inayoweza kujibu shida za watu wote kwa asilimia 100. Hii ni bajeti iliyozingatia maoni mengi ya Wabunge wakati wakichangia bajeto ya wizara mbalimbali.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuzingatia umuhimu wa ujenzi wa Tanzania ya viwanja hivyo ni jambo muhimu sana kuimarisha sekta ya kilimo. Tunapokwenda kuimarisha kilimo cha mazao ya kimkakati, nashauri Serikali kuendelea kuwekeza kwenye mazao ya mbegu za mafuta ya kula kama alizeti, ufuta, nazi na mchikichi, hii itatupunguzia uagizaji wa mafuta ya kula. Pamoja na mazao ya jamii ya mikunde kwani pamoja na hayo mazao hayo husaidia kukuza vipato vya jamii husika na katimaye kwa nchi nzima.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na changamoto za pembejeo lipo pia tatizo la masoko kwa mazao yetu. Hivyo, naishauri Serikali kuimarisha masoko ya mazao na kuimarisha vyama vya ushirika. Hapa naiomba Serikali kuangalia sera na muundo wa Vyama vya Ushirika kwani vyama vingi vimekuwa ni vyama vya msimj wa mazao, mavuno ua mazao yakiisha na vyama husika huwa likizo na vingi havina uwezo wa kujiendesha wala watumishi wenye weledi.

Mheshimiwa Naibu Spika, utalii Kanda ya Kusini bado haujapewa msukumo wa kutosha kwani viko vivutio vingi Kanda ya Kusini Mikoa ya Lindi na Mtwara havijatangazwa. Ukanda wa Kusini tunahitaji geri la utalii wa picha kwa Pori la Akiba la Selous, kwani utalii wa uwindaji hauna nguvu kwa sasa. Mfano Wilaya ya Liwale pamoja na kupakana na Selous hakuna manufaa ya moja kwa moja jwa watu wote, lakini pia Liwale kuna Boma la Mjerumani ambalo halitangazwi kabisa.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Sera ya kuunganisha mikoa yetu kwa barabara za lami likapewa msukumo wa kutosha, kwani bado kuna mikoa bado haijaunganishwa kwa barabara hata za changarawe. Mfano Mkoa wa Lindi na Morogoro katika Wilaya za Ulanga na Liwale. Barabara ya Nangurukuru- Liwale ni barabara iliyotajwa mara nyingi hata kwenye ilani ya Chama Cha Mapinduzi. Hivyo naiomba Serikali ikafikiria kuijenga barabara kwa kiwango cha lami ili kuinua uchumi wa watu wa Liwale na Kusini nzima kwa ujumla.

Mheshimiwa Naibu Spika, niipongeze pia Serikali katika kuimarisha miundombinu ya afya kwa ujenzi wa vituo vya afya, hospitali za wilaya, hospitali za mikoa na zile za rufaa sambamba na upatikanaji wa dawa na vifaatiba, lakini bado tatizo ni kubwa hasa kwa vituo vya afya. Mfano Halmashauri ya Liwale yenye kata 20 zenye jiografia ngumu zina vituo viwili tu vya afya ambapo ujenzi wake unaendelea. Vivyo basi pamoja na shukrani kwa vituo hivyo viwili naendelea kuomba Serikali kutuongezea vituo vingine hasa vile ambavyo wananchi wameanza kuweka nguvu zao katika Kata za Barikiwa, Lilombe na Miruwi.

Mheshimiwa Naibu Spika, mradi wa LNG Lindi ni mradi wa mfano Barani Afrika nan i mradi muhimu sana kwa taifa letu hasa kwa wakazi wa Kusini, hivyo naiomba Serikali kuharakisha mazungumzo ili mradi huu uweze kuanza, kuwa na majadiliano yasiyoisha kutakatisha tamaa wawekezaji wa mradi huu.

Mheshimiwa Naibu Spika, miradi ya maji ni miradi iliyohujumiwa muda mrefu hapa nchini. Hapa naomba sasa miwapongeze Mawaziri kwenye wizara hii kuwa hatua walizoanza kuchukua. Iko miradi mingi sana ya maji imesimama, mfano katika Halmashauro ya Liwale yenye vijiji 76 ni vijiji 10 tu ndivyo vijiji vyenye miradi ya maji iliyokamilika, vijiji 14 miradi imesimama na vijiji 51 havina maji kabisa. Hivyo naishauri Serikali kupitia miradi yote iliyosimama ba wahusika kuendelea kuwachukulia hatua kwa mujibu wa sheria. Viko visima 28 Liwale vimechimbwa lakini havina mtandao wa mambomba, hivyo wananchi kukosa huduma ya maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuendelea kusambaza mifugo nchi nzima ni lazima liangaliwe upya ni bora kuimarisha ufugaj wa kisasa kuliko hivi sasa wafugaji wanasambaa nchi nzima. Mfano, Wilaya ya Liwale yenye misitu ya asili sasa inaanza kutoweka kutokana na wafugaji kuvamia mapori bila mpangilio matokeo ya haya licha ya kusambaza mifugo tunasambaza pia mapigano ta wakulima na wafugaji.