Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Augustino Manyanda Masele

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. AUGUSTINO M. MASELE: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hutuba ya Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango. Hotuba hii imejaa majibu ya kero mbalimbali za wananchi katika sekta zote muhimu za kijamii kama vile elimu, miundombinu, umeme, reli, barabara, maji, afya, viwanja vya ndege, bandari, madini na kadhalika. Aidha, kero mbalimbali zilizokuwa zinakwaza mazingira wezeshi katika kuvutia uwekezaji nchini Serikali imekuwa ikichukua hatua mbalimbali kuhakikisha vikwazo vilivyokuwa vinasababisha mazingira magumu kuvutia wawekezaji kuja hapa nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, kodi mbalimbali na tozo zilizokuwa zinakwamisha uwekezaji katika sekta mbalimbali, Serikali imechukua hatua kwa kukutana na wadau ana kwa ana. Kwa mano, Mheshimiwa Rais amekuwa akikutana na wadau muhimu katika sekta za madini na wafanyabiashara kutoka sehemu mbalimbali ambapo katika mikutano yote ambayo Mheshimiwa Rais amepata fursa ya kukutana ana kwa ana na wadau kero za nyingi zimetatuliwa na kurejesha imani ya wafanyabiashara kwa Serikali yao.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imewekeza kwa kiasi kikubwa katika miundombinu wezeshi, kwa mfano Serikali imeweza kuanza ujenzi wa Reli ya Kati kwa kiwango cha kimataifa standard gauge (SGR) ujenzi wa Reli hii ukikamilika utachangia kwa kiasi kikubwa uboreshaji wa huduma katika bandari ya Dar es Salaam ambayo ni bandari muhimu kwa nchi ambazo hazipakanina bahari za Uganda, Rwanda, Burundi, Malawi, Zambia, Jamhuri ya Kidemocrasia ya Mashariki.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, uwepo wa SGR katika Tanzania itakuwa ni ukombozi wa moja kwa moja katika ukuaji wa uchumi kwa ujumla katia kusafirisha watu na mizigo ambapo huduma za usafirishaji utasaidia kupatikana kwa vitu na vifaa kwa bei nafuu na hivyo kudhibiti mfumko wa bei nchini kwani maeneo mengi reli hii inapitia katika mikoa mingi hapa nchini. Pia Serikali imeanza kuchukua hatua kuifufua reli ya Kaskazini lengo ni lilelile la kujenga uchumi kwa usawa katika nchi yetu katika maendeleo ya watu na vitu.

Mheshimiwa Naibu Spika, huduma za afya zimeboreshwa kwa kiasi kikubwa ambapo vituo vya afya vingi vimejengwa na kukarabatiwa zikiwemo hospitali za wilaya na mikoa na zile za rufaa, ambapo watanzania wanapata huduma hizi muhimu na kuweza kupunguza kupeleka wagonjwa nje ya nchi kwa gharama kubwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, viwanja vya ndege vingi vimeendelea kujengwa pamoja na Serikali kununua ndege mpya ambazo zitarahisisha usafirishaji wa watu na vitu hasa watalii. Utalii ni sekta muhimu katika kuchangia katika kukuza uchumi kwa kuwa chanzo kikubwa cha fedha za kigeni nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuanza kwa ujenzi wa mradi mkubwa wa umeme wa maji katika bwawa la Stieglers Gorge utakaozalisha megawatts 2115 ni mwelekeo sahihi katika kuelekea Tanzania ya Viwanda. Kukamilika kwa mradi huu mkubwa tunayo imani kubwa kuwa tatizo ka mgao wa umeme litakuwa limepata ufumbuzi wa kudumu.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunaipongeza sana Serikali kwa kutekeleza kwa vitendo kuhamisha Makao Makuu ya Serikali kuja Dodoma na kuweza kufanikiwa kukamilisha ujenzi wa Ofisi za Wizara mbalimbali katika Mji wa Serikali Mtumba hapa Dodoma. Nasi tunaipongeza Serikali kwa kuipatia fedha Wilaya ya Mbogwe ili iendelee na ujenzi wa majnengo ya Ofisi za Mkuu wa Wilaya na jengo la Halmshauri ya Wilaya ya Mbogwe.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunayo maombi kwa Serikali kutoa fedha kwa ajili ya unejzi kwa kiwango cha lami kwa barabara ya Butengolumasa, Iparamasa, Mbogwe, Masumbwe, Mwabomba, Nyankende, Bugomba na Ulowa, Ulowa hadi Kalina ili kuwa chachu ya maendeleo katika maeneo ambako barabara hii inamoitia.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuunga mkono hoja ya Mheshimiwa Waziri wa Fedha ba Mipango.