Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Omar Abdallah Kigoda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. OMAR A. KIGODA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naunga mkono hoja, pili niwapongeze Mawazili wote wawili na watendaji wao kwa bajeti zuri waliyowasilisha. Mimi nataka kujikita kwenye ushauri kuhusu suala la mwananchi kutoa mizigo bandarini mwenyewe. Niimpongeze Serikali kwa kuleta utaratibu huu, hii itasaidia sana kwa mwananchi kupunguza gharama kubwa zitokanazo na makampuni ya clearing.

Mheshimiwa Naibu Spika, ushauri wangu ni kwamba Serikali lazima itafute utaratibu au mpango ambao utamsaidia huyu mwananchi kutoa mizigo yake. Ikiwezekana kuwe na one stop center kwa huyu mwananchi aweze kufanya utaratibu wote eneo moja na kumaliza kila kitu na kupata mzigo wake. Niliona utaratibu kama huu Oman.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.