Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kushauri mambo kadhaa katika Wizara hii muhimu katika maendeleo ya nchi yetu ili kuleta tija kwa kizazi hiki na kizazi kijacho, kuboresha maslahi ya Walimu kulingana na umuhimu Mwalimu katika kuboresha elimu nchini ni lazima Mwalimu aweze kulipwa stahiki zinazostahili kulingana na hali halisi ya maisha kwa sasa. Kulipa madai ya Walimu kwa wakati kulingana na Sekta ya Elimu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Walimu wanapocheleweshwa kulipwa madai yao kwa wakati inapelekea Walimu wetu wengi kukosa utayari wa kufundisha kama ilivyokuwa mwanzo, wanakata tamaa. Mfano, Manispaa ya Sumbawanga iliyoko Mkoa wa Rukwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na tabia ya kutowalipa Walimu pesa ya likizo na kupelekea kuona kama wanatengwa. Suala la Afisa Elimu kumwadhibu Mwalimu, hali hii imeendelea kuonyesha manyanyaso makubwa kwa Walimu wetu kwa mfano dalili iliyojitokeza hivi karibuni katika Wilaya ya Sumbawaga Mkoa wa Rukwa. Serikali inachukua hatua gani kwa Afisa Elimu huyu?
Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kuleta ufanisi katika Wizara ya Elimu katika Taifa letu, suala hili la kodi kwenye Wizara hii imepelekea ada kuwa kubwa zaidi na hivyo Watanzania wa hali ya chini kushindwa kumudu katika ada husika. Mwingiliano wa Wizara kuwa na chanzo cha tatizo kutokana na changamoto nyingi zinazowapata Walimu wanafuzi pamoja na miundombinu kutokana na mambo hayo kutoshughulikiwa na Wizara moja, imekuwa changamoto.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na Kitengo cha Ukaguzi kutokuwa na vifaa vya kuweza kuwafikia Walimu na kutimiza majukumu yake na kupelekea kuleta matokeo chanya katika Wizara moja ambayo itashughulikia haya yote, suala la mikopo katika Elimu ya Chuo Kikuu kuna vigezo gani vinavyotumika kutoa mikopo hii ambayo imekuwa na malalamiko makubwa hasa kwa watoto wanaotoka familia za kimasikini?
Mheshimiwa Mwenyekiti, TAMISEMI, upandishwaji wa madaraja katika Sekta hii ni lazima Wizara ifanye marekebisho. Suala hili linaleta mkanganyiko mkubwa hasa katika Manispaa ya sumbawanga. Hii ilitokana tu na uzembe wa vyombo husika. Hatua zichukuliwe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la Waraka Na. 5, elimu bure, liende sambamba na miundombinu, ada elekezi kulipa madai yote ya Walimu, mikopo hata kwa Walimu walioamua kujiendeleza ili kuondokana na ujinga na kukomboa Taifa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kuboresha elimu tujiulize mambo yafuatayo katika Wizara hii ya Elimu. Nini chanzo cha elimu yetu kushuka? Nini kinazuia kulipa madai ya Walimu? Kwa nini Walimu hawawezeshwi katika matibabu? Kwa nini mitaala yetu ni tatizo? Kwa nini ada elekezi leo? Lini Wizara itatoa Motisha kwa Walimu wa vijijini? Ni lini Serikali italeta mashine ya kuchakata vyeti nchini?