Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Naibu Spika, ningependa kupongeza bajeti hii kutokana na kuangalia angalau baadhi ya mambo ambayo yamekuwa kero kwa wananchi walio wengi wajasiriamali. Wajasirimali wengi walikata tamaa uanzishaji wa biashara ulioendana na kodi kabla ya biashara kuanza. Wajasiriamali wengi walimalizia mitaji yao kwenye kodi hivyo kuja na punguzo la kodi hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, ningependa kupongeza kauli ya Serikali ya kutowafungia wafanyabiashara kwani imekuwa Serikali ikipata hasara kubwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, nipende kuchangia juu ya hali mbaya ya halmashauri zetu hivyo zimeshindwa kutekeleza utoaji wa asilimia nne za wanawake na mbili za mikopo kwa walemavu pia nne za vijana kutokana na vyanzo vyote vikuu vya halmashauri kuchukuliwa na Serikali Kuu.

Mheshimiwa Naibu Spika, urejeshaji wa fedha kutoka Serikali Kuu ni mdogo hivyo kusababisha halmashauri nyingi kushindwa kujiendesha. Naishauri Wizara ya Fedha kupunguza gharama za uhamasishaji wa uhakiki wa ardhi ambao sasa hivi ni asilimia kumi imekuwa mzigo sana kwa wale ambao wananunua ardhi kutoka kwa mmiliki mmoja kwenda kwa mwingine.

Mheshimiwa Naibu Spika, niishauri TRA kukaa na wadau au wafanyabisahara kujua shida zao badala ya kuonekana kwa walipakodi wakati wa kufuatilia kodi tu.