Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. ENG. RAMO M. MAKANI: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu sanaa na burudani. Inaongoza kwa kasi ya kukua – 13.7%, lakini inachangia kidogo sana 0.3%. Tuongeze uwekezaji katika Sekta hii. Ikijumuishwa na utamaduni tuboreshe mchango katika utalii especially katika eneo la program ya urithi wa ukombozi wa Afrika elimu ya UNESCO yaani – The African Liberation Heritage Programme.

Mheshimiwa Naibu Spika, utekelezaji wa miradi mikubwa (kielelezo na kimkakati). Tuboreshe manufaa ya kukamilika kwa miradi, improve project completion benefits e.g technology transfer kwa wanafunzi na wataalam wachanga, nafasi za ajira, local materials, maintenance - for rest of the project life.

Mheshimiwa Naibu Spika, mchango wa diaspora, haujajitokeza vyema katika mpango na bajeti 2019/2020.

Mheshimiwa Naibu Spika, mapato ya kodi kupungua; mojawapo ya sababu ni biashara ya magendo katika ufukwe. Ufukwe una urefu wa kilometa 900 kutoka Tanga hadi Mtwara. Eneo la ufukwe litumike kama fursa kwa utalii wa fukwe. Mipango ipo hasa katika FYDP’s lakini ni vyema tukatafsiri kwa vitendo, iwekwe miongoni mwa vipaumbele kukamilika, Sekta Binafsi ni njia bora na rafiki zaidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, zao la korosho; mchango wa kilimo 28.3% ndiyo unaongoza katika Pato la Taifa. Mchango wa kilimo cha mazao ndiyo unaongoza miongoni mwa nyinginezo ndani ya kilimo. Korosho inaongoza mazao yote, hivyo kuboresha uzalishaji, masoko na uongezaji thamani ni muhimu. Suala la malipo ya mkulima wa korosho lishughulikiwe kama darura, hiyo itasaidia.