Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Joyce Bitta Sokombi

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. JOYCE B. SOKOMBI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kupata nafasi hii nami niweze kuchangia Hotuba ya Bajeti. Kwa mtazamo wangu bajeti hii siyo Gender Responsive Budget bali ni bajeti ambayo inamkandamizi mwanamke. Kwa nini nasema hivyo? Ni kwa sababu Serikali imerudisha ushuru kwa upande wa taulo za kike (Pedi). Hii ni kumfanya mwanamke huyu ambaye suala hili la hedhi ni la kimaumbile na lazimishi, kwa nini nitozwe kwa sababu hii ya kupata hedhi?

Mheshimiwa Naibu Spika, nipende kuishauri Serikali iweke ruzuku na bei elekezi kwa wafanyabiashara wa pedi kwani bila kufanya hivi wafanyabiashara hawa kila mtu ajipangie bei yake itakuwa shida kwani pakiti moja ya pedi inauzwa Sh.1,500/=, ukiongeza hili ongezeko la thamani ambalo ni Sh.1,646.7 ambayo ni 1,647 x 18% ya VAT/100 = 296.406 or 297.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hivyo 1,500 + 297 = 1,797 kwa kila pedi moja ya bei ya chini ambayo ni 1,500/=. Hii ni bei ya zamani tukiongeza ongezeko la thamani ya sasa pedi moja itauzwa kwa bei ya Sh.1,797.

Mheshimiwa Naibu Spika, fedha za maendeleo, kilimo ni uti wa mgongo kwa nchi yetu. Zaidi ya 75% ya Watanzania ni wakulima na katika hiyo 75% wanawake ndio wanaojihusisha na kilimo lakini cha kushangaza fedha za maendeleo tunazotenga kila mwaka kwa mwaka 2018/2019 zimetengwa shilingi bilioni 98, hii ni aibu kwa nchi na Taifa kwa ujumla ukichukulia hii ni awamu ya Serikali ya Viwanda.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hali hii ya kumkandamizi mkulima huyu kwani fedha zilizopelekwa ni 0.143% 41 bilioni, kwa kiwango hiki wanategemea watapata wapi malighafi wakati unaikandamiza sekta hii na badala yake wanawekeza kwenye vitu mfano, barabara, ndege, Stiegler’s George, tunaona ni kwa jinsi gani wanachukua hadi fedha za ziada za kwenye Kilimo, Afya, Elimu naomba itambulike kuwa watu ni kilimo, watu ni afya, watu ni elimu, watu ni maji. Mfano mzuri ni wa Abraham Lincoln alisema if you think education is expensive try ignorant kwa maana kama unafikiri elimu ni gharama jaribu ujinga.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali hii imekuwa haiwekezi kwenye elimu ndio maana tunapata changamoto nyingi kwani hakuna wabobezi wa kutatua changamoto hizi. Nipende kuishauri Serikali tuwekeze kwenye elimu ya kilimo bora chenye tija pia tuwekeze kuwatafutia wakulima masoko yenye uhakika na bei ya kutomkandamizi mkulima ili mkulima huyu afurahie kazi yake ya ukulima.