Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. ALMAS A. MAIGE: Mheshimiwa Naibu Spika, namwomba Waziri wa Fedha na Mipango wakati wa majumuisho afikirie mambo yafuatayo:-

(a) Kupunguza SDL ili kurahisisha ufanyaji wa biashara nchini;

(b) Kupunguza matumizi ya Wizara Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa kuleta mpango wa kujenga nyumba za Ofisi za Balozi zetu kwa mkopo na benki kwa dhamana. Nyumba zitakazojengwa ndani ya miaka 10 tutamaliza madeni na kuwa na nyumba zetu;

(c) Serikali ifikirie kuirudisha VETA kuwa chini ya Wizara ya Kazi na Ajira katika Ofisi ya Waziri Mkuu ili waajiri wanaochangia zaidi ya shilingi bilioni tisa kwa mwezi waone faida yake iliyokusudiwa hapo awali ya kuongeza ujuzi wa wafanyakazi. Waajiri hawaoni mantiki ya VETA kuwa chini ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia; na

(d) Suala la REA haliendeshwi vizuri katika vijiji vya Jimbo langu la Tabora Kaskazini lenye vijiji 87 na REA III (I) nimepangiwa vijiji 18. Mpaka sasa ni vijiji vitatu tu ndiyo vimewashwa, Waziri wa Nishati aje na maelezo kwa nini mradi huu unaendeshwa bila uwiano katika maeneo mbalimbali nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha pamoja na kielelezo cha nafuu ya SDL kwa nia ya kuongeza mapato kwa Serikali.