Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi, ili nami niweze kuchangia bajeti hii. Kwanza naomba nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa kibali cha kusimama jioni hii katika Bunge lako Tukufu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nianze kwa kuunga hoja mkono bajeti hii ya Wizara ya Fedha na Mipango. Naomba nimpongeze kaka yangu Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango, maarufu kama chambo kwa lugha la kiha, Naibu Waziri Mheshimiwa Dkt. Ashatu Kijaji, Katibu Mkuu Dotto, Watendaji wote wa Wizara ya Fedha kwa kazi nzuri wanayoifanya. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba uniruhusu nimshukuru Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuweza kukubali kukutana na wafanyabiashara wanaotoka katika maeneo yote ya nchi ya Tanzania. Walikuwepo watu watano-watano kutoka katika wilaya, alikubali kupokea ushauri wao, akawaruhusu kutoa mawazo yao na akakubali kuwaruhusu kuweza kutoa kero zao. Kwa niaba ya wanawake wa Mkoa wa Kigoma ambao ni wafanyabiashara na wanawake wote wa Tanzania ninamshukuru sana Rais kwa kuwaweza kutenga muda wake wa kukubali kukutana na wafanyabiashara. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niendelee kuishukuru sana Serikali kwa kuondoa tozo mbalimbali kwenye biashara mbalimbali, hatua hii itaendelea kuhamasisha wawekezaji kuweza kuendelea kuwekeza katika nchi yetu. Hii itasaidia sana kurudisha biashara maeneo mbalimbali ya nchi, ili wafanyabiashara waweze kufanya biashara yao bila kuwa na wasiwasi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, biashara nyingi zilifungwa kwa ajili ya kutokuwa na imani na watu wa TRA kutokana na wingi wa kodi na jinsi walivyokuwa wanatoza kodi kwa manyanyaso makubwa, lakini kwa hatua hii sasa wafanyabiashara wataweza kuwa na imani na Serikali yao na wataweza kufanya biashara kwa uhakika zaidi na bila usumbufu wowote. Kwa kweli, wafanyabiashara walienda kukata tama. Natokea Mkoa wa Kigoma, wengi walikuwa wanafunga biashara wanahangaika kukimbia huku na huku, ili labda waweze kutafuta sehemu ambayo hawawezi kupata manyanyaso, lakini kwa hatua hii nina amini na nina imani wafanyabiashara wataweza kuwa na hali ya utulivu na kuendelea kufanya shughuli zao. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nilikuwa naomba niungane na Wabunge wenzangu kama walivyosema na ninaomba nichangie katika maeneo matatu. La kwanza lilikuwa katika kodi, lakini la pili naomba kuzungumzia viwanda na malighafi inayotakiwa kutumika viwandani. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa viwanda kama vile walivyosema Waheshimiwa Wabunge wenzangu ni lazima kuhakikisha tunahamasisha matumizi ya malighafi zinazotokana na na mazao ya kilimo kama vile mchikichi, kahawa, pamba, tumbaku, chai, korosho, n.k. Tukijenga viwanda vya namna hii wananchi wetu wataweza kupata soko na uhakika wa soko kwa hiyo, wataweza kuzalisha kwa wingi kwa sababu watakuwa sasa wanajua wakizalisha watapeleka bidhaa zao wapi, lakini ajira itapatikana kutokana na viwanda vitakavyokuwa vimejengwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niseme kama ifuatavyo kwa mfano, katika Mkoa wa Kigoma lipo zao la mchikichi. Mkoa wa Kigoma lipo zao la mchikichi ambalo zao hilo linapatikana katika Mkoa wa Kigoma na viwanda vinavyotumia mahitaji ya zao la mchikichi vitazalisha bidhaa kama vile mafuta, sabuni, mashudu kwa ajili ya chakula cha mifugo, n.k. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, bidhaa ya mafuta, sabuni na mashudu zitatumika kwa ajili ya Wananchi wa Kigoma na Wananchi wa Tanzania, kwa ujumla. Kwa hiyo, tukizalisha kwa wingi hatutaweza tena kutumia pesa zetu za kigeni kwenda kununua bidhaa nje, tutaweza kununua bidhaa zetu za ndani ya nchi. Kwa hiyo, nilikuwa ninaiomba Serikali kwa vile sasa Kigoma inaanza kuzalisha mchikichi na kwa sababu sasa hivi wananchi wameshakuwa tayari sasa kuweza kuanza kulima kilimo cha mchikichi, ninaiomba Serikali iweze kusaidia mbegu, ili wananchi waweze kulima kilimo chenye tija. Kwa sasa mbegu ni tatizo…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)