Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. ENG. RAMO M. MAKANI: Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue fursa hii kukushukuru kwa kunipa nafasi hii niweze kuwa miongoni mwa wachangiaji jioni ya leo. Nimshukuru kwa namna ya pekee kabisa Mwenyezi Mungu kwa ajili ya afya na uzima alionipatia na kuweza kusimama hapa leo. Mchango wangu mimi ni kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza bajeti ya mwaka 2019/2020 tunayoijadili inakwenda kutekeleza mpango wa mwaka mmoja wa mwaka 2019/2020 huo huo. Huo mpango wa mwaka mmoja tunaoujadili ni sehemu ya mpango wa miaka mitano unaoendelea ambao unaisha mwaka 2020/ 2021 ambao na wenyewe pia ni sehemu ya Dira ya Taifa tuliyojiwekea tangu mwaka 2000.

Mheshimiwa Naibu Spika, Dira ya Taifa ambayo inaendelea kudumu kwa muda wa miaka 25, mipango yetu ya miaka mitano na mpango mwaka mmoja mmoja kwa miaka mitano yote tulipitisha wote kidemokrasia. Kwa kuwa tulipanga wote basi hata kutekeleza tutekeleze wote kila mmoja akiwa amesimama kwenye nafasi yake. Ikiwa katika utekelezaji tunakutana na mafanikio basi tutajipongeza na pale ambapo tutakuwa hatuwezi kufikia malengo basi tutafute sababu kwa nini hatujafikia malengo na tutatue tatizo hili. Kukaa pembeni na kulalamika haitasaidia mtu mmoja mmoja wala haiwezi kusaidia Taifa, tuweze kuangalia namna bora zaidi ya kuweza kutekeleza mipango tuliyojiwekea wenyewe. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na Dira, nataka niishauri Serikali ijaribu kuangalia kipindi ambacho Dira inadumu kwa sababu nimeangalia ya Kenya nimeona wao Dira yao iliyoko sasa inaishia mwaka 2030, Uganda inaishia mwaka 2040, Rwanda ya kwanza inaisha mwaka 2020 lakini ya kwao ina miaka 20 wakati ya kwetu ni ya miaka 25, Kenya ni miaka 22, Uganda miaka 32. Halafu hao wa Rwanda wanayo tayari kwenye mpangilio dira mpya, wanazo mbili tayari; itakayoishia mwaka 35 na itakayoishia kwama 2050, hizi ni za vipindi vifupi vifupi vya miaka 15. Je, ni vizuri kupanga Dira ya muda mrefu sana au muda mfupi au muda wa kati.

Mheshimiwa Naibu Spika, natazama pia hata malengo ya kidunia, nimeziangalia MDG’s zinadumua miaka 15, hata the Sustainable Development Goals na zenyewe pia ni miaka 15, sasa sisi Dira yetu ilikuwa ni miaka 25, hebu tujaribu kuona hapo nini kinaweza kufanyika pengine kuna namna bora zaidi ya kufanya. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, ni suala la ufuatiliaji na tathmini, naipongeza Serikali sana kwa sababu kwenye kitabu cha hotuba ya bajeti safari hii ukurasa wa 33 Serikali imezingatia sana suala hili na imeliweka vizuri kwa sababu, taarifa za huko nyuma za kina za kupitia utekelezaji wa mipango iliyotangulia zilizungumza suala hili kwamba, lilikuwa ni suala ambalo lilikuwa ni gape. Kama muda ungetosha ningeweza kusoma hiki kipengele kimoja kwenye Comprehensive Review Report for Tanzania Five Years Development Plan ile ya kwanza ya 2011/2012 mpaka 2015/ 2016.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa kwa kuwa, muda hautoshi siwezi kwenda kusoma kunukuu, lakini kifupi ilikuwa inaonesha kabisa kwamba, kukosa kufanya ufuatiliaji na tathmini ni mojawapo ya changamoto kubwa ambazo zilikuwa zikiturudisha nyuma katika kutekeleza mipango yetu. Kwa hiyo, naipongeza Serikali hatua ambayo imeichukua sasa hivi ya kuweza kuhakikisha kwamba, sasa haturidii au tumerekebisha makosa yale. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la pili kwenye uchangiaji, hili ninataka tu kurejea mchango ambao ulitolewa humu ndani na mmojawapo wa wachangiaji akiwa anazungumzia mradi mmojawapo kati ya miradi ya kimkakati, mradi wa reli ya kati ambayo inaboreshwa kwenye kiwango cha Standard Gauge. Alisema mchangiaji mmoja kwamba, hakuna jipya, mbona hii nchi ina Standard Gauge Railway tangu mwaka 75/76 na ambayo ilijengwa na Nyerere na kaunda. Kwa kifupi alionesha kabisa kutothamini, ni kama kuudharau mradi huu wa Standard Gauge Railway.

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka tu niwafahamishe wale ambao hawafahamu kwamba, kukamilika kwa mradi wa SGR huu tunaokwenda kuujenga sasa hivi kunakwenda kuifanya Tanzania kuingia kwenye kundi la nchi ya pili kuwa na speed train katika Afrika. Tuna treni moja tu ambayo inakwenda kwa kilometa 320 kwa saa, iko Morocco, lakini baada ya hiyo zinazofuata zote ni 160 kilometres per hour ambayo ndio sisi tunakwenda kuifikia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, mradi huu ni mradi mzuri, ni bora na ni muhimu. Na kifupi tu ni kwamba, uchukue tu mfano kwamba, maana yke, tafsiri yake ni nini ya haraka ni kwamba, watu wanaweza kutoka Dar-es-Salaam na kufika hapa Dodoma ndani ya saa pungufu ya tatu au wakichelewa sana saa tatu. Ni sawasawa na mtu atakayekuwa anasafiri kutoka mojawapo ya vitongoji vya Dar-es-Salaam kwenda katikati ya mji kwenda kufanya kazi kwa siku. Maana yake utaokoa muda kwa hiyo, utaongeza tija katika uzalishaji kwa sababu watu watakuwa wanakwenda kwa haraka. Kwa hiyo, naishauri Serikali iendelee kuongeza kasi ya kutekeleza mradi huu kwa haraka kwa sababu ni mradi wa manufaa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jabo langu la pili la kuchangia ni nafasi ya lugha ya Kiswahili katika kutekeleza miradi ya maendeleo au katika kuharakisha maendeleo ya nchi. Historia ya nchi hii inatuambia wazi kabisa kwamba, hata tulipokuwa tunatafuta uhuru mojawapo ya silaha ambayo inatamkwa waziwazi kabisa kwamba, ilitumika na ikasababisha tukapata uhuru kirahisi na pengine mapema sana ni lugha ya Kiswahili. Kwa hiyo, maana yake ni kwamba, ni vema kwenda na Kiswahili pia, hata katika hatua ya kutafuta maendeleo, umefanya vita ya kutafuta uhuru, sasa fanya vita ya kutafuta maendeleo kwa kutumia lugha ya Kiswahili.

Mheshimiwa Naibu Spika, sababu gani, Kiswahili kinaelimisha, Kiswahili kitarahisisha kutoa taarifa kwa watu, kitaunganisha watu pamoja na pengine niweze kunukuu tu msemo mmoja wa Kingereza unasema, if you want to go fast go alone but if you want to go far go together, maana yake wengi kwa pamoja ndio mnaweza mkafanya jambo la kudumu, sustainability. Sasa kama unataka kufanya jambo la kudumu lazima ushirikishe watu wengi. Watu wengi mnawezaje kuweza kuwasiliana vizuri, ni kwa kutumia lugha ambayo kila mmoja ataielewa.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)