Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Seif Khamis Said Gulamali

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manonga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. SEIF K. S. GULAMALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuwasilisha mchango wangu katika sekta hii. Napenda kuwasilisha mawazo yangu juu ya elimu hasa katika kupanga ada elekezi katika shule binafsi. Ni kweli nchi etu imekuwa na utoaji wa elimu ya Serikali na sekta binafsi katika shule za Serikali. Hilo liko wazi katika ada kwani ni bure, lakini shule binafsi ni shule ambazo wazazi hupeleka watoto kwa matakwa yao bila kulazimishwa na mtu yeyote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwangu mimi siyo tatizo kwa ada wapangazo, tatizo langu, naiomba Serikali ifuatilie kwa kina kama ada watoazo ni sawa na huduma wapatazo. Maana haiwezekani ada iwe kubwa lakini mahitaji muhimu hayalingani na gharama wazilipazo. Hivyo tunaiomba Serikali ifuatilie kwa kina kama ada zinaendana na huduma zenyewe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuwasilisha mawazo juu ya ada zinazotozwa na Vyuo vyetu katika kozi mbalimbali. Mfano Chuo cha Taifa cha Usafirishaji NIT katika fani ya Aviation, ada yao ni shilingi milioni 10 ambayo kwa mtoto masikini wa Kitanzania ni bei kubwa sana ambayo hawezi kumudu. Huo ni mfano tu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vipo vyuo vingi mfano SAUTI Mwanza, AMUCTA Tabora, Tumaini University, Dar es Salaam na vinginevyo vimekuwa vikitoza ada kubwa katika fani za sheria na nyinginezo tofauti na ada katika Vyuo vya UDSM na UDOM huku vyuo hivi vikipata RUZUKU toka Serikalini. Hili halikubaliki, kwani kwa muda fulani wanafunzi wa vyuo hivi waligoma wakidai ada zishuke. Hivyo tunaomba Wizara ilitazame maradufu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuiomba Wizara kutoa marupurupu ya ziada kwa Walimu wanaofanya kazi katika maeneo hatarishi kama Wilaya za Igunga, Nzega, Uyuyi na nyinginezo ili kupunguza wimbi la Walimu kuhama katika maeneo yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Sera ya Elimu, inataka kila Wilaya kuwa na VETA, hivyo tuombe Wizara itupe support katika hatua tulioifikia ya uanzishaji wa hivyo basi, katika upungufu wetu tuiombe Wizara itupe ushirikiano katika kufukia azma ya Sera ya Elimu ya Juu na uwepo wa VETA katika Wilaya. VETA ya Manonga Wilaya ya Igunga.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Wilaya yetu tuna ujenzi wa Maabara ambapo nyingi zimekamilika lakini tatizo ni vifaa vya Maabara. Tunaiomba Wizara katika Jimbo la Manonga itusaidie vifaa vya Maabara ili iturahisishie upatikanaji wake ili wanafunzi wetu waweze kupata huduma hii ya kusoma kwa vitendo. Shule zote Kata ya Chomachenkole, Ziba, Mkinga, Simbo, Mwisi, Chabutua Ichama, Mtobo-Misana, Ngulumwa, Ndebezi, Igoweko, Mwashiku na Sungumizi tunaomba shule hizi zipatiwe vifaa vya kujifunzia ikiwa ni pamoja na vitabu vya Arts.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mapendekezo yetu tunaiomba Wizara itupandishie Shule za Ziba Sekondari pamoja na Mwisi Sekondari ili tuwe na Vidato vya Tano na Sita.
Hili linatokana na shule hizi kwamba ni za Tarafa hapo awali, lakini kutokana na kuwa mazingira ya shule hizo ni mazuri sana ikiwa na ukubwa wa zaidi ya ekari 50 kwa shule ya Mwisi na zaidi ya ekari 10 kwa Shule za Ziba, lakini pia kijiografia shule hizi zimekaa pazuri kwa kuwa tayari kuhudumia wanafunzi wa ndani ya Wilaya hata nje ya Wilaya kutokana na maeneo hayo kuwa na huduma mbalimbali za kijamii. Hivyo, kwa Wilaya yetu ya Igunga kuwa shule hizo zitakuwa zimesaidia kupunguza uhaba wa shule hasa ikizingatiwa kwamba Igunga tayari tuna Shule ya Igunga Day na Nanga.