Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nikushukuru kwa kunipatia nafasi ili niweze kuwa mchangiaji wa kwanza katika siku hii ya leo. Moja kwa moja nikiunga mkono hotuba ya bajeti kuu ya Serikali iliyowasilishwa, nikikubaliana na mapunguzo ya tozo yaliyofanyika na mabadiliko ya kanuni mbalimbali.

Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kwa kuunga mkono kufutwa kwa kodi ya ongezeko la thamani katika taulo zinazotumiwa na wanawake. Ninaunga mkono kwa sababu, kupungua kwa kodi hii wote tuliona hakukuwa na mabadiliko yoyote katika bei na Serikali ilieleza kwamba, kuondolewa kwa kodi ya ongezeko la thamani, lakini gharama ya uzalishaji iliendelea kuwa juu.

Mheshimiwa Naibu Spika, gharama ya uzalishaji imeendelea kuwa juu kwa sababu, pamba nyingi tunayozalisha, asilimia 70 ya pamba tunayozalisha Tanzania inaenda nje na asilimia 30 tu ndiyo inayobaki kutumiwa katika nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hata wale wanaozalisha nchini, ile pamba inakwenda kutengenezwa kwanza kule nje ya nchi na kurudi Tanzania ili iweze kuzalisha pedi, kwa hiyo, moja kwa moja gharama za uzalishaji inakuwa iko juu. Kwa hiyo, ninaunga mkono kufutwa kwa kodi ya ongezeko la thamani katika taulo za kike. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja ya kupunguza kiwango cha kodi ya mapato ya makampuni kutoka asilimia 30 hadi 25 kwa wawekezaji wapya wa kuzalisha taulo za kike. Ninaunga mkono kwa sababu gani, kutawezesha kuvutia wawekezaji, kutaongeza ajira, kutaongeza mapato na hata asilimia kubwa ya pamba yetu tunayozalisha itatumika nchini, pamba yetu itakayotumika nchini, gharama ya uzalishaji itakuwa chini.

Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kwa kusema, Mkoa wa Simiyu mapema mwaka 2017, tulipitisha mpango wa uwekezaji katika mkoa. Moja ya uwekezaji ilikuwa nikuwekeza kiwanda cha kuzalisha vifaatiba, vikiwemo drip za maji, pamoja na taulo za kike.

Mheshimiwa Naibu Spika,kwa nini Mkoa wa Simiyu, ni kwa sababu tunauhakika wa maji ya kutoka Ziwa Victoria, tuna uhakika wa pamba, kwa sababu asilimia 60 ya pamba inayozalishwa Tanzania inatokea Mkoa wa Simiyu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuwepo kwa kiwanda katika Mkoa wa Simiyu, pamba itazalishwa kwa gharama ndogo kwa sababu pamba hiyo inatokea mkoa huohuo, na nina uhakika kiwanda kitakapotengenezwa kitamudu soko la nchi nzima. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo hili pia limekuwa likiungwa mkono na Makamu wa Rais, kwamba Simiyu sasa tuanzishe kiwanda cha uzalishaji wa taulo za kike. Ninavyooingea, Mfuko wa Wafanyakazi umeonesha nia ya kujenga kiwanda katika Mkoa wa Simiyu, Mfuko wa Bima ya Afya umeonesha nia ya kuwekeza kiwanda. Ninachoomba ni commitment ya Serikali; kwamba watakapokuja kujibu watupe uhakika ni lini sasa kiwanda hicho kitajengwa ili tuweze kumpnguzia mzigo mwanamke katika bei itokanayo na ununuzi wa taulo.

Mheshimiwa Naibu Spika, niendelee pia kwa kuunga mkono Serikali; moja ya kipaumbele katika kuandaa mpango ilikuwa imezingatia umuhimu wa kumaliza miradi inayoendelea ili kupata matarajio tarajiwa. Vilevile naunga mapendekezo ya kurekebisha Kanuni ya 23 ya Kanuni za Sheria za Bajeti ya Mwaka 2015 ambayo inampa mamlaka Mlipaji Mkuu wa Serikali kuongeza muda wa kukamilisha miradi hiyo. Mwanzo fedha ilikuwa ikibaki mwisho wa mwaka anapewa miezi mitatu tu ili fedha hizo zimalizwe.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono si tu kwa ajili ya kuwepo fedha za kulipa walipaji ambao wanadai hati za madai, lakini hii pia itasaidia katika halmashauri za mitaa kupunguza matumizi mabaya yaliyokuwa yalifanyika kwa fedha iliyobaki. Fedha nyingi sana zimekuwa zikibaki katika Halmashauri. Kwa mfano, fedha iliyopokelewa 2017/ 2018 katika halmashauri 176, bilioni 783 iliyotumika ni milioni 521 tu; kwa hiyo asilimia 33 ilibaki mwisho wa mwaka.

Mheshimiwa Naibu Spika, halmashauri nyingi zimekuwa zikifukuzana kumaliza fedha mwisho wa mwaka na si kukamilisha miradi kwa ubora. Kwa kumuongezea muda Mlipaji wa Serikali fedha hizi zitatumika kama zilivyotarajiwa. Naomba kukiri kwamba Waheshimiwa Madiwani walikuwa wakihoji kuhusu matumizi ya fedha wanaambiwa wakubaliane kwa sababu tusipokubali fedha zitarudi Serikalini; na pale kulikuwa kuna mianya ya matumizi mabaya ya fedha za Serikali. Nikiri kwamba Serikali imeona kuongeza muda kwa sababu fedha nyingi zinaletwa mwisho wa mwaka. Kwa kuwa tunatekeleza cash budget naomba basi kuwe na time frame ya mwisho wa fedha ziletwe angalau mwanzoni mwa mwezi wa sita ili fedha nyingi zisiendelee kubaki maana yake badala yake miradi inatekelezwa kwa ubovu, ubovu, ubovu, ubovu kwa sababu ya kukimbizana kumaliza fedha.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia naomba nichangie kuhusu mapato yanayokusanywa na halmashauri zetu nikiweza kulinganisha na mchanganuo wa matumizi namna jinsi ulivyo ili sasa tuone wapi tunatakiwa tufanye ili ule mgawanyiko uweze kuleta manufaa kama yalivyokusudiwa. Mapato ya halmashauri ambayo ni asilimia 100 mgawanyiko wake bado unaleta uzito katika utekelezaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano, asilimia 40 inakwenda kwenye miradi ya maendeleo, asilimia 10 inakwenda kwa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu ile asilimia 50 inayobaki matumizi yake mengine, fedha zake ni mfuko wa Afya ya Jamii (CHF), wengine mamlakaa ya maji, kuna likizo na matibabu ya Watumishi, kuna uendeshaji wa Ofisi ya Mkurugenzi. Nasema hivyo kwa sababu gani? natafuta pale kuhusu Mheshimiwa Diwani fungu lake pale liko wapi? kwa kuwa fedha nyingi ziko allocated kwa matumizi mbalimbali. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kama hatutaona haja ya kuwasaidia Waheshimiwa Madiwani waletewe angalau posho ile ya madaraka ya mwezi walipwe na Serikali Kuu utekelezaji wa fedha za miradi ya maendeleo hautafanyika, asilimia 10 ya wanawake haitapelekwa, kwa sababu ni vigumu sana utetee asilimia 10 ipelekwe halafu fedha za miradi ya maendeleo ikafanyike wakati wewe Mheshimiwa Diwani maslahi yako hayajalipwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuunga mkono hoja nikisema sasa Wizara ya Fedha an TAMISEMI wakae wapiti ile asilimia 10 mgawanyiko wa matumizi yake. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuunga mkono hoja.