Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. ZAINAB A. KATIMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa niweze kuchangia hoja iliyopo mezani. Kwanza nianze kwa kupongeza sana jitihada kubwa zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano, jitihada kubwa zinazofanywa na Wizara katika kuleta maendeleo katika nchi yetu hii ya Tanzania, lakini kwa upekee kabisa na kwa msisitizo mkubwa sana, niishukuru Serikali kwa kuwa sikivu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hapa katika bajeti ya Wizara ya Fedha nilitaka kushika shilingi ya Mheshimiwa Waziri wa Fedha kwa sababu ya hoja ile ya kutaka Serikali iweze kutoa grace period ya miezi 6 kwa wafanyabiashara wanaoanza biashara/wafanyabiashara wapya kabla ya kuanza kulipa ile kodi ya mapato. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, na ukifungua katika ukurasa wa 84 wa hotuba utaona kwamba wamesema hapa kwamba Serikali imesema kwamba itatoa unafuu wa kutolipa kodi kwa kipindi cha miezi 6 kuanzia wakati mfanyabiashara au mwekezaji anapopewa namba ya utambulisho wa mlipa kodi. Kwa hiyo, ina maana Serikali ni sikivu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri nakushukuru sana kwa sababu hii ilikuwa ni changamoto kubwa sana ya vijana pamoja na wafanyabiashara wengine lakini ilikuwa ni changamoto kubwa sana kwa vijana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, na ukiangalia pia msingi wa kodi ya mapato (income tax). Msingi wa income tax upo kwenye faida yaani income tax inapatikana kutoka kwenye faida na siyo mtaji. Na hapo awali tuseme tu labda tuzungumzie vijana walikuwa wanakutana na changamoto gani yaani unakuta kijana anakosa ajira, hawezi kuajiriwa inabidi ajiajiri yeye mwenyewe. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa ukiacha tu kwamba unakuta kijana amesoma miaka 3 Shahada yake ya Sociology, miaka yote anafundishwa theories za Ma- philosopher mbalimbali kina Karl Marx wanasema nini na nini halafu anakosa ajira inabidi aingie kwenye biashara ambayo tukiangalia hata katika mfumo wetu au katika mitaala yetu ya elimu, bado haijatengenezwa kiasi ya kuwatengenezea msingi wa kuanzisha na kuendeleza biashara wahitimu wetu, unakuta kwamba kijana hajui anaanzia wapi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, akipambana na hiyo changamoto, anarudi tena anakutana na changamoto ya kukosa mtaji, akipambana na changamoto ya kukosa mtaji, akipata huo mtaji kwa mkopo bado anakutana na suala kwamba lazima atumie mtaji wake ule kuanza kutoa kodi kabla hajaanza kufanya biashara. Kwa hiyo, naipongeza sana Serikali kwa sababu kwa kutoa nafuu hii ya miezi sita kwa mfanyabiashara mpya kutokulipa hii kodi kwa kweli mmewasaidia vijana sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nashauri katika siku hizo za mbele, tuone kama tunaweza ku-extend hii grace period ili iweze kufikia hata mwaka mmoja kwa sababu kama nchini wanakuja wawekezaji ambao wanaweza kupewa grace period/tax holiday hadi ya 5, 3 years. Kwa hiyo, sisi wazawa wenyewe ili ku-encourage watu waweze kuwa na moyo wa kufanya startups na kwa sababu tunajua kujenga msingi wa biashara siyo jambo rahisi. Kuna mtu anaweza akaanzisha biashara mwaka mzima lakini akashindwa kuiimarisha. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tunaomba sana Serikali katika hizo siku za mbele tuangalie ni namna gani tutaongeza hiki kipindi ili kiweze kufika mwaka mmoja. Tutawa-encourage watu wawe wana moyo wa kuanzisha biashara, wasiwe na uoga lakini hii itawanufaisha sana vijana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la taulo za kike tumesikia limezungumzwa sana, imechangiwa na Wabunge mbalimbali lakini mwaka jana tuliona kwamba Serikali ilichukua jitihada ya kuondoa VAT katika bidhaa hii ya taulo za kike. Hata hivyo, tumeona jitihada hii haikuzaa matunda kwa sababu haikuleta punguzo la bei katika bidhaa hii ili kuleta unafuu kwa watoto wetu wa kike hususan wale ambao wako shuleni. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa niseme tu kwamba ninaunga mkono maamuzi ya Serikali ya kuirudisha hii VAT kwenye bidhaa hii ya taulo za kike lakini siyo hivyo tu nina ushauri. ushauri wangu ni upi, pamoja na kwamba VAT imerudishwa katika bidhaa hii ya sanitary towels hizi taulo za kike na kwa kuzingatia kwamba raw materials au malighafi zinazotumika kuzalisha bidhaa hii ya taulo za kike ndani ya nchi na zenyewe zimeondolewa ushuru wa forodha lakini naomba Serikali iweze kuondoa VAT katika raw materials zinazotumika kutengeneza hizi sanitary towels. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hoja inaweza ikawa kwamba ukiondoa VAT kwenye malighafi za kutengeneza taulo za kike ndani ya nchi, hizi malighafi zinaweza kutumika pia kwa matumizi mengine tofauti. Sasa kwa hoja hiyo, Serikali inaweza ikaangalia utaratibu wa kuweza kuwa malighafi hizi zinaagizwa kwa quarter kama vile inavyofanyika sukari za viwandani.

Mheshimiwa Naibu Spika, hii naamini kwamba ikiondolewa hii VAT kwenye hizi malighafi (raw materials) za kutengenezea taulo za kike itasaidia katika kupunguza gharama ya uzalishaji na itapunguza pia bei, lakini itapunguza bei ya taulo za kike kama Serikali itaweza kuweka na kutoa bei elekezi na kuelekeza kwamba bidhaa hii ya taulo za kike iweze kuwekewa price tag yaani kama vile tunavyoona ukinunua kwenye gazeti, gazeti limeandikwa 1,000. Kwa hiyo, hawezi mfanyabiashara akachukua gazeti akaenda kuuza 1,500 kwa sababu bei ya gazeti imeshaandikwa kwenye lile gazeti. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba Serikali iweze kuona namna gani itaelekeza na ita-regulate ili bidhaa hii ya taulo ya kike kwa sababu tunajua tayari cost of production itakuwa imepunguzwa na faida itakuwa inapatikana, wafanyabiashara wasitumie misamaha hii ya kodi kujinufaisha na kuongeza wigo wa faida yao na badala yake ile intention ya kuondoa hizi kodi iweze kuwa realized. Kwa hiyo, naomba sana Serikali iweze kufanya hivyo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, siyo hivyo tu, ushauri wangu mwingine ninaomba Serikali iangalie uwezekano wa kuweka au kutolewa kwa hizi sanitary towels katika mfumo wetu wa bima za afya (health insurance) kwa sababu sisi sasa hivi tunaelekea katika utaratibu wa kuhakikisha kwamba kila mtanzania anaweza kuwa na bima ya afya.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa katika mfumo wa bima ya afya, kinachoweza kufanyika sisi tunajua bima za afya zina madaraja na hata kwa mfano leo hii National Health Insurance Fund (NHIF) yenyewe ina kadi ya kijani, nyekundu, njano na kadi za Kibunge, hayo yote ni madaraja ya bima ya afya. Kwa hiyo, sasa yale madaraja kwa sababu tunataka hizi taulo za kike (sanitary towels) ziweze kupatikana kwa wale wenye uhitaji ambao tumeshasema hapa wenye uhitaji ni watoto wetu wa kike ambao wapo shuleni wanakosa hizi taulo za kike na kuna siku wanakosa masomo shuleni kwa kukosa vitu vya kujihifadhia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kwa muktadha huo huo, hii bima ya afya unaweza kutengenezwa utaratibu ambapo kuna madaraja ya hizi bima za afya ambayo beneficiaries wake ndiyo wanaweza ku-benefit kwa kupewa sanitary towels. Na kwa sababu hizi bima za afya anaweza akakata bima mzazi na beneficiaries wakawa familia nzima au anaweza akawa mnufaikaji mmoja yule aliyekata bima. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa kwenye ngazi ya familia inajulikana na hata zile kadi za bima, kila muhusika anapewa na particulars zake zinajulikana. Kwa hiyo, ule umri wa kuwa ni mwanafunzi na vielelezo vya kwamba huyu ni mwanafunzi vinaweza vikajulikana na Serikali na hawa wenye sifa wakawa wana utaratibu wa kupewa hizi sanitary towels kwa kila mwezi labda unasema wanapewa piece mbili. Mimi na… (Makofi)

NAIBU SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa kengele ya pili imeshagonga, ahsante sana. Mheshimiwa Rose Kamili Sukum atafuatiwa na Mheshimiwa Benardetha Mushashu, Mheshimiwa Ahmed Ngwali Juma ajiandae.

MHE. ZAINAB A. KATIMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.