Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Emmanuel Papian John

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. EMMANUEL P. JOHN: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwanza kwa kunipa nafasi na napongeza Bajeti ya Wizara ya Fedha kwa maana ya namna ambavyo imekuja na inavyokidhi mahitaji yetu na kwa namna ambavyo mapunguzo mengi ya kodi na utitiri wa kodi nyingi kwa Watanzania ambavyo zimeondolewa.

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka kusema juu ya viwanda, lakini niongezee pale kwa Mheshimiwa Selasini kwamba wakati tunafikiria kuchukua hivi viwanda kuvitaifisha, zipo benki zetu zilikopesha hivi viwanda kwa miaka kadhaa na zile pesa ziko huko na ni za Watanzania ambao wali-inject pesa zao kwenye zile benki zikatunzwa. Tutakapokwenda kutaifisha hivyo viwanda kwa ule utaratibu mzima wa kuondoka na watu wa Biashara na Viwanda watu wa Wizara ya Fedha, watu wa TAMISEMI na ule mnyororo mzima wa kwenda kuhakikisha kwamba vile viwanda vinarudi Serikalini, basi mimi nataka tuongezee kwamba tuondoke na wale watu wa benki zetu wanaokopesha wakae chini na document zao, wahakikishe wanaona chao kiko wapi na mwisho wa siku Serikali itakapochukua mamlaka ya kuvitaifisha basi na zile benki zetu ziweze kuokolewa kwa sababu tukivitaifisha na pesa za benki zilizokopesha pale ziko kule tayari ni kwamba tumesababisha benki zetu kuanguka. (Makofi)

Sasa naomba nifikirie wakati mnakwenda muongozane na hizo benki zilizokopesha ili kuweza kuokoa chao kwa sababu tayari kama mtu ameshakufa ni lazima tujue nani anadaiwa na nani alikuwa anadai ili marehemu aondoke salama. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nilitaka kusema juu ya hivyo viwanda, leo tunajenga viwanda Tanzania lakini kuna jambo moja nimeanza kuligundua kwamba inawezekana ikatufikisha pagumu. Naomba Serikali ifanye jambo moja la utafiti wa kina na ijiridhishe kwamba kuna nchi ndani ya East Africa sasa baada ya kuona Tanzania inajenga viwanda ikifika saa 5 usiku inashusha half price ya umeme ili viwanda viweze ku-produce na ile raw material na zile product zote ziweze ku-compete na bidhaa za viwanda vyetu hapa Tanzania. Serikali ilichunguze, ilifanyie kazi kwa haraka, ipunguze michakato, isijadili mara nyingi ili kuokoa viwanda vyetu tunavyovijenga sasa ili viweze kubaki salama. Vinginevyo zile products za hivyo viwanda zikiingia hapa yeye atakachofanya ataondolewa kodi, atapunguza kodi, ata- compete na viwanda vya hapa, under that competition management ya ku-manage hilo soko itakuwa kwenye competitive na hizo nchi hatutakuwa tuna-benefit kitu na mwisho wa siku viwanda vyetu vinaweza ku-collapse. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nizungumze juu ya ardhi; kodi ya ardhi mimi naona kama inakuwa kubwa. Kodi ya ardhi kwenye investment za mashamba makubwa, ranches, industrial areas, mambo mengi, naona kama kodi ya ardhi inakuwa kubwa. Naomba Serikali mliangalie hili na kwa accumulation ya madeni makubwa yaliyopo hebu ondoeni penalty na interest muone ni namna gani watu wanaweza ku-afford kulipa hizi accumulated madeni mengi ili watu waweze kukusanya na hiyo pesa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Rais amekuwa anaonesha mara nyingi, waive interest, waive penalty kwenye benki, waive kwenye kodi za Serikali, punguza haya mambo ili watu waweze kufanya kazi otherwise utakuwa unahesabu mabilioni ya pesa makubwa yaliyowekwa kwa wananchi ambayo ni unaffordable watu kulipa na badala yake mnaishia kuhesabu mabilioni ambayo hayawezi kulipika na mwisho wa siku mnaishia migogorio. Waive hii ku-simplify maisha ya watu, punguzeni hii ili watu waone namna gani ya kuweza kusonga mbele. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna miradi ya kimkakati kwenye Halmashauri zetu ambazo watu wamekuwa wana- apply wanatengeneza miradi ya kimkakati ambayo ni ya kuona ni namna gani hizo Halmashauri zetu zinaweza kujitegemea.

Mheshimiwa Naibu Spika, nasema tena, Waziri wa Fedha, hebu tufanye kazi kwa kufanya analysis kama una Halmashauri 50 au 100 zina application ofisini kwako, zimekuja zinaonesha miradi ya kimkakati, turnover ya mradi katika Halmashauri fulani inaonesha miaka mitano au kumi, lakini kuna Halmashauri uki-implement huo mradi turnover yake ku-manage huo mradi na kuleta income na kupunguza mzigo mkubwa kwa Serikali ndani ya mwaka mmoja, upi wa kuanza? Tengeneza kufata track hivi vitu kwa kuona namna gani quick return of investment uitumie hiyo itusaidie ku-support miradi hii. Leo Kiteto tuna mradi wa gulio, soko la mazao.

Mheshimiwa Naibu Spika, Waziri akitupa sisi zile pesa ambazo tumeomba kwenye soko letu la mradi ni kwamba sisi baada ya misimu mitatu tuna uwezo wa kuwa tunajitegemea kwenye Halmashauri yetu ambayo tunaweza kujitegemea hata kwa asilimia 80. Tukikupunguzia kukudai pesa za kutusaidia kama ruzuku kwa asilimia 80 ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto tumeokoa kitu kikubwa sana. Tusaidie tujenge, tutumie huo mud amfupi kurudisha hiyo pesa ambayo sisi tunajitegemea wenyewe ile pesa uliyokuwa unatuletea upeleke kwenye Halmashauri nyingine ambazo hazina miradi ya ku-survive na ku-sustain zenyewe, tutakuwa tumepunguza burden kwa Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, yapo majengo kwenye Halmashauri zetu tunajenga. Mimi nimeona tunajenga majengo makubwa sana kwenye Halmashauri zetu. Hivi kwenye hizi Halmashauri zetu tuna haja gani ya kujenga Ofisi ya Mbunge kama haya majengo makubwa ya Halmashauri yapo! Mbunge mpe vyumba viwili aweke bendera yake pale, asonge mbele na wananchi wake, tupunguze kujenga, hizi pesa tuzipeleke kwenye shughuli nyingine ambazo zinaweza kusaidia kujenga madarasa yetu. Huo ni ushauri wangu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niende kwenye mikopo ya kilimo, mifugo na uvuvi; nataka kuiomba Serikali iangalie hivi sisi tunaona kwenye nchi nyingine wanakuwa na grants kubwa zinazo-support miradi mingi kwa wananchi na mwisho wa siku hii miradi inapofanyika kwa mfano miradi ya maziwa, kuboresha wakulima, kufanya mambo ya kahawa, kuwapa mbegu za miche, korosho na kadhalika kuna a lot of grants, kwa nini Tanzania haziji? Hawa donor friends/countries wanao-inject hizi pesa na hii miradi mikubwa na kampuni kubwa zinazo-support hii kwa nini Tanzania hatuwaoni? Hebu jitahidini muwaone. Kama mnaona kwamba wachunguzeni muwaone, hizi grants zinapokuja zinasaidia wale wakulima wetu, wavuvi wetu, wafugaji wetu kufanya namna ambavyo inawezekana waweze ku-survive then wanapokuwa wana-grow ndipo unapoweza ku- introduce kiwanda kikapata raw materials, ndipo utakapokwenda ku-introduce kiwanda kikapata wanafanyakazi wengi, ndipo vijana wetu wasomi walioko mtaani watakapokimbilia. Ndiko Serikali itakapokwenda kukusanya kodi kesho kutwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, we are joking! Hapa tunafanya utani Tanzania kwenye kilimo, mifugo na uvuvi, mfugaji ukimpa ng’ombe wawili wa maziwa au ng’ombe mmoja mwisho wa mwaka ukamwambia wewe nenda TRA kalipe kodi ya shilingi 100,000 hawezi ku-feel kama alikuwa analipa kodi, it’s just a peanuts, lakini kwa nchi tunakuwa tumekusanya kitu kikubwa ambacho mwisho wa siku Serikali inapata.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba nishauri, hebu angalieni hizi grants ziende kwa wananchi, zi-supprort ku-uproot poverty iliyopo, lakini pia iwe kama chachu na ku- boost vijana wetu wasomi wanaokimbia SUA wanaenda mtaani, mwisho wa siku wanaanza kusoma kompyuta, amesoma animal science, anaanza kusoma kompyuta, sijui accounts huku amesoma kilimo (agri-business), hiyo biashara ya nini? Hebu jaribu kuona namna gani tunaweza ku-trigger vijana wetu wakaenda kwenye grassroots kwenye sekta ya kilimo na mwisho wa siku tunapo-push hii inafanya benki zetu zianze kupunguza risk ya kukopesha hawa watu kwa sababu tayari mazingira yameshaandaliwa. Kwa hiyo unapomkopesha na anaona end product ya kiwanda ipo, benki haiwezi kusita kujadili mkopo aliyeomba kwa mwananchi mkulima au mfugaji ili aweze kutoa hizo pesa na akaweza kufanya biashara wakati huo tukiendelea kukusanya kodi yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi naomba niombe mwisho tunayo mazao makubw ya biashara kama kahawa, korosho, chai, pamba na kadhalika, leo tunahangaika kila ukifanya hivi inagoma, ukifanya hivi tunasumbuka wakati tuanfikiria kucheza na haya mazao dunia nzima inatuangalia sio sisi tunaolima haya mazao peke yake. Niombe kuwe kuna uwezo wa kufikiri na kuamua haraka. Uwezo wa kufikiri na kuamua kwa muda ili tuweze kwenda na wakati kwenye haya mazao. The more you delay one month, kahawa imeshuka bei, korosho imepigwa chini, pamba hainunuliki, soko limeanguka, nchi ina-shake, naomba Serikali delayment ya vikao vya michakato ya kutomaliza kwa wakati na kuamua jambo, Serikali iliangalie sana. Wakulima wetu watakufa, watateseka, watapoteza na hatutapata income. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niombe inapotokea of anything katika business trend yoyote ile umeona kwamba soko la korosho katika mfumo wa kulinunua ime-shake hivi twist immediately, hamisha mzigo wa watu, lipa wakulima pumzika. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa mzungumzaji)