Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Bhagwanji Maganlal Meisuria

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chwaka

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. BHAGWANJI MAGANLAL MEISURIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kupata nafasi hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, Waziri wa Fedha na Mipango nakupongeza sana kwa bajeti yako pamoja na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango pamoja na Watendaji wote, kwa sababu ya hiki kitabu walichoandika basi naunga mkono moja kwa moja kwa sababu kitabu hiki kimeandika uhakika na Serikali itasimamia, Wabunge na Watanzania sote tunaunga mkono. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili, nampa hongera Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano, Dkt. John Joseph Magufuli kwa kusimamia Ilani ya CCM, amesimamia wanyonge wote Tanzania kwa kufanikisha kupunguza mambo mbalimbali kama ushuru pamoja na matatizo mengine, sekta zote amesimamia. Vilevile Rais wangu wa Zanzibar pamoja na Makamu wake wamefanyakazi nzuri Zanzibar kwa kusimamia Zanzibar nzima, maji, umeme pamoja na nyumba, barabara, nawapongeza sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nizungumzie kuhusu barabara; barabara za Tanzania zinatakiwa kuboreshwa kwa sababu wanapakia container kutoka Dar es Salaam mpaka kwenda mipakani, pamoja na mizigo midogo midogo, Serikali tunapata ushuru kutokana na mizigo, hawa watu wanapakia mizigo wanafika mpaka sehemu za Burundi, Kenya pamoja na Malawi, nashukuru sana Serikali kusimamia kutengeneza barabara iboreshwe.

Mheshimiwa Naibu Spika, Waziri Mkuu pamoja na Makamu wa Rais wamesimamia Serikali yetu, Mheshimiwa Waziri Mkuu anasimamia Mawaziri wote, Mheshimiwa Waziri Mkuu anasimamia Wabunge wote kwa kushikamana na kufanyakazi nasi tunaunga mkono.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuzungumzia kuhusu bandari ya Zanzibar na bandari ya Dar es Salaam. Mheshimiwa Rais amekwenda kutembea nchi mbalimbali na bahati nzuri tumepata Rais wa Congo amekuja kutembelea Bandari yetu ya Dar es Salaam pamoja na reli ya standard gauge. Bandari ya Dar es Salaam inatakiwa kupanuliwa kwa sababu meli moja inapita, inatakiwa kupanuliwa ili zipite meli mbili kwa pamoja, kwa hivyo nampongeza Rais na Rais wetu wa Congo wakae pamoja tupate kuiendeleza bandari yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, bandari ya Zanzibar Mpigaduri, naomba Rais wangu wa Muungano amsaidie Rais wa Zanzibar ili bandari ya Mpigaduri itengenezwe kwa sababu container nyingi zinakuja na container zetu za Zanzibar zinakwamba Mombasa na mahali mbalimbali, hivyo ninaomba Serikali yetu ya Tanzania, naomba Muungano wetu Zanzibar tupate msukumo kutokana na Tanzania, Rais wetu wa Muungano Mheshimiwa Dkt. Magufuli aisaidie Zanzibar kutengeneza bandari yetu na kuboresha kwa sababu container kutoka Dar es Salaam inakwenda mpaka Burundi, inakwenda Kenya mipaka yote basi Serikali tunaongeza kipato.

Mheshimiwa Naibu Spika, reli ya standard gauge namshukuru Rais amefikiri Mheshimiwa Magufuli kufanya kitu cha muhimu sana kwa Tanzania itapakia mali mbalimbali, biashara ndogo, biashara kubwa, container na wananchi watafaidika kwa hivyo, peleka salama kwa Mheshimiwa Rais hongera sana kwa kutengeneza reli ya standard gauge. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu viwanda, ninaomba Mheshimiwa Rais asimamie viwanda vyote. Viwanda vinatakiwa kuboreshwa kwa sababu viwanda vipo vya aina nyingi, kuna viwanda vya sukari, viwanda vya pamba, tumbaku, alizeti, pamoja na korosho na vingine. Viwanda hivyo lazima tusimamie vifanyekazi, vikifanyakazi viwanda basi tunaongeza mapato na TRA wanapata mapato. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tunakuja…

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Bhagwanji muda wako umekwisha, ahsante sana. Ahsante sana Mheshimiwa Bhagwanji. (Kicheko/Makofi)

Waheshimiwa Wabunge tunaendelea na Mheshimiwa Sophia Mwakagenda atafuatiwa na Mheshimiwa Dkt. Godwin Mollel, Mheshimiwa Injinia Lwenge ajiandae.

MHE. BHAGWANJI MAGANLAL MEISURIA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa heshima yako, naunga mkono Serikali na bajeti. (Makofi)