Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Jaku Hashim Ayoub

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. JAKU HASHIM AYOUB: Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue fursa hii kwanza na mimi kukushukuru kuniruhusu kuchangia mjadala huu ambao ni muhimu na ndio afya ya Serikali yetu, bila ya fedha huwezi kufanya kitu. Nichukue fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri na watendaji wake pamoja na Katibu Mkuu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nianze na mchango wangu kwa Serikali zetu hizi mbili ni sikivu, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Bila kupoteza muda nianze na TRA, kwa kweli siku zote Mheshimiwa Rais kama hatukujipanga watendaji wa TRA nafikiri mko ndani mnasikiliza mchango huu, siku zote atabadilishwa Kamishina, itakuwa kama kubadilisha shati siku zote. Hapa pana uwajibikaji na utendaji, siku zote suala hili lina kazi. TRA mmekuwa midomoni mwa watu/ wafanyabiashara sana lakini niwaombe panapo haki ya mtu jaribuni kuangalia haki ya mtu, tusifikie TRA kutumia nguvu za ziada kumlazimisha mtu, kuku anataga yai moja huwezi kumlazimisha kutaga mayai matatu utamkosa mpaka yule kuku, kwa hiyo hili mliangalie. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Murad alizungumza sana kuhusu Kariakoo, sasa hivi haipo limebaki jina tu, kutengeneza jina kuna kazi kuchafua ni mara moja. Kwa hali ya Kariakoo haipo, kurejesha kuna kazi sasa hivi, wafanyabiashara wengi washafunga virago kutafuta maslahi kwingine. Hili mkae na mliangalie TRA, hali si nzuri, kodi hizi zinakusanywa kwa viwango vyake na utendaji wake, tusitake kumuonea mtu wakati hana hatia.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna watu wengine wanalazimishwa wasaini kabla hajaja kupelekwa mahakamani, kosa halijulikani, kuna mtu ana kesi ya mwaka 2010 mpaka leo, sheria ya TRA inasemaje miaka mingapi kufunga file? Tusifufue maiti wakati ilishaoza, hatuwezi kufika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hoja yangu kubwa kuhusu Zanzibar kukopa hapa tutapiga kelele mpaka dakika ya mwisho Waheshimiwa Wabunge hasa kwa upande wetu wa Zanzibar. Kuna sheria ambayo ilipitishwa naomba kuinukuu ya tarehe 03 Machi, 2017; The Written Law Miscellaneous Amendment Act 2017; hii sheria kama Mwanasheria Mkuu yupo naomba akaiangalie haiko vizuri sana. Nasema kwa sababu zangu ninazozijua pamoja na kuwa na elimu yangu ni ndogo.

Mheshimiwa Naibu Spika, amendment section two “The principal Act is amended in section 2, by (a) adding appropriate alphabetical order the following of definitions:

“Consolidated Fund” means Consolidated Fund of Government refered to in the Constitution;

“On-lending” means an arrangement whereby the Government borrows from the external or domestic source and thereafter passes on the loan of another entity such as Revolutionary Government of Zanzibar, parastatal organizations, local Government of any other public body corporate.

Mheshimiwa Naibu Spika, hii sheria haiko vizuri kwa maslahi ya Zanzibar na imepitishwa hapa sijui tulikuwa wapi. (Kicheko)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo hii tuliangalie, maana yake kwa haraka SMT inaweza ikakopa SMZ kama ni mashirika au halmashauri za mjini kukopeshwa, kwa hiyo ile ndoto yetu ya Mpigaduri pana kazi kubwa sana, tuwe wa kweli wajumbe hii angalieni sheria hii ikoje? Mimi elimu yangu ni ndogo. Kwa hiyo, mkopo ule kujenga bandari ile pana kazi kubwa kwa sheria hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, haitoshi nakwenda tena mbele; The principal Act is amended by repealing section 12 and replacing for it the following; Revolutionary Government of Zanzibar may, where arrangement between the Government and the lender requires on-lending arrangement enter into on-lending arrangement with...

Mheshimiwa Naibu Spika, namba mbili; on-lending arrangement under subsection (1) shall be effected through on-lending agreement which shall, amongst other things, contain the terms and conditions of the primary kuna high and equally. Hii sheria bado ina kazi kubwa, vinginevyo tutapata matatizo sana Serikali ya Mapinduzi kukopa.

Mheshimiwa Naibu Spika, muda hautoshi lakini hii sheria ina mambo mengi huko mbele angekuwepo Mwanasheria Mkuu hapa ningemkabidhi hii ingekuwa vizuri, lakini huko mbele ina marekebisho mengine, lakini nitakuletea copy moja ili uione kuna nyingine za Government, Loans, Guarantees and Grants Amendment Act ya mwaka 2003 nayo haiko vizuri kama nitaruhusiwa kuja na hoja binafsi nitakuja nayo na naomba kuinukuu; “The Minister shall, within three months prior to the commencement of fiscal year other than the fiscal year in which this Act comes into operation, cause to be prepared for approval by the Government; an annual Debt Strategy and borrowing plain ambayo sheria hii ni ni mazonge matupu, kwa hii sheria naomba iangaliwe vizuri ili Zanzibar waanze kujikomboa na si vibaya Serikali ya Jamhuri Muungano kutokana na uwezo wako wakaifikiria Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ilikuwa na kilio tulipitisha sheria hapa ya TASAC (ya meli) lakini ninavyojua mimi mtu anapokamatwa, anatakiwa afuate sheria za sheria kama meli imekamatwa China itafuata sheria za nchi ya China, Zanzibar uchumi wake umekuwa mdogo, sasa ZMA imekuwa pale haina kazi kipindi hiki na usajili wa meli umeanza nafikiri Zanzibar kabla ya Tanzania Bara.

Kwa hiyo, mambo mengi narudia tena yale yale kwa Zanzibar imeanza mapema, kwa hiyo ifike pahali muangalie uchumi wa Zanzibar umekuwa ni mdogo, tufike pahali sheria tuiangalie ZMA imekwama kutokana na sheria ile, lakini sheria inasema meli inapokamatwa inahukumiwa na sheria za nchi, siwezi mtukakamatwa Oman akaletwa Tanzania akahukumiwa, anahukumiwa kule kule sheria na nchi hiyo, tufike pahali ili tuliangalie.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini njie na lingine niendelee kushukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuondoa VAT na hatimaye kuwa sifuri na unaweza kuomba mambo mengi, lakini ukafanikiwa moja mengine yakaja baadae, niendelee kuomba tena umeme ule walionunua Tanga Cement, Twiga Cement na baadhi ya kampuni nyingine na bei niliyonunua Zanzibar karibu almost sawa, ukizingatia Zanzibar miundombinu ni yake mwenyewe ya baharini na ikaharibika anatengeneza kwa pesa zake. Kwa hiyo, hilo nalo mlifikirie na mlichukue, huwezi kuomba mambo yote kwa mpigo ukaja ukafanikiwa kwa wakati mmoja, hili mkae na mlifikirie, hali iko mashaka na duniani kote kuna bei ya rejareja na jumla kwa hiyo hili nalo mlizingatie. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini nije kwenye suala la bidhaa za Zanzibar kuingia katika soko la Tanzania Bara; imekuwa kizungumkuti cha muda mrefu tufike pahali, hapa rafiki yangu Mheshimiwa Mwijage alipokuwa Waziri wa Viwanda na Biashara tulikuwa tukipigana vikumbo sana, leo tufikieni sukari ile ya Zanzibar pamoja na udogo wake kwani kuleta hapa kuna tatizo gani? Leo bidhaa za Zanzibar zimeingia kule hakuna question mark yoyote, leo bidhaa zinatoka Uganda, zinatoka Congo, zinatoka Zaire zinaingia bila vikwazo vyovyote. Zanzibar inategemea biashara tufike pahali napo hili mlizingatie.

Mheshimiwa Naibu Spika, nije kwnye suala la ajira za Muungano; hapa nilikuwa nikiomba kidogo papangwe formula maalum kuhusu ajira kwa sekta za Muungano, hiki ni kilio cha muda mrefu hakujawa na formula maalum mpaka muda huu. Kama ipo nafahamishwa ipo, kwa hiyo naomba nifute kauli yangu hiyo naambiwa ip, kwa hiyo ipo naomba kufuta kauli yangu hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, nije kwenye mgao wa mashirika ya Muungano iiwepo TCRA, Posta, benki NBC na kadhalika nyingine mpaka muda huu hayo mashirika hayajatoa gawio.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kumalizi nije kwenye suala la Zanzibar inategemea zaidi uchumi wake karafuu, Mungu ajalie ziweze kuzaa, lakini kukikosekana karafuu ni utalii; sasa hivi utalii umekuwa ukigwaya gwaya maana yake, ikiwemo sheria ya Wizara ya Fedha za Tanzania sheria mnazozitunga Tanzania Bara baadhi ya sheria muwashirikishe ndugu zetu wa Zanzibar, kuna sehemu zinawagusa, haziko sawa.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimesikia kengele yako imelia, ahsante sana. (Makofi)