Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Masoud Abdalla Salim

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtambile

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. MASOUD ABDALLAH SALIM: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, nichukue fursa ya kumshukuru Mwenyezi Mungu, Subhanah Wataalah anijalie uzima na afya njema, kuchangia bajeti ya mwaka 2019/2020 na nianze na Mheshimiwa Waziri kwa hotuba yake katika ukurasa wa 95 akisema kuelekea uchaguzi za Serikali za Mitaa, mwaka huu Oktoba, 2019. Akataja sifa 10 na kuna baadhi ya sifa ambayo moja ilikuwa kidogo na ukakasi na Spika akarekebisha, labda niseme kuna baadhi ya sifa ambazo uliziacha, naomba nikukumbushe.

Mheshimiwa Naibu Spika, miongoni mwa sifa ambazo tunataka kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa kuwachagua viongozi wanaofaa, awe anathamini utu wa binadamu, miongoni mwa atakayechaguliwa, lakini pia awe anatoka katika chama ambacho hakina tabia ya watendaji wake kuzikimbia fomu za wagombea wengine wanapopata fursa, akaingia mitini, hiyo ni sifa nyingine ambayo ya kuchaguliwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini sifa nyingine ambayo itakuwa ni nzuri kuliko yote, awe anatoka katika chama ambacho kinakubali kushinda, chama ambacho anakubali kushindwa pale ambapo anaposhindwa, asiwe na tabia ya kung’ang’ania na kuandaa mazingira ya amani kutoweka, akishindwa akubali kushindwa, hizo ni sifa ambazo Mheshimiwa Mpango uliziacha. Tunaomba ukija hapa uziingize sifa hizo, kwamba tunataka uchaguzi Serikali za Mitaa, sifa hizo kuzitaja uliziacha, naomba uzikubali na ninafikiri kwa unavyocheka, sifa hizi umezikubali. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naanza na bajeti sasa; bajeti hii ya mwaka huu haina uhalisia, bajeti hii ya mwaka huu inaonekana mnakwenda kutumia fedha nyingi zaidi kutokana na mchanganuo ambao umeleta, mapato/ makusanyo ya muda wa miaka miwili, tunakwenda kutumia ndani ya mwaka mmoja, yaani ukusanye fedha za miaka miwili, ambayo makusanyo yetu kwa mwaka ni trilioni 1.2, makusanyo yetu ni trilioni 1.2 kwa mwezi, lakini kwa jinsi ambavyo umetuletea matumizi yako, tunakwenda kutumia trioni 2.5 kwa mwezi, kwa sababu zifuatazo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Deni lako la Taifa unasemani trilioni 9.7; ukiangalia mchananuo kama utagawa kwa mwezi, utakuta kwamba ni lazima upate bilioni 810. Ukienda kwenye mishahara trilioni 7.558; ukiangalia je, kwa mwezi utakuta kwamba unapata bilioni 629. Ukienda kwenye matumizi mengineyo (OC) trilioni 3.576; ukienda kwa mwezi utakuta kwamba kuna bilioni 298; ukienda kwenye fedha za maendeleo, ukiachia fedha za wahisani zile, trilioni mbili pointi; trilioni 9.73, nazo lazima ukusanye upate bilioni 811, hizo ni trilioni 2.5! (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa unashangaa leo Waziri unakuja na bajeti ya matumizi ya trilioni 2.5 zipatikane, lakini unasema na makusanyo yetu sisi ni trilioni 1.2, kwa mwezi! Hiyo ni bajeti ya kiini macho, kizungu mkuti, haifahamiki, funika kombe! (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri, tunataka bajeti ya uhalisia, siyo bajeti hii, hii bajeti haitekelezeki, tunakwenda kuumiza watanzania. Mimi halafu nashangaa, namshangaa Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri wake kwamba hii bajeti, kweli haitoi jibu! Haitoi jibu kwa sababu gani, inaelekea moja kwa moja, utaratibu unaonekana, hata wafanyabishara wenyewe, kilio kila kona, maduka Kariakoo yamefungwa, uvuvi bahari kuu hauna jibu, hamkujipanga, ni kivutio kikubwa, lakini kila tukitoa ushauri kwetu sisi, mama ntilie nako ni kilio. Sasa hii ni bajeti ya aina gani mwaka huu! Bajeti hii ni kiini macho, kizungumkuti, haifahamiki. Naomba huwezi kuchukua trilioni 2.5 ambayo lazima uzipate, lakini makusanyo yako ni trilioni 1.2. nimshauri Mheshimiwa Waziri, bajeti hii ifumiliwe upya, haifai kabisaa.

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, suala la wakulima; wakulima wamekuwa na malalamiko makubwa kila wakati. Suala la korosho limekuwa ni kubwa, mmeweza, mmechukua muda mrefu, wakulima wa korosho wanalalamika, mara hii mmekwenda kuweza kuwakopa wakulima wa korosho, hamjawalipa, mmewalipa baadhi ya wakulima, baadhi ya wakulima wengine hamjawalipa na nini athari yake hii, athari yake wanashindwa kuandaa mashamba. Kama Serikali ni ya wanyonge, walipeni wanyonge wa korosho! Hata hawa wafanyakazi wa ngazi ya kati, walipeni fedha zao! (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hili ni jambo kubwa sana, lakini kama mkiendelea kutowalipa fedha zao za korosho, basi kinachoonekana, morali inashuka, morali kwa wakulima wa korosho inashuka kila siku! (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hasa mimi nawashangaa, mnasema Serikali hii ni ya wanyonge, wakulima, lakini nashangaa kwa nini hamsikii kilio tunacholia, Halmashauri zinakosa mapato!

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri andaa mazingira, andaa mazingira kwamba ni jinsi gani mtaweza kulipa wakulima wa korosho na taarifa ambazo zipo, ambazo bado hazijathibitishwa, mna mpango wa kwenda kuwalipa wakulima wa korosho kwenye mwezi wa nane na wa tisa, kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa iwe kama ni kampeni. Ndiyo taarifa zilizopo zinazozagaa, ni kawaida yenu hamuwalipi, mpaka karibu karibu ama kuna uchaguzi fulani ndiyo mnafanya ujanja ujanja, mnakwenda kuwalipa na amesema Mheshimiwa Bwege, mkiwalipa mtapigwa, hamkuwalipa mtapigwa. Kwa sababu wao wana macho wanajua wapi wanachagua. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, labda niseme kwenye miradi ya maendeleo; kwenye miradi ya maendeleo, taarifa ya miradi ya maendeleo, kwa upande za Zanzibar. Kitabu kile hakionyeshio kabisa jinsi gani ambavyo mnakwenda kutekeleza miradi ya maendeleo kwa upande wa Zanzibar, ni eneo dogo sana ambapo mmetaja. Ni sehemu moja tu ya ulinzi, kidogo tu, lakini kuna Mradi wa Mpigaduru kabisa hamkuutaja, kuna miradi kadhaa mlikwishaahidi zamani, kuna Bandari ya Wete, Bandari ya Mkoani, mliahidi. Sasa nimshauri Mheshimiwa Waziri, katika miradi yote 552, lakini ukiachia miradi ile ambayo iko katika mambo ya Muungano, hata miradi ambayo ipo katika Ofisi ya Makamu wa Rais, mabadiliko ya tabianchi, mnakwenda kujenga kuta katika fukwe, hamkutaja hata mradi mmoja kutoka Zanzibar, kwa upande wa Unguja na Pemba, hili ni jambo ambalo linatuumiza kweli.

Mheshimiwa Naibu Spika, hasa, na Mheshimiwa Waziri January Makamba, wewe unafahamu jinsi tatizo la fukwe, wewe umefika Kisiwa Panza na maeneo mengine, kwa nini katika kitabu kile hamkuonesha utaratibu wa kwenda kujenga kuta katika fukwe katika mabadiliko ya tabianchi, mmewatenga Wazanzibari, hili lazima tuliseme, tatizo nini? Niwashauri mara nyingine mtakapoandaa taarifa, basi Zanzibar muweze kuihusisha vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, katika jambo lingine ni hali ya uchumi unavyoendelea; katika hali ya uchumi unavyoendelea, kumekuwa na aina fulani ambayo inaonekana wazi wazi kwamba ni kwanini baadhi ya benki zinafungwa! Serikali imekaa tu, kuna benki ambazo zimefungwa, unaifuata benki, imefungwa, kuna Kagera Farmer Cooperative Bank,imefungwa, Benki ya Wakulima imefungwa, lakini hata Benki ya Wanawake, nayo imefungwa! (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ni sababu zipi za msingi ambazo zinaonekana kwamba kuna kuwa na mdororo huu wa uchumi! Moja ya sababu inaonekana Benki ya Wanawake kufungwa, taarifa ambazo tunazo ni kwamba Serikali iliahidi kuboresha Benki hii ya Wanawake, lakini fedha hamkupeleka! Sasa kwa nini msipeleke fedha na mnasema kwamba wanawake kwanza, tunawajali mama zetu, hawa ni wazee wetu, kwa nini basi mlipelekea mpaka Benki hizi, Benki hii ya Wanawake kufungwa...

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)