Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Sebastian Simon Kapufi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, awali ya yote na mimi naomba nianze kwa kuunga mkono hoja. Nimshukuru Waziri, Naibu Waziri na watendaji wote ndani ya wizara, lakini naomba naomba pia niseme mbele yako, mimi ni Katibu Mkuu wa Chama cha Kibunge cha Idadi ya Watu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa nyakati tofauti ndani ya mwaka huu, nilikuwepo katika miji ya Kigali, Rwanda; nilikuwepo Accra, Ghana na hivi majuzi nilikuwa Vancouver huko Canada. Dunia kwa ujumla wake inaongelea suala zima la akina mama na watoto wa kike, kwa maana ya idadi yao. Tunaambiwa kuna takribani bilioni 1.7 akina mama na wasichana ambao huwezi ukawaacha kwenye uchumi wa dunia. Tukicheza nje ya watu hawa kwa wingi wao, akina mama ambao pamoja na kuzungumzia suala la equality, lakini ndiyo watu ambao tunaambiwa tukija kwenye masuala yanayogusa uchumi, ni watu makini, ni watu ambao uchumi wao, katika eneo la kada ya familia, ukikuta kuna baba, kuna mama, mama anaimarisha uchumi wa familia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika,kwa hiyo, mipango yetu na bajeti, bila kuwagusa hawa tunakuwa hatujawatendea haki. Kwa hiyo, nilikuwa naomba, duniani huko, wanawaangalia kwenye sura hiyo na huwezi ukakimbia hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tunaambiwa na mtaalam mmoja wa IFAD, anakwambia kuijenga dunia bila njaa, huwezi ukaacha akina mama. (Makofi/Vigelegele)

Mheshimiwa Naibu Spika, na bado tunaambiwa wanakwenda kwa maana wanazalisha kati ya asilimia 20 mpaka 30, sasa nilitaka nianze kwa sura hiyo. Baada ya kulisema hilo, naomba pia Mheshimiwa Mpango, tunaambiwa hivi, tugusie standard gauge, tugusie mambo yote, bila kugusa afya ya msingi, kuna tatizo kubwa. Kwa hiyo, uwekezaji ambao hauendi kugusa afya, haya mengine yote hayana nafasi. Nalisema hilo kwa sababu walimu, wanafunzi, iwe ni askari, iwe watu wengine wote, nguvu kazi yenye afya ndiyo inaweza ikafanya mambo mengine yote. Kwa hiyo, naomba pia bajeti yetu ijikite pia katika universal health coverage, bila kusahau primary health care. Ni maeneo hayo ambayo tunaambiwa watu wetu wanakufa kwa sababu ya kukosa afya na pia tunakwenda kwenye umaskini mkubwa kwa sababu ya gharama kubwa za afya. Kwa hiyo, nilikuwa naomba hayo tuyaangalie kwa namna ya pekee. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nikitoka hapo naomba nigusie suala la reli, natoka Katavi, Mpanda, nilikuwa naomba na wazungumzaji wengine wameongea hapa, shirika hili bado linafanya mambo yake kizamani. Kwa mfano kule nyumbani, unaambiwa kwamba wateja ni wengi, mabehewa hayatoshi, hawaoni kwamba hilo ni soko, ni fursa ya kuchangamkia, kwamba kama wateja ni wengi, mabehewa machache, dawa ni kuongeza mabehewa, lakini utashangaa wamelalamika leo, wamelalamika kesho, watalalamika kesho kutwa, hatua hazichukuliwi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kama shirika linaona nivizuri kutofanya kwa, maana yake hata mashirika mengine, kwa mfano, mashirika ya ndege, hapa tumeona ikionekana wateja ni wengi Dodoma, wanaweza wakaongeza hata trip ya pili, zikaja hata ndege mbili kwa wakati mmoja. Sasa kwa nini hawa hawaangalii katika sura ya kibiashara? Nilikuwa naomba hilo waliangalie sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nikitoka hapo, eneo la kilimo, ni kweli na nakubali, tuseme yote tutakayoweza, bila kilimo, liko tatizo, lakini kilimo pekee cha kutufuta machozi ni kilimo cha umwagiliaji. Uzuri wa kilimo cha umwagiliaji, kwanza, wewe unakuwa na nafasi ya kuki-control,maji kidogo, maji zaidi na mwanga unakuwepo, lakini hiki kilimo cha kutegemea mvua za Mwenyezi Mungu, mara mafuriko na vitu vingine vya namna hiyo. Kwa hiyo, tukijikita kwenye kilimo cha umwagiliaji, tukichanganya na hicho kingine cha kutegemea msaada wa Mwenyezi Mungu, tuna uwezo wa kuifanya nchi yetu ikawa ghala la chakula na kukasaidia watu wengine katika maeneo mengine. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nikitoka hapo, suala la diplomasia ya uchumi, ndiyo maana tuna mabalozi nje ya nchi, tuna watu wengine wa namna hiyo. Inasikitisha kusikia ukiliona chungwa zuri, kama ni parachichi zuri, ni kwamba lilizalishwa Tanzania, limekwenda huko, halafu likapewa label ya nchi nyingine, mabalozi wetu wako wapi! Suala zima la diplomasia ya uchumi iko wapi katika kuinusuru nchi katika mambo hayo? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, na inasikitisha pia, ni kweli, hata mimi mara ya mwisho nilivyokuwa huko Canada nilisikia mtu mmoja akizungumza kabisa, kwa maana ya Mlima Kilimanjaro uko nchini kwao. Hasa mimi niendelee kusema, haya yote, kama mwenzako anafanya hivyo kwa ku-take advantage ya wewe, si na sisi tuna nafasi ya kulifanya hilo pia! Kwa hiyo, eneo hilo nilikuwanaomba sana, naomba sana tuliangalie katika sura hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, eneo la umeme ni kweli, nashukuru kasi inayoendelea, lakini kwa maeneo mengine kwa mfano hata kule kwangu Katavi, kasi si ile, najua hili Mheshimiwa Waziri husika atasikia pia kwa kupitia wewe. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nikitoka hapo, naomba niingie ene la madini, mara ya mwisho nilizungumza hapa, mimi ni mdau wa shughuli za uchimbaji madini, napata ugali wangu wa siku kwa kupitia uchimbaji wa madini. Nilikuwa naomba niishauri nchi yangu mambo yafuatayo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la kwanza, pamoja na kuambiwa mchango wa uuzaji dhahabu nje ya nchi umeongezeka kwa asilimia 0.7, tuache maeneo mengine ya utalii, fukwe na mambo mengine ya namna hiyo. Mimi naomba nijikite kwenye madini tu, tuna uwezo wa kuitoa nchi hii hapo ilipo ikaenda mbali zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tulipokutana na Mheshimiwa Rais, kwanza chukulia niseme, kwa maana ya idadi ya wachimbaji, nichukulie hata kwa idadi kidogo ya 6,000, nitaje tu au milioni sita tufanye. Hebu chukulia kila huyo mmoja, akazalisha kilo moja tu ya dhahabu, ni grams ngapi, kilo ngapi za dhahabu zitapatikana katika nchi hii, lakini mambo ambayo tunatakiwa tuyafanye, mimi niseme nashukuru kwa hatua ambazo Serikali imeanza nazo, lakini tunatakiwa twende mbali zaidi! Tusifunge milango, tutoe nafasi, kwa mfano, kuna nchi hazina madini, lakini wazalishaji wazuri wa madini na wanauza nje ya nchi. Tujiulize wanafanyaje watu hawa! Kwa nini tusiige? Sisi kama nchi, kwanza madini tunayo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, na niseme kwa mfano, leo pamoja na sheria hizi nyingine ambazo tunaziweka, bado wenzetu wa utafiti hawajafanya utafiti wa kutosha na ndiyo maana unaweza ukakuta ukilala, ukiamkia unasikia kuna gold rush somewhere, mtu alikuwa amekwenda tu kwa ajili ya kuchimba viazi, anaondoka na kipande cha dhahabu, mtu alikuwa ameenda kwa ajili ya kuchimba kisima, anaondoka na kipade cha dhahabu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa tutengeneze sheria rafiki ambapo, kwa mfano, mimi nimekwenda peke yangu porini, nikakutana na kipande cha dhahabu cha size ya kiatu, wewe haupo, polisi hayupo, mwingine hayupo, unategemea mimi nifanyeje!

MBUNGE FULANI: Naondoka nacho.

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI: ...ndiyo maana katika mazingira hayo, tukitengeneza mazingira rafiki, mtu huyu awe tayari ku...

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)

NAIBU SPIKA: Muda wako umeisha Mheshimiwa, kengele ya pili ilishagonga.

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja. (Makofi)