Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Dr. Charles John Tizeba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. DKT. CHARLES J. TIZEBA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kunipa nafasi ya kuchangia hoja iliyo mbele ya Bunge lako tukufu. Kwanza nianze kumpongeza Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na Naibu Katibu Mkuu na watumishi wote katika Wizara hii ya Fedha na Mipango kwa sababu kwa ukweli wanajitahidi. Wanajitahidi, hilo halina shaka kwa sababu makusanyo yameongezeka na miradi inatekelezwa. Niseme tu kwa ufupi kwamba huko Buchosa tunaona mambo yanaenda. Makao makuu yetu ya Halmashauri yanajengwa, Hospitali ya Jimbo au ya Halmashauri inajengwa na miradi mingine ya vituo vya afya na kadhalika inatekelezwa vizuri. Nawashukuru sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na shukurani hizi naomba niseme mambo ya jumla matatu au manne yafuatayo; moja, ni lile la uamuzi wa Serikali kuruhusu wananchi kuingia bandarini, kila anayeenda kutuma au kupokea mzigo. Hili jambo nimuombe sana Waziri wa Fedha alitazame upya. Huko nyuma bandari yetu iligubikwa na wizi, msongamano, urasimu, rushwa na kadhalika, kuna kitu kinaitwa port community wakakaa, wakafikia makubaliano kwamba watu wote wanaokuwa na mizigo ya kutuma au kupokea kuzagaa mle bandarini ni moja ya visababishi vya watu kuiba kuombaomba fedha zisizokuwa na utaratibu kwa sababu wengi wanakwenda kule hawaelewi hata abc za utoaji wa mizigo huko bandarini. Nafahamu jana aliongea kwa sauti sana Mheshimiwa Gulamali, lakini naomba tu niendelee kumshawishi Waziri kwamba hili jambo litazameni upya, sio kila mtu anaweza kufungua kompyuta akaona TANCIS inavyofanya kazi akaacha kupeleka usumbufu kwa maafisa wa bandari na TRA walioko kule. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo lililopo kuna ugumu sana wa watu kufungua kampuni hizi za clearing and forwarding, ni kama vile kuna kakundi kanajihakikishia monopoly ya hiyo kazi, lakini hizi kampuni zingekuwa nyingi za kutosha wala hizo gharama Mheshimiwa Mpango unazozisema zisingekuwa kubwa hivyo kwa sababu competition ingekuwa kubwa ya kupata wateja and therefore bei za huduma ile zingeshuka.

Kwa hiyo, zitazame tena, tusirudi tena kule bandari yetu hiaminiki, mzigo ukaanza kuhama. Leo tuko kwenye ushindani mkubwa, tuko kwenye ushindani mkubwa na Msumbiji, Kenya, Angola na Namibia. Kwa hiyo tukifanya tu jambo lolote la kuifanya tena bandari yetu ionekane sio competitive tunakuwa tunajiharibia wenyewe. Tuyatazame vizuri haya maamuzi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine niombe sana Serikali, nimesikiliza Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano wakiwasilisha bajeti sikuusikia uwanja wa ndege wa Mwanza ukizungumziwa. Haiwezekani jamani, ilikuwa ujengwe wakati wa Mwandosya akiwa Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi, sijui kilichotokea, mimi sitaki kwenda huko, lakini ukajengwa wa Songwe, Mwanza tupo tu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sio kwamba ninakunanihii wewe, hapana, lakini ilikuwa ujengwe Mwanza ukajengwa Songwe tukakaa kimya, kote ni Tanzania. Sasa tunaomba na wa Mwanza ukamilike kwa sababu sio hela nyingi kihivyo kwamba Taifa litafilisika Mwanza tukiwa na terminal nzuri pale kama mahali pengine zilivyo. Ni mji mkubwa pili hapa nchini, kwa nini usipate sifa na heshima unaostahili?

MHE. FRANK. G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Naibu Spika, Taaarifa.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Tizeba kuna Taarifa. Mheshimiwa Mwakajoka.

T A A R I F A

MHE. FRANK. G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimkumbushe tu kaka yangu Mheshimiwa Tizeba pale anazungumzia kwamba eti Songwe walikaa kimya, lakini ukumbuke kwamba juzi tu Chato kuna uwanja mkubwa kabisa unajengwa pale, kwa hiyo mambo yanaenda vizuri si ndiyo? (Kicheko)

MHE. DKT. CHARLES J. TIZEBA: Mheshimiwa Naibu Spika, unajua Mwakajoka nakuheshimu kwa hiyo sitakujibu. (Kicheko)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Tizeba unaipokea Taarifa hiyo?

MHE. DKT. CHARLES J. TIZEBA: Mheshimiwa Naibu Spika, Taarifa hiyo sijaipokea kwa sababu anajua sio Taarifa.

Mheshimiwa Naibu Spika, niishukuru Serikali kwa uamuzi wake kabisa na hapa shukurani za pekee ziende kwa Rais wetu Dkt. John Pombe Magufuli kwa uamuzi wa kujenga daraja la kati ya Busisi na Kigongo. Huo utakuwa ukombozi mkubwa sana kwa watu wa Kanda ya Magharibi. Leo watu wakitoka Dar es Salaam wale wanaokwenda Kagera wanalazimika kupitia Kahama na kwingineko, lakini lile daraja likikamilika ile njia itakuwa saa 24 watu wanasafiri, maisha yatakuwa murua. Tuombe Mungu tu kwamba daraja hili likamilike mambo ya Watanzania yaende kuwa, na nadhani litakuwa la kwanza la aina yake hapa Afrika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niishukuru pia Serikali kwa uamuzi wa kujenga meli ndani ya Ziwa Victoria. Kimekuwa kilio cha watu wa Ziwa Victoria.

Ombi langu Mheshimiwa Kwandikwa, ile meli ikikamilika ile sijui mbili zile, zile ndogo ndogo zianze kuhudumia watu wa visiwani. Kuna visiwa vingi katika Jimbo la Buchosa, kuna visiwa vingi Jimbo la Geita, kuna visiwa vingi Jimbo la Muleba, kuna visiwa vingi Jimbo la Bukoba Vijijini. Sasa hizi meli zilizopo leo, Butiama, Clarias na kadhalika tunaomba zianze kuhudumia hivyo visiwa, zisije tena na zenyewe zikabaki pale kwenda ile ile route ya Bukoba – Mwanza wakati kuna Watanzania chungu nzima kwenye visiwa kule wanasumbuka. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niende jambo Iingine la uvuvi. Asubuhi Mheshimiwa Serukamba amezungumza kidogo, naomba nisisitize hili jambo. Bado yako masharti magumu sana kuwafanya Watanzania wafuge samaki majini. Naomba ni-declare interest katika hili, ninafanya hiyo shughuli, kwa hiyo ninajua ugumu uliopo kwa mwananchi wa kawaida kufika mahali akapata leseni zote ili aweze kufanya ufugaji wa samaki majini. Masharti bado ni magumu sana. Vibali vya NEMC shilingi milioni 20, huyo Mtanzania wa kawaida ili apate kibali cha shilingi milioni 20 yuko wapi? Hujazungumzia kodi zilizoko katika vifaa vya kutengeneza cage zenyewe. (Makofi)

Kwa hiyo, niombe sana haya mambo yatazameni punguzeni hizi kodi, haya masharti, wezesheni wananchi wafanye shughuli za kujiletea kipato. Leo ziwani kule samaki wa kuzaana tu wenyewe hivi ni shida, Mheshimiwa Mabula amesema hapa viwanda vinafungwa kwa sababu uvuvi ule sio endelevu. Njia bora ya kuwa na uvuvi endelevu ni kufuga samaki. Vietnam na kadhalika wote wanafuga samaki na wana-export samaki kwa mabilioni ya dola na sisi tunaweza. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine la jumla ni hili la madeni ya watumishi wa Serikali. Jamani jiwekeni kwenye miguu ya hao walimu, wahudumu, wakunga, sijui watu gani ambaye anadai shilingi 200,000 miaka mitatu au minne. Lakini hilo moja la watumishi, wako watumishi wa umma wa ngazi za vijiji, madiwani na vitongoji, hawa nao wanateseka sana, halmashauri hazina pesa za kukata hizo asilimia 10 kuwapeleka kule. Kwa nini inakuwa vigumu kufikiria kuwapa na wao kamshahara, mimi nakaita kamshahara vyovyote vile lakini ya uhakika. Kuna halmashauri leo Madiwani hawajalipwa posho zao zile za mwezi miezi 10. Wanapata wapi nguvu za kufanya kazi vizuri hawa? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nizungumzie mambo ya Buchosa na hakika kama kumbukumbu yangu hainipotoshi ndiyo Halmashauri pekee isiyo na hata sentimeta moja ya lami. Kama yumo Mbunge mwingine humu Halmashauri yake haina hata sentimeta moja ya lami anyooshe mkono. Acha bwana wewe, Mpanda Mjini imejaa, acha! (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niombe tena hili jambo la barabara ya Sengerema – Kahunda, niliongea wakati wa bajeti ya Ujenzi na Uchukuzi yameandikwa maneno sio sahihi, kitabu kile haijulikani kimerekebishwa, Mheshimiwa Kwandikwa namuona Engineer Kamwelwe hayupo. Fanyeni kila mnaloweza hili jambo likae sawasawa. Nikipinga bajeti sitakuwa nimekosea. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, la mwisho, kivuko…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)