Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Raphael Michael Japhary

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Moshi Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. RAPHAEL J. MICHAEL: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kupata nafasi ya kuchangia bajeti hii ya Serikali ya mwaka 2019/2020. Mchango wangu kwa Serikali ni kwamba tuna kipindi cha miaka minne tangu tumepewa dhamana kwa upande wa Chama cha Mapinduzi kuongoza nchi hii, nilitaka kupata tafakari ya Serikali kwamba je, kwa miaka minne hiki walicho-achieve ndiyo yalikuwa matarajio ya Watanzania? Na ninajaribu kutafakarisha Serikali kwa sababu naamini mwaka 2015 wakati wa kampeni za kuogombea kila upande ulikuwa na movement zake for change. CHADEMA walikuwa na movement for change na upande wa CCM walikuwa na Magufuli for change. Maana yake nikwamba wananchi walikuwa na matumaini makubwa sana ya mabadiliko makubwa ya maisha yao katika nchi hii.

Mheshimiwa Spika, sasa nilifikiri kwamba labda Serikali itafakari baada ya miaka minne yale matatizo ya wananchi yametatuliwa na yametatuliwa kwa kiwango gani? Nadhani tungetafakari hili kwa undani tungejipima vizuri zaidi. Hapa tunabishana kati ya maendeleo ya watu na maendeleo ya vitu ambayo kwa ujumla yote ni muhimu katika nchi yetu. Lakini wananchi walipokuwa wanakimbizana na sisi barabara zilikuwa hazijengwi? Wananchi walipokuwa wanakimbizana na sisi reli zilikuwa hazijengwi? Ndege zilikuwa hazipo? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa haya maswali tukitafakari tutajua hitaji kubwa la wananchi katika nchi hii ilikuwa kuondokana na umaskini walionao. Je, katika miaka yetu minne tumeweza kuondoa umaskini Watanzania walio nao? Hayo ndio nafikiri maswali ya msingi ya kuuliza. Hivi sisi tunataka tushukudie nini?

Mheshimiwa Spika, nadhani sisi Watanzania hasa Chama cha Mapinduzi tunakuwa wagumu kuamini kuliko hata tomaso alivyokuwa ameamini ufufuko wa Yesu. Kwa nini kwa sababu Watanzania wote tuliopo hapa tunafahamu kabisa ndugu zetu ni maskini, wana maisha ya dhiki, wana matatizo, wote Wabunge hapa tuliopo hapa ndani tunajua kwamba tuna matatizo makubwa ya dependence ya watu wetu, kwa sababu hawana uwezo na tuna uhakika kwamba dependence imeongezeka halafu tunaambia uchumi unakuwa kwa 7% kwa hiyo articulate hali yetu ya maisha ya Watanzania na tunapongezana kabisa yaani mnapongezana as if your doing so well, hamtaki kukubali kwamba Taifa limerudi nyuma mno maisha ya watanzania yamezidi kudidimia.

Mheshimiwa Spika, lazima tujipime kwamba hivi mwaka 2015 maisha ya Watanzania yalivyokuwa ya huko kijiji na miaka minne sasa maisha yalivyo. Hivi mazuri yakikuwa wakati gani yalikuwa mazuri kipindi hicho au kipindi hiki? Ndicho kipimo cha maendeleo ya wananchi. Sasa nilikuwa naomba Mheshimiwa Waziri anisaidia ni mtu mwenye weledi mkubwa sana na ni mbobezi wa masuala ya uchumi anisaidie na Naibu wake Waziri nawaamini kabisa kwa uwezo wao, sina mashaka nao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, labda waniambie ni kwa nini wamechagua mtazamo wa uchumi uliofungika kwa maana ya contractionary economic policy and in ward looking policy kuliko kuangalia expansionary policy uchumi unaoangalia nje zaidi. Tafakuri yangu inaniambia tunapotazama uchumi wa ndani tukaangalia kodi zetu za ndani na mapato mengine yasiyo ya kodi ya ndani kama chanzo cha ku-finance miradi ya maendeleo tunazidi kuumiza watu wetu. Tunaweza tukawa na mawazo bora sana ya kusaidia miradi mikubwa ya nchi hii, ya kusaidia maendeleo ya nchi hii lakini tukaosa approach bora ya kui- finance miradi hiyo hayo ndio mawazo nafikiri hayo ndio mawazo ya Kambi ya Upinzani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Kambi ya Upinzani haijawahi kufikiri kwamba kuna ubaya wa kujenga reli, Kambi ya Upinzani haijawahi kufikiri kama kuna ubaya wa kuwekeza kwenye ndege, Kambi ya Upinzani haijawahi kufikiri kwamba kuna ubaya wa kuwekeza kwenye miundombinu yoyote ile. Lakini tunadhani tunachofautiana Mheshimiwa Waziri katika approch ni namna gani tu-finance hii mipango ili wananchi wetu wa chini wasiteseke. Sasa problem tuliyonayo ni kwamba tunabishana hapa tu kwamba labda kuna watu wanaopinga haya mambo, which is not true. Wote tunakubali kwamba lazima wananchi waendelee, lakini approach zetu zikoje katika suala la mitazamo ya kiuchumi, sasa nyie ni wabobezi wakubwa mliopewa dhamana hii kubwa, ni vizuri Mheshimiwa Waziri na mimi ungeniambia ni kwa nini ume- opt kwenye mawazo ya uchumi uliofungika ya kubana uchumi zaidi kuliko kufungua uchumi, nadhani unge-opt kwenye approach ya kufungua uchumi leo hotuba yako Mheshimiwa Waziri ingekuwa inaonesha namna gani uta- attract FDI - Foreign Direct Investment katika nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, hotuba hii ingeonyesha hivi kama solution, labda hotuba leo ingeonesha namna gani uta- incorporate PPP - Public Private Partnership ambayo ingeweza kusaidia, lakini kwenye mpango wenu mnaonekana sana kwamba mna-discourage PPP, mna- discourage uwekezaji kutoka nje. Mnaamini kwamba through hizi Kodi ambazo mnaumiza wafanyabiashara, mnaumiza wafanyakazi zinaweza zikawasaidia kwenda mbele. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwangu mimi naamini kwa Kambi ya Upinzani hatuamini kwamba mko kwenye mtazamo sahihi, ndiyo ninachofikiri hicho na kimsingi hapa ndipo tunapopata tatizo hapa, kigugumizi kwa sababu watu hasa tunabishana, hivi wananchi wanapata maendeleo ama ni wanataka vitu?

Wananchi wanataka vitu maendeleo ya vitu, lakini wanachotaka maendeleo yao pia. Hawataki vitu tu, wanataka wapate uhakika wa huduma za afya, wanataka wapate uhakika wa huduma za maji, wanataka uhakika wa kipato cha kulisha familia zao, wanataka wapate uhakika kusomesha watoto wao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hamuwezi kusema mme-achieve economically while people are suffering, na mnakusanya Kodi mnazitumia kwa expense ya maisha ya Watanzania kwa sacrifice ya maisha ya Watanzania, haiwezekani, kwa hiyo ni lazima Mheshimiwa Waziri kwa uwezo wako na kwa ubobezi wenu mtazame hili kwa upana wake, na hili nafikiri siyo jambo la kubishana sana ni jambo la kutazama namna gani tunahakikisha miradi ya maendeleo inafanyika lakini namna gani tunahakikisha kwamba watu wetu wanapata huduma wanazostahili na vipato vyao vinakuwa, ili na wananchi nao wa-feel huu uchumi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, unapowekeza kwenye standard gauge unafanya jambo jema, lakini mradi utakapo toa matokea baadaye sana je kwa sasa hivi Mwananchi huyu wa Tanzania aendelee, amefunga mikanda for fifty years, hajapata mabadiliko, amepata matumaini kwamba baada ya kuingia Serikali hii atapata mabadiliko, ataongeza kipato chake, as we are talking leo mfanyakazi hajaongezewa mshahara. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ninapozungumzia leo...

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Ahsante sana.

MHE. RAPHAEL J. MICHAEL: Mheshimiwa Spika, watu wanapunguzwa kazi, tunapozungumzia leo biashara zinafungwa, ninapozungumzia leo matatizo ni mengi makubwa katika nchi hii, lakini sisi tukikaa hapa kwenye Bunge hili tunapongezana kwamba tunafanya vizuri katika uchumi huu, tunahitaji philosophy za kitaalam sana tuchanganyane huku ndani, lakini wananchi...(Makofi)

SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Japhary.

MHE. RAPHAEL J. MICHAEL: Mheshimiwa Spika, philosophy, kwa hiyo ninadhani ni wakati wa kutafakari...

(Hapa baadhi ya Wabunge walizungumza bila kufuata utaratibu)

SPIKA: Eti! Ni ya pili tayari.

MHE. RAPHAEL J. MICHAEL: Mheshimiwa Spika, ya kwanza.

(Hapa baadhi ya Wabunge walizungumza bila kufuata utaratibu)

SPIKA: No, alianza na dakika 35.

MHE. RAPHAEL J. MICHAEL: Mheshimiwa Spika, ya kwanza.

(Hapa baadhi ya Wabunge walizungumza bila kufuata utaratibu)

SPIKA: Tayari ni dakika kumi. (Makofi)

MHE. RAPHAEL J. MICHAEL: Mheshimiwa Spika, Ya kwanza.

SPIKA: Wala hujaonewa kabisa.

(Hapa baadhi ya Wabunge walizungumza bila kufuata utaratibu)

MHE. RAPHAEL J. MICHAEL: Mheshimiwa Spika, nimeonewa kwa kweli.

(Hapa baadhi ya Wabunge walizungumza bila kufuata utaratibu)

SPIKA: Tayari, tayari dakika kumi.

MHE. RAPHAEL J. MICHAEL: Mheshimiwa Spika, ahsante.