Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa fursa ya kuchangia. Jambo la kwanza nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutuamsha salama na kutufikisha kutimiza wajibu wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, awali ya yote kwanza nimpongeze Mheshimiwa Waziri wa Fedha kwa kuonesha katika bajeti ya mwaka huu dhamira ya kuanza safari ya kufanya reforms katika mambo ambayo yamekuwa yakilalamikiwa na Wabunge na Watanzania kwa muda mrefu. Kwa hiyo, mimi nampongeza sana, hasa suala la kutengeneza demarcation ya line kati ya TBS na TFDA katika hatua ya awali. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo la pili, nimpongeze Mheshimiwa Dkt. Mpango na Mheshimiwa Profesa Kabudi kwa namna walivyo-handle suala la Airtel na kupelekea Serikali kupata 49% share. Wameli-handle jambo hili in a civilized and professional way. Nataka nimuombe Mheshimiwa Waziri, na niiombe Serikali kwa ujumla wake; tunapo-handle masuala ya private sector this is the best way ya ku-handle wawekezaji wa ndani ama wa nje. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini nisisitize tumepata share asilimia 49 katika Airtel. Ombi langu, kwa kuwa tunakuwa sehemu ya bodi, tunakuwa sehemu ya management, ikija obligation ya investment kwa sababu kwa takwimu, Airtel is not making profit, likija suala la investment na Telecom Sector inabadilika kila siku hakikisheni mnawekeza kama wadau wengine waliokuwa partners katika business, this is very important. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la tatu kuhusu Airtel; Serikali ina TTCL, nimemsikia Mtendaji Mkuu wa TTCL akisema siku moja kwamba utakapokwenda maeneo ambayo hakuna mtandao wa TTCL unaweza ukafanya roaming kwa kutumia Tigo, it is wrong in business. Sisi tutakuwa tunalipa sana kumlipa Tigo kwa sababu tunatumia infrastructure yake. Ninawashauri, ingieni makubaliano na Airtel ambayo mna 49% kama Serikali ili tutakapokuwa maeneo ambapo TTCL haipo itumie infrastructure ya Airtel kufanya mawasiliano kwa sababu itakuwa ni within the circle ambako ninyi mna-stake.

Mheshimiwa Spika, nitoe maoni yangu katika hoja iliyopo mbele yetu. Nimesoma hotuba ya Waziri, nimesoma hotuba za Wizara tatu ambazo tunazitarajia kuwa ndiyo input kuweza ku-attain malengo yaliyoko katika hotuba ya Waziri; nimesoma hotuba ya Wizara ya Wizara ya Kilimo, nimesoma hotuba ya Wizara ya Mifugo, nimesoma hotuba ya Wizara ya Viwanda na Biashara.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Nape ameongelea Sekta ya Kilimo, nataka tu on record ukichukua total development budget tuliyotenga mwaka huu ya shilingi trilioni 12, uka-compare na kile ambacho tumekitenga katika sekta ya kilimo na mifugo ambazo kwa ujumla wake zinachangia zaidi ya asilimia 30 ya GDP yetu. Fedha tulizotenga kwa ujumla ni shilingi bilioni 161 wakati development budget ni shilingi trilioni karibu 13. Hii ni sawasawa na asilimia 1.3; hatuwezi kupiga hatua. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa hoja yangu ni nini; nimesoma monetary statement, hii hapa ya BOT na ninaomba ninukuu maneno; BOT wanasema; global economy itashuka kutoka 3.6 kwenda 3.3 kwa sababu ya trade war iliyopo kati ya China na Marekani. Sasa sisi kwenye global economy who are our trading partners and what are we selling? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sisi tunauza mazao ya kilimo na ninaomba niyasome hapa; zao la tumbaku, limeshuka kutoka 1.2 million kgs tuna-project mwaka huu 2018/2019 tutakuwa na tani 50,000 ndiyo tutakayoenda kuuza kwenye soko la dunia. Korosho mwaka 2016/2017 ilikuwa tani 265,000; mwaka 2018/2019 tani 224,000; mkonge kutoka tani 36,000 sasa tuna- project tani 15,000; chai kutoka tani 26,000 tunakwenda tani 19,000; sukari kutoka tani 330,000 tunakwenda tani 327,000; pareto kutoka tani 2,150 tunakwenda tani 1,800. Zao pekee ambalo tuna-project ku-grow ni zao la kahawa kutoka tani 48,000 kwenda tani 61,000; pamba na yenyewe tunajua kinachoendelea.

Mheshimiwa Spika, sasa nini ninachotaka kusema Mheshimiwa Waziri wa Fedha umempa Commissioner General wa TRA target ya kukusanya 1.7 trillion shillings. Mheshimiwa Waziri Commissioner General hawezi kukusanya na huyo utamtumbua. Nasema haya in very good faith kwa sababu ili tukusanye kodi ni lazima tuzalishe, ili tukusanye kodi ni lazima tufanye biashara. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Spika, sasa ushauri wangu ni nini; ukienda kwenye lending, kutoka mwaka 2016 mpaka mwaka wa fedha 2018/2019 sekta ya kilimo uwekezaji wa mikopo umeshuka kutoka asilimia 11 mpaka -4; sekta ya manufacturing kutoka asilimia 20 mpaka 17; sekta ya transport kutoka asilimia 27 mpaka asilimia 4; building kutoka asilimia 9 mpaka -2; trade kutoka 2.2 mpaka -2.1; hotel and transportation kutoka asilimia 7 lending kushuka mpaka -1.6%.

Mheshimiwa Spika, nini kitakachotokea; excise duty zitashuka, VAT zitashuka, consumption taxes zote zitashuka na Mheshimiwa Rais wakati anaongea na wewe Mheshimiwa Waziri na wataalam wakati anaongea na wafanyabiashara, alisema kodi za ndani zinashuka na kodi za ndani ni zipi; kodi za ndani ni VAT on consumption za ndani; kodi za ndani ni PAYE, kodi za ndani ni excise duty, hizi zote ziko related na biashara. Kama hatutafanya proper harmonization na regulation kwenye biashara hatuwezi kutoka. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri Dkt. Mpango, sasa hatua ya kwanza ninayokuomba na ninajua hii utakumbana na matatizo Serikalini, fanya maamuzi yafuatayo; muite Waziri wa Viwanda na Biashara, kaa naye, muombe mfanye mabadiliko makubwa. Tuna sheria hapa; tuna Sheria ya CARMATEC, tuna Sheria ya TIRDO, tuna Sheria ya EPZA, tuna Sheria ya TanTrade, tuna Sheria ya TEMDO; hizi taasisi zina-contradict zenyewe. Fanyeni harmonization. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la pili; mtu yeyote anapotaka kusajili biashara hatua ya kwanza anayofanya ni kwenda sehemu inatwa BRELA, BRELA ni kifupi cha Business Registration and Licensing Agency. Ushauri wangu, chukueni Sheria ya BRELA, hizi taasisi zote ziwekeni mle ndani, anzisheni kitu kinachoitwa Business Registration Licensing and Regulatory Authority. Ili mtu anapoingia kusajili biashara, kuchukua leseni, anakutana na kila kitu mle ndani, akitoka anakwenda kufanya biashara yake. Uta-reduce bureaucracy, uta-reduce cost of business. (Makofi)

MBUNGE FULANI: Bashe una akili wewe.

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Spika, la pili angalia kitu hiki Mheshimiwa Mpango GDP contribution, sekta iliongoza kukua ambayo ni ya sanaa inachangia 0.3% hii ndiyo imekua, imeongoza kukua katika uchumi wetu, sekta inayokua ambayo inachangia asilimia kubwa ya GDP, sekta ya kilimo imekuwa kutoka 3.7% kwenda 5% marginal growth is less than population growth, hamuwezi ku-break through.

Ushauri wangu tuhakikishe tuwe na mpango na mimi hili linanisikitisha, ukisoma mpango wa maendeleo huwa hapa tulioupitisha hauna smart objective, tunapozungumzia smart objective ni lazima ziwe measurable, unazalisha pamba kutoka tani 200,000 kwenda ngapi? Unazalisha tumbaku kutoka tani moja kwenda ngapi?Unazalisha kahawa kutoka wapi kwenda ngapi?Usipofanya namna hii hamuwezi kujipima, hatuwezi kujipima...

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Malizia Mheshimiwa.

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Spika, namalizia kwa neno moja,naomba niseme hivi yupo hapa tulikuwa handsome boy Waziri Mwijage aliasisi cotton to clothes, ule mpango umeishia barabarani, aliasisi mpango wa leather to leather product umeishia barabarani, aliasisi mpango wa mbegu za kunde, mazao ya mbegu za kunde mpango umeishia barabarani. Mheshimiwa Waziri tunawaomba tulifanya mabadiliko mwaka 1967 kwenda kwenye uchumi wa kuhodhi wa Serikali, tukafungua masoko 1990s kwenda 2000 umefika wakati wa kupitia mfumo mzima wa Serikali, badilisha Sheria ya Income Tax, badilisha Sheria ya VAT, badilisha Tax Administration Act, usipofanya namna hii hauwezi kufikia malengo tuliyojiwekea ni lazima tuwe production oriented kuliko tax oriented kwenye uchumi wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ombi moja kwa heshima yako na kwa kiti chako, Waziri umetangaza hapa wafanyabiashara wasikamatwe, Nzega kwangu imetua tax force wiki iliyopita na kamji kale kadogo, wamekamata wafanyabiashara saa hizi wako polisi zaidi ya wiki, pale Wizarani kwako Mheshimiwa Waziri na Mwenyekiti niseme Waziri amekuwa mwalimu na dada yangu Ashatu mwalimu, wanajua kwenye maendeleo kuna-primitive way of wealth accumulation, nchi hii huko nyuma watu walipiga dili niwaombe hebu kale kaofisi namba 43 pale Hazina, Dar es Salaam ambako kamekuwa- connected na TAKUKURU ambako wafanyabiashara wanapiga foleni mpaka leo kuhojiwa mambo ya mwaka 2008, 2009, 2010.

Nikuombe Rais Magufuli ni man of decision mpelekee, toeni amnesty, watu waliowahi kupiga deal jamani Mheshimiwa Mpango hawezi kufukuzwa hata siku moja kwa wizi hata siku moja I can bet. Lakini huko nyuma watu walipiga deal, na deal zote zilianzia Serikalini, leo wanao- suffer ni wafanyabiashara, wanauza mali zao kulipa madeni ya miaka ya nyuma, tutawaumiza, wasameheni tangazeni amnesty, atakayeiba kuanzia leo mumshughulikie. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naunga mkono, ninachokiomba Serikali fanyeni harmonization mipango na bajeti havionani, ahsante. (Makofi)