Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. ALMAS A. MAIGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kuniruhusu na mimi pia nichangie Bajeti Kuu ya Serikali yaani mapato na matumizi kwa mwaka 2019/ 2020.

Mheshimiwa Spika, kwanza napenda kutoa pongezi sana kwa Wizara hii, hasa kwa Mheshimiwa Dkt. Mpango, dada yangu, Mheshimiwa Dkt. Kijaji na Katibu Mkuu - Ndugu Doto James, na wengine wote wataalam wa Wizara hii ambao wamekaa na kuandaa bajeti hii ambayo kwa kweli imekidhi viwango, lakini pia imekidhi matakwa ya wananchi wa Tanzania na vilevile itatuvusha hapa tulipo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimeshuhudia upande wa pili kule wanaongea mambo mengi sana. Jana mtu mmoja alijikita katika kusema kwamba Mheshimiwa Dkt. Mpango na mama yangu, Mheshimiwa Dkt. Ashatu hawafai na waondolewe katika nafasi hizo. Lakini hiyo ni dalili ya rangi mbili waliyonayo hawa wenzetu, wamesema sana, lakini mimi nashuhudia kwamba Mheshimiwa Dkt. Mpango na wenzake, timu hii ndiyo bora kabisa katika utawala wa Tanzania, na ninawapongeza sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini vilevile wenzetu hawa kwanza wanasema bajeti hii imepangwa vibaya na Mheshimiwa Dkt. Mpango hafai, lakini ukikutana nao kule nje wanaungana na wananchi ambao wanasema bajeti hii ni nzuri sana. Kwa hiyo, wao wanashindwa kujifaragua peke yao wanajiunga na wananchi ambao wanasema bajeti hii ni nzuri na hiyo nampongeza sana Mheshimiwa Dkt. Mpango na hasa Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Magufuli ambaye alimteua Mheshimiwa Dkt. Mpango na Naibu wake kufanya kazi hii ngumu sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tuna sungura mdogo hatuwezi kumgawa watu wote sawasawa akatuenea na kushiba, lakini tukubali kwamba kazi hii siyo rahisi, mtu yeyote akivaa viatu vya Mheshimiwa Dkt. Mpango na mwenzake Mheshimiwa Dkt. Ashatu, atapata tatizo hili ambalo tunalipata kwamba hela hii haitoshi na kinachopatikana tunakigawa sawasawa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niende sasa kwenye kuchangia bajeti hii na nianze na umuhimu wa sekta binafsi hapa nchini. Sekta binafsi nchini hapa ndiyo inayojenga vitega uchumi vikubwa, kwa mfano barabara na hivi karibuni viwanja vya ndege, na mfano Terminal III ambayo inakusudiwa kuingiza hela nyingi sana kutokana na ndege zitakazotua pale, watalii na abiria ambao watalipia gharama za kiwanja hicho. Na mimi ni--declare interest kwamba katika local content ya kiwanja hicho, Kampuni ya Ulinzi na Usalama iliyofunga mitambo pale ni SSTL Group ambayo ni kampuni yangu.

Mheshimiwa Spika, sekta binafsi pia inajenga vitega uchumi vingine kwa mfano reli inayojengwa na Yapi Merkezi ni kampuni binafsi, lakini vilevile umeme wa Rufiji unajengwa na sekta binafsi; lakini pia umeme wa REA nchini hapa unajengwa na sekta binafsi. Kwa hiyo sekta binafsi hii ina miradi mingine kadhaa. Namuomba Mheshimiwa Dkt. Mpango aipe umuhimu wake kama uti wa mgongo kama ambavyo katika nchi nyingine imepewa. Sisi hapa uti wa mgongo huu wa sekta binafsi umepinda na hauna nguvu yoyote na sasa unalegealegea sana. Mheshimiwa Dkt. Mpango, uimarishe sekta binafsi ya ulinzi ili iweze kuchangia barabara katika kukuza uchumi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo lingine ambalo ni muhimu sana tumelisema sana na ni-declare pia mimi ni mwajiri vilevile ni suala la SDL. Mheshimiwa Dkt. Mpango hili tumelisema sana. Sisi tunashindwa kufanya biashara hapa kwa sababu ya kitu kinachoitwa ease of doing business; asilimia 4.5 ni kubwa kuliko SDLs zote duniani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hapa Afrika Mashariki ni Kenya tu wana-charge sekta ya utalii asilimia 1.2, kwingine kote Uganda hakuna, Rwanda hakuna, Burundi hakuna, kote na dunia nzima Tanzania ina-charge asilimia 4.5, ni kubwa sana. Tunaomba utakapokuja kufanya majumuisho yako, hebu fikiria upunguze hata kidogo. Tumetoka mbali, tulikuwa na asilimia sita, lakini tunakuomba uipunguze taratibu, hatusemi mara moja, lakini fikiria hata kupunguza kiasi kidogo, sisi waajiri na wafanyabiashara tutafurahi sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, suala hili limeletwa pia Serikalini, katika mambo ambayo Mheshimiwa Rais alitaka yaletwe Tanzania Private Sector Foundation (TPSF) na waajiri tumekuletea hili suala la SDL, lipunguzwe hata kidogo. Tafadhali utakapokuja kufanya majumuisho yako tupunguzie SDL kutoka asilimia nne kwa kiasi chochote kile ambacho utaona kwamba hakitaumiza bajeti.

Mheshimiwa Spika, lipo suala la VETA; VETA ilipobuniwa ilikuwa katika Wizara ya Kazi na madhumuni yake ni kufundisha wafanyakazi skills. Lakini sasa VETA imehamishiwa kwenye Wizara ya Elimu ambayo inafundisha elimu. Sisi waajiri ambao tunachangia mfuko huo kwa zaidi ya shilingi bilioni tisa kwa mwezi tunaona kama zile hela zinapotea. Lakini pia imekuwa inachukua watoto badala ya wafanyakazi ambao walikusudiwa kwenda kuongeza ubunifu na ujuzi.

Mheshimiwa Spika, lipo suala la REA; REA hii haiendi vizuri kwenye jimbo langu. Mimi nina vijiji 87, katika REA III(i) nilipewa vijiji 18 mpaka leo hii vijiji vitatu tu, Mheshimiwa Dkt. Kalemani vijiji vitatu tu ndiyo vimewashwa katika 18, asilimia 16, basi na muda unakwenda. Lakini mbaya zaidi hata nyumbani kwa Mbunge umeme hakuna, nimesema, nisemeje sasa ili mnielewe?

Mheshimiwa Spika, lipo suala la mwihso ambalo pia namuomba sana Mheshimiwa Dkt. Mpango alifikirie kupunguza matumizi. Balozi zetu kule nje tunapanga nyumba na nyumba hizi ni ghali sana. Asilimia zaidi ya 60 ya matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje inakwenda kupanga majengo na tunadaiwa hatupeleki hela kule, tujenge majengo yetu kwa njia ya mortgage. Tukianza kujenga majengo kwa muda wa miaka kumi kwa mkopo na tuna-mortgage majumba yaleyale, baada ya miaka kumi tutakuwa na nyumba zetu.

Mheshimiwa Spika, mfano mzuri hapa Tanzania, Mabalozi wangapi wamepanga? Wamejenga nyumba zao na sisi tuone mbali, Mheshimiwa Dkt. Mpango, punguza matumizi ya Wizara ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa kujenga nyumba zetu. Mimi nilikwenda kuangalia kiwanja ambacho tulipewa Muscat, kwa gharama yangu, nimefika kule Muscat jiwe la msingi limewekwa na Mheshimiwa Dkt. Kikwete. Leo huu mwaka wa ngapi tangu Mheshimiwa Dkt. Kikwete aondoke. Mpaka tunaona aibu tumekwenda kuondoa kile kibao limekuwa pori.

Mheshimiwa Spika, lakini pia tulipopewa kiwanja cha Kenya tulibadilisha kiwanja cha Kenya Ubalozi hapa, wenzetu wamejenga Ubalozi wa Kenya wanafanya matengenezo ya kawaida. Sisi kile kiwanja cha kwetu Kenya mara kitakiwe kuuzwa, Mzanzibari mmoja akaenda kukichukua akapeleka mahakamani; kwa nini tusijenge nyumba zetu kwa mkopo kutumia mortgage system? Jambo hili litatusaidia sana kuondoa madeni yaliyopo.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kuniruhusu nichangie bajeti hii. Naunga mkono hoja mia kwa mia. Ahsante sana. (Makofi)