Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Jitu Vrajlal Soni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. JITU V. SONI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana awali ya yote naomba nichukue fursa hii kuanza kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa siku ya leo kuniwezesha kuchangia. Lakini pia nichukue fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na timu yao nzima kwa kazi kubwa na nzuri sana wanayofanya na niwapongeze kwamba bajeti ya awamu hii imeleta matumaini makubwa ni bajeti moja katika bajeti ya hii miaka minne ambayo ni ya mfano kabisa, imelenga kila sekta, lakini imelenga hasa kwa kuwezesha viwanda vya ndani na ukuaji wa uchumi wa ndani kukua kwa kasi kubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini pia nishukuru kwa kuanza kutekeleza suala lile la blueprint kwa kuondoa tozo angalau 54, ni mwanzo tu lakini ninaamini kwamba sasa mtakuja na ile sheria Bungeni ya kuweza kuifanya blueprint yote iweze kutekelezwa ili viwanda/biashara ya ndani iweze kukua na tuweze kuzalisha bidhaa na tuweze kushindana kwa bidhaa zinazotoka nje lakini pia bidhaa zetu ziweze kwenda nje kushindana katika masoko mbalimbali. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia nishukuru kwamba mmeweza kuendeleza msamaha wa kodi kwa muda wa miezi sita mingine kwa wale ambao ilikuwa bado hawajalipa. Niwapongeze mmeweza pia kupandisha ile threshold ya VAT kutoka milioni 40 kwenda mpaka milioni 100 lakini pia wale ambao walikuwa chini ya/waliotakiwa kupeleka mahesabu baada ya milioni 20, sasa ni milioni 100.

Mheshimiwa Spika, ningeomba kwenye orodha hiyo kama inawezekana makampuni ambayo ni limited, ambayo hayapo kwenye mfumo huu, ambayo yapo chini ya milioni 100 ni watu wamependa formalize biashara zao lakini bado biashara zao zipo chini ya milioni 100 na wao pia waendelee kupata msamaha huo ili pawe na usawa. Mtu anaye- formalize asiadhibiwe na lengo kubwa ni kutoa sekta isiyo rasmi kuwa rasmi. Kwa hiyo, pangekuwa na vivutio zaidi kwa sekta ambayo watu wamejirasimisha basi wao wapate vivutio zaidi ili wengi waondoke huko kwenye sekta isiyo rasmi na kurudi kwenye sekta ambayo ni rasmi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia niwapongeze kwa kushusha kodi ambayo haijasemwa na watu wengi, mmeshusha vile viwango vya kodi kwenye presumptive tax kutoka 150,000 kwenda laki tatu na kitu, kwa hiyo kodi zimeshuka. Kwa hiyo, wafanyabiashara wengi sasa wataweza kulipa zile kodi na hawatafungiwa biashara zao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ombi langu lingine kwamba tunaomba mkija sasa wakati wa Finance Bill tuweke utaratibu wa kuwa na one stop center badala mtu kutafuta leseni na vibali maeneo mbalimbali kama ilivyo kwenye TIC kwa wale wanaojisajili TIC wale wa nje, sasa na sisi wa ndani kupitia Afisa Biashara wa Mkoa na Wilaya, tukienda tukilipa sehemu moja, tozo na ada zote ulipie sehemu moja unaachana nao mpaka mwakani, sasa huko Serikali ijue kwa sababu yote inaingia kwenye Mfuko Mkuu wa Serikali, wajue namna ya kugawanya hizo tozo na ada. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, bado nasisitiza blueprint usipoitekeleza bado hatutakuwa tunaweza kushindana kwa bidhaa zetu kwenda nje wala humu ndani, lakini ni hatua moja nzuri mmeanza nayo, niwapongeze lakini naomba hiyo sheria ije mapema. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lingine ambalo ni muhimu, mnakusanya fedha vizuri lakini bado matumizi mabaya yapo kwa mfano GPSA, TEMESA lakini pia TBA, hayo ni maeneo ambayo haya mabilioni mnayokusanya wanaenda kuyatumia vibaya, ni kichaka ambacho kimejificha ambapo kwa mfano TEMESA ukipeleka magari ya Halmashauri kutengeneza pale ni kero kubwa, unaweza kutengeneza kwa nusu ya bei na kwa viwango vilevile tukiwa tunatengeneza nje hivyohivyo katika majengo ya Serikali na nini.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo muichunguze TEMESA na GPSA hiyo Sheria ya Manunuzi wanapanga watu wakuwa- supply 10 kwa mfano kwa mwaka mzima. Iwe ni wazi GPSA ibaki ku-regulate kwamba kama BOT wanaangalia bei za foreign exchange na nini ni ngapi, GPSA ibaki ku-regulate bei, lakini iwe wazi kwa mtu yeyote, saa yoyote tenda ikitolewa waweze kujaza ndiyo mtaona manufaa, value for money itapatikana. Kwa hiyo, GPSA, TEMESA, TBA muwaondoe. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini ombi langu lingine, undeni Tanzania Regulatory Authority, upper stream, lower stream ili wote wawe chini ya taasisi moja na wao wote waweze kufanya ndiyo mtaweza kuondoa kodi, tozo, ada na ushuru mbalimbali nyingi, lakini pia wafanyabiashara wengi wanaomba kwamba hizi regulatory bodies badala ya kwenda kupiga faini za ajabu ya kwanza watoe onyo na kuwaambia rekebisha, ya pili iwe ni onyo kali zaidi na ya tatu ndiyo iwe faini, siyo mara ya kwanza anakuja anakufungia biashara anakutoza faini za ajabu, hapo ndiyo tutaona lengo lao kuu ni kufanikisha watu wafuate sheria na utaratibu.

Mheshimiwa Spika, lakini ombi langu lingine ni kama Kamati ya Bajeti ilivyopendekeza na siku zote tunapendekeza suala la kuondoa kodi kwenye mitambo ya maji na mitambo ya kuvuna maji ya mabwawa na malambo. Hii itasaidia watu wengi zaidi kuwekeza kwenye sekta binafsi badala ya kutegemea Serikali ifanye mambo yote haya kwenye umwagiliaji, maji ya kunywa, maji ya mifugo na mabwawa ya samaki na bado tukitengeneza hayo mabwawa, athari tunayopata ni uharibifu wa yale maji ya mafuriko kuharibu miundombinu itakuwa haipo, kwa hiyo mkiondoa.

Mheshimiwa Spika, leo hii kwa wale ambao wanapata msamaha ni makampuni makubwa na miradi ya Serikali, lakini mtu binafsi hapati hiyo. Hasa upande wa kilimo hatuwezi kupata kwa sababu bidhaa zetu hazipo vitable, kwa hiyo vital on deferment kwenye capital goods sisi hatupati. Kwa hiyo, nivizuri mkatuondolea ili watu wengi binafsi pia waweze kuleta mitambo ya maji na tuweze kusaidiana na Serikali kuboresha huduma ya maji kwa pande zote.

Mheshimiwa Spika, ombi lingine tunawashukuru na tunawapongeza mmeweza kuondoa kodi kwenye vifaa au mashine za kuchonga vito, lapidary na za kutengenezea jewellery. Tunaomba sasa mfike hatua ya pili kwa sababu hatua ya kwanza mmeondoa duties, mngeondoa na VAT kabisa ili sasa zile mashine ziwe za bei nafuu na Watanzania wengi watakaopata mafunzo pale Gem Center pale Arusha basi waweze kupata hizi mashine kwa bei nafuu zaidi. Kwa hiyo, mngeweza kutuondolea kodi kwenye hilo.

Mheshimiwa Spika, tunawashukuru kwamba mmeondoa kodi kwenye refrigerated trucks kwa ajili ya horticulture, lakini tunaomba mngetanua wigo zaidi ili uweze kuhusisha pia sekta ya maziwa, nyama na samaki kwa sababu bidhaa hizo mkiweza kuondoa kodi, wale wavuvi hawatahitaji kuuza samaki wao wanapovua, wanaweza kuzi- refrigerate kwa bei nafuu kwenye containers ambazo zitakuwa refrigerated za ushirika na hata wale wa kuku badala ya kuuza kuku kwa haraka kwa bei ya chini, wanaweza kuwa-process na kuwaweka kwenye fridge wauze taratibu ili mkulima aweze kufaidi moja kwa moja. Kwa hiyo, pamoja na kuwa mmesaidia Sekta ya horticulture mngetanua wigo kwenda kwenye maziwa, samaki na lakini pia kwa upande wa nyama. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lingine ni ombi la kuondoa kodi kwenye solar waterpumps itasaidia sekta ya maji kwa upande wote lakini pia ukileta kama umwagiliaji, kodi hizo hazilipiwi lakini ukileta hivihivi bila kutaja umwagiliaji ina kodi. Kwa hiyo, inaleta usumbufu mkubwa, mngeziondoa ili sekta nzima ya maji iweze kupata…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Ahsante Mheshimiwa Jitu Soni.

MHE. JITU V. SONI: Ahsante, nashukuru na naunga mkono hoja mia kwa mia. (Makofi)