Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Allan Joseph Kiula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. ALLAN J. KIULA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kuweza kunipa nafasi na mimi niseme maneno machache katika bajeti hii.

Mheshimiwa Spika, cha kwanza naunga mkono hoja, cha pili natoa pongezi kwa Wizara kwa maana ya Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri na watendaji na naposema watendaji namaanisha wataalam, hili suala la wataalam nasisitiza kwa sababu wakati mwingine tulikuwa tukichangia humu bila kuzingatia utaalam wa watu ndio maana tunakuwa tumekazana kukosoa. Lakini pia nipongeze Wizara kwa kufuta tozo 54 hii ni historia, watu wengi walitarajia labda vinywaji vitapanda bei na nini lakini sasa naona Mheshimiwa Dkt. Mpango amewapiga chenga. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia ile tax ammnesty na kutolewa kwa extension nitoe pongezi na nisisitize tu kwamba Wizara iongeze juhudi za kufuatili hasa hiyo kodi iweze kupatikana. Lakini pia suala la biashara miezi sita, watu wanaoandikishwa TIN kupata ule msamaha kwa miezi sita ni jambo kubwa sana, isipokuwa katika kuchangia hapa nimesikia kuna kitu kinaitwa bajeti hewa. Sasa nilijaribu kujiuliza bajeti hewa ni kitu gani, lakini bajeti hiyo ikashushwa hadi trilioni 29.

Mheshimiwa Spika, kwa kumbukumbu waliosoma ile sura ya bajeti tuliona kwamba vipo vyanzo vimewekwa vyanzo hivyo ndio vinakwenda kwenye shilingi trilioni 33 na baadhi ya vyanzo hivyo ni kodi na mapato ambayo tutakutana nayo ambayo sio ya kikodi lakini kuna mikopo ya ndani na nje na kuna misaada, sana sana ninachoweza kusisitiza ni kwamba Wizara sasa ifanye close monitoring iweze kufuatilia hivi vyanzo hivi viweze ku- perform hilo ndio jambo kubwa, kwa sababu kila siku bajeti inakuwa kulingana na mahitaji na kuna commitment zinaongezeka kulingana na mahitaji, kwa hiyo hatuwezi kuwa tunarudi nyuma tunasonga mbele. Pia tutambue kwamba katikati huwa kuna mid review ambayo huwa inafanyika kuangalia hivi vyanzo vina perform vipi, kwa hiyo ni mambo ya kitaalam ndio maana nilisisitiza suala la wataalam. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo lingine ambalo ni muhimu mimi nikalizungumza kwa sababu nina uzoefu nalo kidogo ni suala zima la clearing and forwarding. Suala la kwanza ni kujiuliza kwa nini tulianzisha clearing and forwarding na wanatambuliwa na nani, ndio maana wengine waliochangia wakasema kuna WCO inawatambua, East African Custom Management Act ya mwaka 2004 inatambua jambo hilo, kwa hiyo jambo hilo ni kubwa sana, lakini pia tuangalie historia ya TRA zilikuwa taasisi tatu zikaunganishwa ndipo ikatoka TRA walikuwa wanafanya kazi vipi na kulikuwa na mapungufu yapi.

Mheshimiwa Spika, sasa hivi tunakwenda ni suala la IT system, kwa hiyo hawa watu wa clearing wanatumia mtandao, kwa maana hiyo ni lazima tuangalia hawa watu tunaosema kila mtu a- clear mzigo wake tutamuwekea huo mtandao kwenye simu. Lakini kuna vibali kutoka kwenye taasisi mbalimbali hivyo vibali watavipata kwa utaratibu upi. Kwa hiyo jambo hili tusije tukaliendea kwa pupa lazima liwe na uratibu mzuri na liangaliwe kwa karibu na lengo kubwa Serikali iweze kupata mapato yake, kunaweza kuwekwa exceptional labda kwenye loose cargo au mtu amekuja na television yake moja airport jambo hilo linatakiwa liangaliwe lakini suala la kumbukumbu ni muhimu sana pamoja na kodi suala la kumbukumbu ni muhimu sana. Kwa hiyo jambo likiangaliwa kwa ujumla wake wamezungumza mambo ya ajira, lakini mimi nilikuwa naangalia modality ambayo tutakwenda kuitumia ni modality ipi kwa sababu hatutaki ku- frustrate suala zima la ukusanyaji wa mapato. Hilo ni jambo muhimu, tunaomba Mheshimiwa Waziri uweze kuliangalia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo lingine ambalo ningependa kulizungumzia ni suala la kodi ya mafuta; ukurasa wa 60 wa kitabu wanasema kutoa ushuru wa forodha wa asilimia 25 kwenye mafuta ghafi. Mwaka jana tuliongeza kodi hapa, lakini mafuta yameendelea kuja na hakukuwa na upungufu wa mafuta/hakuna impact yoyote ya ile hatua iliyochukuliwa na Bunge ya mwaka jana na ziko sababu mbalimbali. mimi baadae nitaleta mapendekezo lakini nilikuwa nafikiri na ninaona hiyo itakuwa ni busara kwenye mafuta ambayo ni ghafi asilimia 25 au dola 250 kwa tani. Pia kwenye mafuta ambayo yako processed asilimia 35 au dola 300 whichever is higher maana yake kunakushuka wanapokuja ku-declare wanasema bei ya mafuta kwenye soko la dunia imeshuka.

Mheshimiwa Spika, mimi nilijaribu kuangalia takwimu mbalimbali nikaona zile bei kweli zinaonekana zinashuka. Kwa hiyo kama bei hizo zinaonekana zinashuka sisi tunapoteza kipato, kwa hiyo wakiweka ile tag ya dola 250 kwa tani au ukiweka tag ya dola 300 ina maana Serikali itapata mapato yake. Lakini pia tumezungumza hii sababu hili jambo ni muhimu sana kwa sababu huku tulisema ukurasa wa 62 nanukuu walisema; “ongezeko la ushuru wa forodha linatarajiwa kuhamasisha uchakataji wa mbegu za mafuta hapa nchini na kuongeza ajira viwandani na mashambani.” Sasa kama hilo ndio lengo na tunataka tuongeze uzalishaji wa mbegu hapa ndani na uchakataji lazima tuweke ile tag ili kuweza kuhamasisha huku lakini pia ziko measures Wizara ya Kilimo inabidi kuchukua ili kuhamasisha uzalishaji wa mbegu za ndani.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo jambo hili nilipenda kulizungumzia liweze kunufaisha viwanda vya ndani lakini pia liweze kunufaisha wakulima kwa ujumla wake. Sasa hivi bei ya mashudu nikitoka hapo kuna mbei ya mashudu kwa mkulima ni shilingi 200 lakini bei hiyo imeshuka kutoka shilingi 400,300 mpaka imefika shilingi 200, kwa nini kwa sababu ya ada na tozo zingine ambazo hazikuzungumziwa kwenye tozo zilizofutwa. Kwa hiyo ningeomba kama ningeomba kabisa ile tozo ya shilingi 20,000 kwa tani iweze kufutwa itakuwa ni hatua kubwa sana. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Allan malizia.

MHE. ALLAN J. KIULA: Mheshimiwa Spika, kwa kumalizia naomba Wizara waangalie ili waongeze juhudi za formalization ya informal sector kwa sababu huko ndio tutakusanya kodi watu wawekwe kwenye mfumo wa kodi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuchangia, ahsante. (Makofi)