Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. DAVID E. SILINDE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana na mimi kunipatia fursa hii kuchangia hotuba ya bajeti kwa mwaka 2019/2020. Mimi napenda kuanza kwa kusema kwamba duniani kote maendeleo ya nchi hayategemei kodi peke yake na ninalisema hili kwa sababu wimbo humu ndani sasa hivi imekuwa ni kodi, kodi, kodi, taratibu za kikodi, sasa leo mimi nitazungumza zaidi kwenye kushauri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kodi ni moja ya kitu ambacho kinasaidia maendeleo, lakini kodi asilimia kubwa ya nchi nyingi inatumie kwenye kulipa mishahara na recurrent budget kwa maana hizi OCs, matumizi mengineyo.

Mheshimiwa Spika, dunia ya sasa kama unataka kuendelea, kuna njia kubwa mbili tu za kufanya; jambo la kwanza ni Foreign Direct Investment na jambo la pili ni Private Public Partnerships. Hayo ndiyo mambo makubwa ambayo yanaweza kukutoa kwenye kasi ile ambayo dunia inaitaka ya sasa.

Mheshimiwa Spika, leo tumepitia hotuba ya Wizara ya Fedha na kwenye hotuba ya Wizara ya Fedha na baadhi ya hotuba zilizotangulia, Serikali ya Chama cha Mapinduzi, imeainisha baadhi ya miradi ambayo bado haitekelezeki.

Mheshimiwa Spika, wameelezea Mradi wa LNG wakati wa Nishati na Madini kwamba uko kwenye negotiation, wameelezea mradi, kwa mfano mradi ambao mwingine umekufa wa Bandari ya Bagamoyo, kuna Mradi wa Liganga na Mchuchuma, kuna Mradi wa SGR na kuna Mradi wa Stiegler’s Gorge. Miradi hii ingetumia mfumo wa FDI na PPP, hebu fikiri leo uchumi wa Tanzania, tumekuwa katika level gani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, LNG dola bilioni 30, unazungumzia trilioni 70 za kitanzania; Bandari ya Bagamoyo, endapo tungeingia mkataba vizuri kabisa, dola bilioni 10, sawasawa na trilioni 24, Liganga na Mchuchuma - dola bilioni tatu, sawa na trilioni saba, SGR trilioni 17 yaani ukimaliza phase nzima na Stiegler’s Gorge trilioni sita. Yaani unazungumzia uchumi ungeongezeka kwa wakati mmoja kwa trilioni 124. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, leo pato letu la Taifa ni trilioni 125, fikiria hizi fedha zingeingia ndani ya uchumi wetu, trilioni 124 kwa wakati mmoja, nakuhakikishia leo Serikali ya awamu ya tano ingekuwa ime-double GDP ya Taifa letu, lakini tatizo liko wapi, watakwambia mikataba mibovu na weakness ambayo tumekuwa tukiifanya kila siku kwenye miradi mikubwa kama hii, yaani wewe ukigundua kifungu kibovu na mkataba wote huutaki, wakati utaratibu wa dunia nzima, kama kuna mahali pana shida, unakwenda una renegotiate. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa hebu angalia trickle down effect kwenye masuala kama haya, leo ajira zingekuwa bwerere kila mahali, kwa sababu kila mtu angepata ajira kwenye maeneo hayo kwa mfumo huo kwa hizo fedha ambazo karibu trilioni 124 zingeingia ndani. Viwanda vingekuwepo vingi nautolea mfano, Bandari ya Bagamoyo peke yake, ilikuwa tu siyo bandari, the whole project ilikuwa na viwanda zaidi ya 1,000 pale. Sasa haya yote yangekuwa yanafanyika kwa wakati mmoja, leo maendeleo yote yangebadilika. Sasa sisi tunatumia fedha za ndani na wakati mwingine tunakopa kwenye mabenki ya kibiashara ku- finance miradi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, na mfano mzuri, SGR tunakopa kwenye mkopo wa kibiashara, Stiegler’s vilevile, tunakopa vilevile humo ndani, tutaanza kulipa kabla hii miradi haija- mature!

Mheshimiwa Spika, na ninayasema haya kwa sababu moja tu, SGR awamu ya kwanza, Dar es Salaam - Morogoro, mpaka sasa umetekelezeka kwa asilimia 48. Bado hatujafika Morogoro, 48% tutakuja kumaliza mwaka gani na tunakwenda kwenye uchaguzi mwakani. Morogoro - Makutupora mpaka sasa umetekelezeka kwa asilimia saba tu, bado asilimia 93! Kwa mwendo huu Rais Magufuli anaweza kuondoka madarakani miradi hii haijakamilkka bado. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini pili, Stiegler’s Gorge mpaka sasa hivi mradi ni kwamba upo tu kwenye ma-study, wametoa bilioni 700, haujaanza ku-mature na tunahitaji umeme ambao ile reli itakapokamilika inatakiwa ianze kutumia ule umeme. Sasa haya yote ni kwamba tunakwenda lakini tunakwenda in a slow, very slow yaani mwendo wa konokono. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa ni vizuri na Mheshimiwa Rais, nakwambia anataka kusikia maneno kama haya, hataki kusikia vitu vingine. Sasa kinachotokea ni nini, Bunge tunashauri, lakini haya mambo hayamfikii!

Mheshimiwa Spika,na mimi kuna kitu kilinishangaza sana, siku ile Mheshimiwa Rais wakati anazungumza na wafanyabiashara, nikawa najiuliza swali, hivi yale yaliyozungumzwa na wafanyabaishara, humu ndani Bungeni hatujawahi kuyasema? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, na kama humu ndani hatujawahi kusema, basi sisi wote hatustahili kuwa Wabunge. Kama hatujawahi kuyasema maana yake hatustahili kuwa Wabunge na kama tumeyasema, hayafiki, tafsri yake ni kwamba kuna watu ni washauri wabovu kabisa wa Mheshimiwa Rais. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, na hii ninaisema kwa sababu moja, mwaka 2006 nikiwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam pale Rais Thabo Mbeki wakati ule alikuja pale, akafanya mdahalo Nkrumah, sasa pale Nkrumah alituambia hivi, kazi ya Urais inaweza kuwa ngumu kama una washauri wabovu na inaweza kuwa rahisi kama una washauri wazuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, na ukisikia huko mtaani, unamsikia Rais Magufuli analalamika, Urais mgumu, Urais mgumu! Kumbe jibu ambalo Mbeki alituambia pale Chuo Kikuu cha Dar es Salaam mwaka 2006 ndiyo leo naliona kwamba amezungukwa na washauri wabovu, ndiyo maana anaona kazi ngumu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, leo Rais anakutana na wafugaji, Rais anakutana na wafanyabiashara, Rais anakutana na wachimba madini wadogo, Rais ata…, yaani Rais anafanya kila kitu mwenyewe! Bunge tunafanya kazi gani? Hasa hayo ndiyo maswali ambayo yanamnyima… (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mimi nimelisema hili kwa sababu mwaka jana kwa mfano Kamati ya Bajeti tulikuja hapa na mapendekezo 11, Serikali ilikataa mapendekezo yote ndani ya Bunge hili! Baada ya miezi mitatu mambo hayajaenda vizuri, mchuzi wa zabibu, katikati ya mwaka wa fedha tukaletewa sheria ya mabadiliko hapa, Rais kule alishapigwa fix, katikati ya mwaka wa fedha tumekuja kubadilisha mapendekezo, mwaka huu wameleta mengine kama matatu, bado kama manne hivi. Sasa haya yote, ndiyo matokeo ya watu kumshauri vibaya Mheshimiwa Rais. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, na Rais anapaswa kushauriwa kwamba unajua na Mheshimiwa Mpango hili unajua, haya mambo ndiyo Rais anakiwa aelimishwe beyond reasonable doubt! (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tukizungumzia, mimi kila siku, siku moja nilizungumzia Rwanda, nimesoma mfumo wa Rwanda. Rwanda Rais Kagame, kabla hajafanya jambo, anaruhusu watu wafanye study analysis, wanakwenda zaidi ya mara tatu, yaani watu wanasoma mfumo sawasawa. Sasa study ya kwanza, study ya pili, study ya tatu, wanajiondoa na wasiwasi wa kutekeleza mambo, baada ya hapo, wanakwenda kutekeleza wakishakuwa wameondoa doubts zote katika ule mkataba. Sasa leo Tanzania, nikawa najiuliza hii mikataba tunayoikimbia, ina maana sisi hatuna hata wasomi/wanasheria wanaoweza kuandika mikataba vizuri! (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ee, tunakaa na watu ambao wanafikiri tu kodi ndiyo inaweza kuleta maendeleo nchi hii, fedha za ndani ndiyo zinaweza kuleta maendeleo nchi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, yaani, with this, namna, hata ukiwapa miaka 100 hakuna chochote watakachokifanya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa we have to think in a different way na haya mamabo mmpelekeeni Mheshimiwa Rais aweze kuyafanyia kazi, kinyume na hapa, tutakwenda tu, tutabidi tu kwamba Bunge basi limalize kazi yake, awe anafanya mwenyewe pale Ikulu awe anaita sijui viongozi wa dini, asikilize maoni yao, na haya mengi tunayoyasema hapa!

Mheshimiwa Spika, waambie watu wako waache kuchujachuja sana haya mambo, yaani wanayakata sana, watu wanataka kusikia huko, taarifa haziji kama zilivyo, kwa hiyo, matokeo yake ni nini, lazima watu muwe na uwezo wa kusikiliza both sides, mambo mazuri na mambo mabaya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, hili niliamua niliseme kwa sababu ndiyo namna pekee ambayo tunaweza tukatoka hapa tulipo, tukaenda mbele zaidi, lakini kitu kingine tulizungumzia kuhusu kilimo. Mimi nimejaribu kusoma, Tanzania sasa hivi tunataka uchumi wa viwanda, lakini hatuwekezi kwenye kilimo! Jana mimi nimejaribu kupitia kwenye mitandao, kwenye kusoma journals nyingi, nchi zote zilizokuwa kiviwanda, kwenye first generation ya agriculture revolution, second generation ya agriculture revolution na third generation ambayo ilikuwa ni ya China, wote kabla ya kwenda kwenye viwanda, waliwekeza kwenye kilimo. Kilimo kilipozidi, ndipo wakaenda kwenye viwanda. Sisi tumekwenda kwenye sera ya viwanda wakati hatuna malighafi na ndiyo maana mnaona, sera ya viwanda haitekelezeki! (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa sababu wewe mwenyewe unajiuliza, leo, hivi unaenda kuanzisha kiwanda, wakati huna pamba ya kutosha, unakwenda kuanzisha kiwanda wakati tumbaku yenyewe imeshuka kutoka uzalishaji wa tani milioni 150 mpaka tani 350,000. Pamba yenyewe imeshuka, korosho imeshuka, tunaanzisha kiwanda kwa malighafi ipi? Za kuagiza kutoka nje ya nje ya nchi! Kasome First Agriculture Revolution, kasome Agrarian Economy, kasome The Green Economy ya China, wote watakwambia causative ya viwanda, causative ya mabadiliko ya viwanda ilitokana na kilimo kikubwa na cha kisasa, ndiyo wakaenda katika uchumi wa viwanda. Ahsante sana. (Makofi)