Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Susan Anselm Jerome Lyimo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. SUSAN A. J. LYIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa fursa hii na nashukuru sana kwamba leo nasimama kuongelea suala la bajeti ya mwaka 2019/2020. Uzuri wa bajeti au ubaya wa bajeti tunaangalia utekelezaji wake na siyo uwasilishwaji wake wether umewasilishwa kwa mbwembwe namna gani, tunaangalia utekelezaji wake wa miaka iliyopita na hapa nina bajeti ya mwaka jana iliyosomwa na kaka yangu Dkt. Mpango na ukiangalia vipaumbele, tunaangalia vile vipaumbele je vilitekelezwa ama havijatekelezwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tukiangalia kipaumbele cha kwanza kabisa mwaka jana ilikuwa ni kilimo na kilimo hicho kilikuwa ni kilimo cha umwagiliaji, ni wazi kwamba bado nchi yetu haijajikita kwenye kilimo cha umwagiliaji. Wote tunajua kwamba sasa hivi kwa kweli kilimo cha kutegemea mvua hakiwezekani kutokana na mabadiliko ya tabianchi. Pamoja na kwamba wameendelea kujitahidi kiasi kidogo, tunategemea kabisa kwa kuwa nchi hii sasa ni ya viwanda ni lazima tufungamanishe bidhaa zinazotokana na kilimo ili sasa ziende zikachakatwe kwenye viwanda na hivyo kuweza kupata fedha.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini ni ukweli kwamba bado kilimo cha umwagiliaji hakijapewa kipaumbele na hata ukiangalia bajeti ya mwaka huu katika vipaumbele vya kilimo hicho kilimo cha umwagiliaji pia bado hakijawekwa kabisa. Kwa hiyo, nilikuwa natoa ushauri tu kwamba ni muhimu sana nchi yetu inarutuba nzuri na kila mahali kuna mazao tofauti, kwa hiyo nilikuwa naomba sana na ni ushauri sababu tumekuwa tukishauri mara kwa maralakini ushauri huwa haupokelewi. Kwa hiyo Mheshimiwa Mpango nchi hii kama tunataka nchi hii tujiondoe hapa tulipo tuweze kujitegemea ni lazima tuwekeze vizuri sana kwenye kilimo cha umwagiliaji kwa sababu tunajua kwamba Tanzania kama nchi zaidi ya asilimia 70 ni wakulima na kati ya hiyo asilimia 75 ya hiyo 70 ni wakinamama, kwa hiyo kama akinamama watakuwa kwenye lindi la umaskini, maana yake nchi hii haiwezi kuendelea kwasababu hakuna jamii iliyotelekeza wanawake ikaendelea. (Makofi)

Kwa hiyo, ninaomba sana sana suala la kilimo liendelee kupewa kipaumbele kwasababu kilimo na viwanda vinaenda pamoja. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini jambo la pili lilizungumziwa suala la wafanyabiashara, wote tumeona ni jinsi gani uwekezaji wafanyabiashara umekuwa mbovu katika mwaka huu unaoisha na ndiyo sababu sasa baada ya kuona na sisi tulivyopiga kelele nyingi kuhusiana na suala la kodi jinsi gani wafanyabiashara wanaondoka nchini, sasa naona hivi karibuni Mheshimiwa Rais aliita wafanyabiashara ninaamini sasa mnaanza kutuelewa na ushauri wetu mnaanza kuupokea kwa sababu nadhani tunaelekea kwenye mwaka wa uchaguzi, lakini hiyo itoshe kusema kwamba tutaendelea kutoa ushauri ambao ninaamini siku ambayo mtajisikia mtauchukua lakini tumekuwa kwenye hii mess kwa sababu ushauri mwingi ulikuwa haupokelewi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kipaumbele kingine kilikuwa ni kuhakikisha kwamba tunakuwa na Madaktari Bingwa, tunakuwa na vitendanishi, lakini tumeshuhudia katika hili Bunge maswali mengi ya Wabunge yakiulizwa kuhusiana na suala na madaktari bingwa hawapo lakini vilevile Hospitali za Kanda pamoja na kwamba tumekuwa na hospitali za Kanda, hospitali hizo hazina vifaa muhimu sana. Tumesikia habari MRA, lakini vilevile nimekuwa nikizungumza na Wabunge wengine wakizungumza katika hizi Hospitali ya za Kanda hususan Hospitali ya Kanda ya Kaskazini na ile ya Mbeya kwamba kumekuwa na tatizo kubwa sana.

Kwamfano Kanda ya Kaskazini - KCMC lengo ilikuwa kuhakikisha kwamba kwa sababu tunajua magonjwa yasiyo ya kuambukiza yamekuwa mengi hususan ugonjwa wa kansa na tukasema kwamba Hospitali ya Ocean Road ambayo ndiyo ilikuwa hospitali pekee inayoweza kutibu hasa kwa njia ya mionzi imelemewa, kwa hiyo Hospitali ya Bugando na Hospitali ya KCMC zikawa zimewekwa mahsusi kwa ajili ya kusaidia.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni jambo la kusikitisha kwamba pamoja na juhudi hizo bado Hospitali ya KCMC ambayo tayari inaweza kupata hiyo mashine, lakini Serikali imeshindwa kujenga kile chumba kwa ajili ya kuhifadhi mashine hizo. Kwa hiyo nilikuwa naomba kwa kweli wananchi wengi wamekuwa wanakufa kwa kukosa huduma za hospitali. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini sasa ukija kwenye bajeti ya mwaka huu kwa kweli mimi nasikitika sana kama mwanamke kuona kwamba bajeti hii Katiba yetu inasema kusiwe na ubaguzi wa aina yoyote, lakini kumekuwa na ubaguzi wa kijinsia na bajeti hii imekuwa gender insensitive. Kwa nini nasema hivyo suala la hedhi ni suala la kibaologia na sisi tulifurahi sana mwaka jana walipoondoa VAT kwenye pads (taulo za kike) na tumeenda hata nchi za nje kutangaza Tanzania ikaonekana kwamba imepiga hatua kuhakikisha kwamba na lengo kubwa lilikuwa ni kuhakikisha kwamba watoto wa kike wanakwenda shule ziku zote za masomo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, wewe ni shahidi kwa sababu ni mwanamke kama mimi, watoto wa shule wa kike wanaotoka kwenye familia maskini wanakosa takriban siku 70 kwa mwaka kwa sababu ya masuala hayo niliyoyazungumza. Tulipiga vigelegele baada ya VAT kuondolewa, leo Mheshimiwa Waziri anasema wameifuta na sababu ya kuifuta wanasema kwa sababu lengo halijatimizwa. Hii ni Serikali, Serikali ina vyombo vyake vya dola ina vyombo vyake vya TRA ina kila kitu kuhakikisha kwamba kitu kikiisha pitishwa na Bunge kinaenda kutekelezwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama mifuko ya rambo ya plastiki imepigwa marufuku na tumeona utekelezaji wake kwa nini jambo kubwa kama hili linalohusu takriban nusu ya Watanzania lishindikane! Mimi naamini hata kama hao wauzaji au wasambazaji wamefanya hivyo Serikali bado ile VAT ambayo ni 18% wangeweza ku-ring fence kwa mfano mimi nachukulia mfano kuna wanawake kwa sababu watu katika umri huo ni kuanzia miaka 12 mpaka 50 sasa tukichukulia kama ni wanawake hawa au wasichana milioni 10 tuchukulie tu milioni 10 kwa mwaka yaani kwa maana ni kila mwezi kwahiyo hawa wanatumia labda pad moja ile I mean ile packet moja au wengine mbili, kwa hiyo tuchukulie wote ni moja kama wangechukua hiyo VAT ambayo ni 360 shilings kwa watu milioni 10 mara miezi 12, maana yake tungekuwa tumepata shilingi bilioni 43 kwahiyo Serikali ituambie hata kuzi-ring fence hiyo VAT wameshindwa? Kama kweli tatizo lilikuwa ni wasambazaji kwa nini wasinge-ring fence hiyo ili walau hizo fedha zinazopatikana basi ziwasaidie watoto wa shule ambao wataenda shuleni.

Kwa hiyo, mimi nadhani hilo ndiyo lingekuwa sasa wameifuta halafu mbadala wake ni mimi? Kwa sababu mimi nina hakika kuna watu tumewaona ambao wanatengeneza tayari walishusha, kwa hiyo wanatuambia tatizo ni wale wasambazaji. Kwa hiyo wasambazaji hao Serikali kama imeshindwa basi wa-ring fence hiyo hela halafu hiyo hela iende ikanunue hizo pad bure wagawe bure kama ambavyo wanafanya wenzetu wa Rwanda wenzetu wa South Africa na wenzetu wa Kenya, kwa hiyo huo ni ushauri wangu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niendelee pia kuzungumzia hilo suala la ubaguzi, tunaangalia tunaona kwamba this time wamekuja Serikali inasema wanakusanya inaenda kukusanya kwenye wigs. Wigs ni bidhaa kwa ajili ya wanawake mawigi kwa Kiswahili. Lakini kuna watu natural hawana nywele, kwa hiyo lazima wavae hizo na unaona humu ndani mwangalie Esther Matiko, Susan Kiwanga umeona jinsi wamependeza, kwa hiyo kuna wengine hawana nywele natural wana vipilipili, kwa hiyo hizi zimeletwa kwa ajili hiyo. Kwa hiyo naendelea kusema kuwa kwa nini hawajachagua bidhaa ya wanaume waiwekee kodi wanachagua bidhaa za wanawake. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo mimi nadhani kwa kweli kuna kila sababu ya kuwambia Waziri kwamba hii bajeti imekuwa very gender insensitive na hatuwezi kukubaliana nayo, nilitegemea Wabunge wanawake tuandamane kupinga hili jambo, siyo hilo moja tu hasa hilo la pad. Lakini nimeanza kwa kauli ya kusema kwamba uzuri wa bajeti ni utekelezaji wake.

Mheshimiwa Naibu Spika, angalia Wizara hizi mwaka jana kwa mfano Wizara ya Kilimo kama nilivyosema ambayo ndiyo inayoongoza kwa ajira ilikuwa imetengewa shilingi bilioni 48 lakini mpaka mwisho imepata only asilimia 42, ukija kwenye upande wa Viwanda na Biashara is even worse ilikuwa imepangiwa shilingi bilioni 90...

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)