Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Daniel Edward Mtuka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. DANIEL D. MTUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa fursa hii na mimi nitoe mchango wangu katika bajeti kuu pamoja na taarifa ya hali ya uchumi, pamoja na Taarifa ya Kamati ya Bajeti. Namshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa zawadi ya uhai ametukutanisha mpaka leo hii pia tunajadili tena bajeti kuu kama tulivyokuwa tumejadili miaka iliyopita. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niende moja kwa moja kwenye majadala. Mimi nikupongeze Waziri Dkt. Mpango, uko kwenye njia sahihi, kelele nyingine hizi kila mmoja ana mdomo wake na ana uhuru wake, lakini angalia kwenye focus yako ndani ya miaka mitano uko kwenye right track na sisi Wabunge kazi yetu ni kuishauri Serikali. Naomba utege sikio sasa usikilize ushauri wa Mbunge anayeitwa Mtuka. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, twende ukurasa wa 80 wa hotuba yako, nikupongeze umetoa umeondoa ule ushuru wa uwindaji wa kitaalam kwa wazalendo pamoja na wageni, hii ni katika kuvutia na kukuza biashara ya utalii, sawa. Naomba nikuongezee na lingine, ukienda pale Wizara ya Mambo ya Ndani, Immigration pale, kuna kitu kinaitwa tozo ya kibiashara hii ambayo wanailipa wale wanaokuja kufanya mikutano ya kimataifa kwenye kumbi zetu, Mheshimiwa Kigwangalla amejinasibu vizuri kwamba sasa anakwenda kujenga kumbi kubwa na nzuri kwa mfano Bagamoyo, sasa muondolee hii tozo hii maana ndio wanayolipa hawa wanaokuja kufanya mikutano, huu ndio utalii wa mikutano. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nitoe tu mfano mfupi sana, Ethiopia wenzetu wanalipa dola 32, Kenya dola 40, Rwanda dola 50, South Africa dola 150, sisi tunatoza dola 250; ninashauri sana tutoze kama jirani zetu dola 40 vinginevyo Mheshimiwa Kigwangalla asije akajenga hizi matembo weupe hawa.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niendelee mbele zaidi, katika kukuza utalii hukohuko hebu pia tuangalie kutumia au kukarabati viwanja vyetu vya ndege, hasa ambavyo viko kwenye mbuga zile za wanyama, nasemea moja kwa moja Seronera. Juzi juzi Serengeti imetunukiwa kuwa mbuga bora kuliko zote Barani Afrika, kutakuwa na wimbi kubwa sana la watalii ambao watakuja, watakuja wengi sana, lakini pia tunataka kuanza safari za kufuata watalii Guangzhou, Mumbai, Johannesburg, tutakuja na watalii wengi sana na wengi wamesikia watakuja tu Serengeti. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Serengeti lile ni likubwa sana, hebu chukulia ile 10 percent tu ya Serengeti ambayo inaitwa Masai Mara iko Kenya, wenzetu wanatengeneza fedha mara kumi zaidi ya sisi ambao tunamiliki asilimia 90, lakini wenzetu wametengeneza viwanja vya ndege, viwanja vizuri kabisa mle ndani. Kwa mfano wana kiwanja kinaitwa Kichwatembo; Masai Mara mle ndani, wana Kiwanja kinaitwa Masai, Alikiombo pia, viko mle ndani; hivi viwanja vimeunganishwa na viwanja vikubwa nikizungumzia Embakasi na Jomo Kenyatta.

Mheshimiwa Naibu Spika, ndege kubwa ikitua pale inakuta tayari hizi Q400 iko tayari pale imeshawasha moto inasubiri wale watalii wanashuka comfortably wanaingia kwenye ndege zile wanaenda kutua Masai Mara kwenye vile viwanja, viwanja vile vimejengwa vina minara ya kuongozea ndege, taa za usiku, taa za kuongozea ndege, lami imewekwa. Sisi cha kwetu kile Seronera hakijawekwa, watalii watakuwa ni wengi mno tunawa-accommodate vipi wale? Tutakosa fedha hapa ambayo ni ya bure ni nje-nje hapa hii pesa, hii pesa tunaikosa hii. Naomba turekebishe kile kiwanja, chomoachomoa kwenye matengenezo ya viwanja vingine vya ndege hebu tuanze na Seronera tukitengeneze kile kiwanja zile ndege zitue kule zipeleke hawa watalii ni wengi mno, hii fedha sio ya kuiachia Mheshimiwa Mpango. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini niende kwenye eneo lingine la kuboresha Shirika la Ndege; ndege hizi tumenunua za kutosha, tunaendelea kununua kama ambavyo tumejiwekea, ndio focus yetu. Mheshimiwa Rais ametusaidia tuna ndege sita na nyingine zinakuja, lakini pia mimi niseme tiketi peke yake kwenye ndege hizi hatutaweza kuendesha Shirika la Ndege. ziko shughuli nyingi ambazo tunaweza kuzifanya ATCL ikawa shirika tanzu kutoka kwenye ATCL tukawa na vikampuni vidogo vidogo vya kuendesha shughuli kama zifuatazo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ya kwanza; tuwe na shirika dogo ambalo linaendesha zile ground handling services ambazo Swissport wanafanya sasahivi. Hii itafanya huduma hizi kwa ndege zetu za ATCL, lakini pia na kwa makampuni mengine tutatengeneza fedha; tutaokoa fedha kwenye kampuni yetu, lakini pia tutafanya huduma kwenye ndege nyingine tutatengeneza fedha.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia tufanye shughuli nyingine inayoitwa in flight catering services, vyakula na vinywaji kwenye ndege ndani ya ndege zetu hizi. Tutengeneze ka-kampuni kadogo tanzu ka ATCL tuuze vyakula kwa kutumia kampuni hii, tuachane na mambo ya ku-hire ni gharama kubwa sana, tutauza vyakula, vitahudumia vyakula kwenye ndege zetu, lakini pia tutahudumia kwenye ndege nyingine, tutatengeneza fedha ya kutosha tu Mheshimiwa Mpango. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini nyingine kuna tozo kama navigation charges; navigation charges ni kama zile ndege inapokuwa inatua lazima waelezwe hali ya hewa, sijui minara kwa mfano ya simu au umeme, zile tower kwa usiku zinakuwa zinachanganya. Kwa hiyo, kunakuwa na ile ramani ambayo inamwongoza rubani, hizo navigation fees.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna fees zingine zinaitwa landing charges na parking charges. Mheshimiwa Mpango hizi gharama yake ni kubwa mno, inakaribia bilioni moja kwa mwezi ATCL inalipa, fikiria hii. Lakini nchi zingine kama kwa mfano Ethiopian Airlines, wale waaarabu kule Emirates kwa mfano Qatar Airways haya ni mashirika ya Serikali. Wamefanya exemption ya haya mashirika, hawalipi hizi charges tatu nilizozitaja, kwa hiyo wana-save. Kwa mfano, tuki-save bilioni moja kwa kila mwezi maana yake ni kwamba tunajiendesha hili shirika. Tuangalie hizi charges angalau tuwape hata muda mfupi wakati linakua tuziondoe hizi charges tatu, ni mwiba mkubwa mno, tufanye exemption, tutakuwa tumelisaidia sana shirika letu la ndege.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunacho chuo kinaitwa ATC Cabin Crew School, hiki ni chuo kinachofundisha hawa ma- airhostess peke yake, hakiwafundishi marubani, marubani wanaenda kufundishwa maeneo mengine nchi za nje, hawa fresh kutoka shuleni. Tukisema hebu tuanzishe kozi sasa na kufundisha marubani pia tuwafundishe humu humu ndani. Kufundisha rubani mmoja kwa wastani ni shilingi milioni 80 kwa mwaka, ni hela nyingi sana, rubani mmoja huyu lakini tukiwa tunawafundisha humu ndani tutapunguza gharama, tuta-save, tutaokoa hii ATCL, tutakuwa tumeweza kulifufua. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, huduma nyingine, tunayo ma-godown. Kuna bidhaa zinaitwa sensitive goods; temperature ya sensitive goods. Kwa mfano mtu labda ametoka nje ametua hapa anaenda Malawi, ana goods zile ambazo ni sensitive na joto labda dawa zitaharibika, tutengeneze godowns, ni biashara nzuri mno, zile goods ambazo zipo on transit ni biashara nzuri mno; anasubiri ndege tunamtunzia bidhaa zake pale, unaona eeh baada ya kutimilika safari anachukua bidhaa zake anaondoka kwenda Malawi, ametuachia pesa. Tiketi peke yake si biashara ya ndege, ndiyo maana tunatoza labda kwa mfano tu Dodoma - Dar es Salaam hapa hela ni nyingi mno shilingi 400,000 mpaka shilingi 500,000 lakini tukizingatia haya Mheshimiwa Mpango na Wizara nyingine, unaweza ukaenda kata kwa 100,000 tu Dodoma – Dar es salaam… (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)