Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Prof. Jumanne Abdallah Maghembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwanga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. PROF. JUMANNE A. MAGHEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushuruku sana kunipa nafasi ya awali kabisa kuchangia hoja ambayo ipo mezani. Kwanza ningependa sana niwapongeze Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango, nimpongeze Naibu wake na timu yote ya Katibu Mkuu kwa kazi nzuri ambayo wamefanya, inaonesha wazi kabisa kwamba katika bajeti ya mwaka huu wamesikiliza sana na kuyaleta yale mambo ambayo tuliyapendekeza katika bajeti ile ya mwaka jana. Kwa hivi tunawapongeza sana kwa kuwa wasikivu na kuleta mapendekezo ambayo na sisi tunaweza kuongeza nyama ili mapendekezo haya yaweze kuwa mazuri zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, imefurahisha sana kwamba Mheshimiwa Waziri ameshughulikia zile kero ambazo ni ndogo ndogo na zinawasumbua sana wawekezaji, kero zile ambazo zimewekwa na TBS, TFDA, OSHA, EWURA, SUMATRA na wengine. Hizi tunawapongeza sana kwa kuziondoa, lakini ninafikiri kwamba mngekwenda mbele zaidi. Uchumi wetu unategemea sana usafirishaji na hasa usafirishi wa nchi ambazo zinatuzunguka. Moja ya kero kubwa sana ya watu ambao wanasafirisha bidhaa kupitia nchini kwetu na wafanyabishara walioko kando kando ya nchi kama Mwanza, Kigoma na kadhalika, ni kusimamishwa barabarani mda mrefu kabisa na polisi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, polisi wanakuwa ni wasumbufu wakubwa sana na nilikuwa namsikiliza hapa Waziri Waziri Mambo ya Ndani akitoa amri, ningependa utoe amri kwamba watu walio na mzigo yao wakishakaguliwa mara moja, wakakaguliwa mahali pengine mara ya pili waachwe waende nyumbani. Wanyarwanda wanachangua kutoka Kigali kwenda Mombasa kuchukua bidhaa zao kwa safari ya kilometa 7,200 round trip badala ya kutoka Kigali kuja Dar es Salaam ambayo round trip ni kilometa 3,200 kwa sababu tu magari yanaokwenda round trip ya kilometa 7,600 yanakwenda na kurudi mapema zaidi ya yale ambayo yanapitia Tanzania. Kwa hivi tuchukue hatua kali kabisa tuhakikishe kwamba polisi hawatuharibii biashara ya nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile ningependa tuchukue hatua ambazo zitatusaidia katika bajeti ambazo zinakuja. Moja hatua hizi ni kuweka msisitizo sana kwenye kilimo. Kilimo kimetajwa na ripoti zote za kamati ambazo zimewasilishwa hapo. Nitatoa mfano mmoja tu katika nchi yetu tuna maeneo ya umwagiliaji ya hekta 485,000 za umwagiliaji. Kama tungelima mpunga kwa kutumia kilimo cha kisasa, kutumia mbegu nzuri, kutumia mbolea ku-control magugu vizuri uzalishaji kwenye mashamba yetu ungefikia tani nane kwenye hekta moja, lakini uzalishaji wetu kwenye kilimo hiki cha umwagiliaji ni tani 1,500 na tunalima mara moja tu kwa mwaka kama vile kwenye mashamba ya kawaida yanayongojea mvua wakati katika mashamba haya ya umwagiliaji tungeweza kulima mara mbili hata mara tatu kwa mwaka kutegemeana na mbegu ambayo tungeweza kuchagua na kwa kuwafundisha wakulima, kwa kuwekeza katika kuwafundisha wakulima tungeweza kupata kwenye bajeti yetu mpaka dola bilioni tano/kumi kwa mwaka kutokana na mauzo ya mpunga kwa nchi za jirani zinazotuzunguka. Kwa hiyo, hebu tuweke nguvu kidogo kuwafundisha wakulima na ituletee mchango huu mkubwa ambao unaweza kupatikana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili ni uwekezaji katika utafiti wa kilimo ni mdogo sana, literal hakuna uwekezaji kabisa na bahati mbaya mwaka jana mwishoni kuna Mhandisi mmoja ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo alifuta uhandisi wote wa biotechnology na uhandisi jeni, nadhani alikuwa amechanganya uhandisi, uhandisi jeni na uhandisi wa mabomba na mambo mengine. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu umeona mwaka huu, nusu ya nchi imepata mvua za masika kuanzia mwisho wa mwezi Mei na mvua hizi kwa mazao tuliyonayo tunategemea mvua mwezi Februari, sasa kama hatufanyi uhandisi jeni, tunategemea nini hapo kesho? Wakati mabadiliko makubwa haya ya tabianchi yakitukumba, yapo mazao ambayo tunayapanda kwa siku hizi kiaibu kabisa. Kwa mfano, kwa nini tunatumia mbegu ya hovyo ya pamba wakati ambapo nchi zote duniani zinatumia bt cotton na sisi wenyewe tunavaa nguo wote hapa za bt cotton, lakini tunakataza Wakulima wetu wasitumie bt cotton wakaongeza uzalishaji mara tatu, wakazalisha pamba yenye nyuzi ndefu, wakapunguza kupuliza dawa mara tatu, badala ya kupuliza mara saba, wakapunguza, wakapiga mara tatu/mara nne. Wakapunguza na wadudu ambao wanakula pamba halafu tukaruhusu pamba iweze kupandwa nchi nzima kuanzia Chunya mpaka Lindi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tunafanya hivyo tumepiga marufuku Kusini kote huko kwa sababu pamba tunayopanda hapa nchini tunawalazimisha wananchi wanapanda ka pamba kale kanazalisha kilo 300 za pamba kwa hekta. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo ni muhimu sana tutoke pale tulipofika, maana pale nyuma tulikuwa tunaruhusu utafiti wa uhandisi jeni, tunaruhusu watu wa-test mazao ya uhandisi jeni kwenye controlled environment, lakini sasa tumepiga marufuku kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, maabara zetu zilikuwa ndiyo nzuri kupita zote Afrika nzima, zote tumefunga na wataalam wetu waliokuwa wazuri kupita Afrika nzima tumewasambaza kila mahali, wako frustrated. Mimi nadhani turudi pale tulipotoka, tufanye utafiti maana wananchi wetu kama wa Bukoba wasingeacha kula ndizi wakageukia ugali kama tungekuwa tuna-test mazao haya ya uhandisi jeni.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika ugonjwa wa mnyauko wana sayansi wetu waligundua kwamba ukiondoa gene ile ambayo ina udhaifu na virusi ya mnyauko, ukaweka gene ya pilipili hoho ndizi zinakuwa ambazo hazina mnyauko, sasa pilipili hoho tunapika, wakati tunapika matoke, sasa kama tukiiweka kwenye mgomba ina shida gani? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo ni lazima tubadilike na ni lazima tubadilike na tuende pamoja na dunia huwezi kuwa unavaa nguo za bt cotton halafu unawazuia wakulima wako wasikuze bt cotton wakati Kenya wanakuza bt cotton, Uganda wanakuza, Sudan wanakuza, Egypt, Mauritania, Nigeria wote wanakuza na nchi zingine zote duniani zinakuza. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa ukisema hii bt cotton ni mbaya, sasa uzuri wake ungekuwa nini, kwa sababu nguo ulizovaa ni za bt cotton, kwa hiyo nilikuwa nataka niishauri Serikali hili ni Serikali kwamba ifikirie upya marufuku yaliyopigwa katika utafiti wa uhandisi jeni.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho nilikuwa nataka nipige tena debe juu ya maabara...

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)