Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Peter Joseph Serukamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. PETER J. SERUKAMBA: Mheshimiwa Spika,na mimi nianze kwa kumpongeza Waziri wa Fedha kwa speech yake nzuri sana.

Mheshimiwa Spika, mimi nitaongelea kwa kweli jambo moja biashara na financial institutions. Asilimia 97 ya kazi Tanzania zinakuwa-offered na private sector, kwa hiyo, nataka tuelewane hapa vizuri kama kuna mwajiri wa kwanza mkubwa Tanzania ni private sector, so lazima huyu mwajiri huyu tumlinde, lazima tuje na instrument za kufanya huyu afanye vizuri zaidi.

Mheshimiwa Spika, tuna benki za biashara tuna benki ya maendeleo ama investment benki kazi yake ni nini. Kazi ya benki hizi ni kuchochea uchumi na biashara hata kama watapata faida lakini cha kwanza ni biashara wachochee. Sasa kinachotokea tungalie investment bank tunaifanyia nini ili iweze kufanya hiyo kazi vizuri. Lazima tuandae mazingira ili hii development bank ifanye vizuri zaidi watu wakope, wawekeze ili biashara ichangamke. Kwenye commercial bank biashara haiwezi kwenda kama commercial bank haziendi.

Mheshimiwa Spika, leo Ndugai umeanzisha biashara utanisamehe, umeweka mkopo benki/umeenda kukopa mkopo benki umeweka mortgage ukishaweka mortgage unapewa pesa. unakwenda kufanyabiashara unashindwa kulipa deni, ukishindwa kulipa deni benki inasema tunauza nyumba TRA wanakuja wanaweka kitu kinaitwa ganesh order kwamba sasa kabla hujachukua hela zako benki huyu tunamdai kodi, tupe kodi yetu, kinachotokea benki inafanyaje NPL zinapanda so leo TRA kwa... kwenye mortgage wao ni super power kuliko aliyetoa fedha maana yake ni nini, maana yake ni moja tu. Watu wengi hawatokopeshwa kwenye mabenki kwa sababu itabidi utajikuta wanaokopeshwa ni hao hao breweries, wakina Azam wale wale wakubwa, wadogo inaanza kuwa shida tukija hapa mbele tunasema kuna mikopo chechefu. Lakini wakati huo huo mabenki yanatoa fedha ikitoka hapo watu wanaenda mahakamani wanaweka order hawezi ku-escute ile order so mahakama inashughulika na banks, TRA inashughulika na banks, NPL zinapanda mabenki yanafanya nini yataanza kufunga branches, yataanza kufanya nini yataanza kupunguza wafanyakazi, yataanza kufanya nini fedha ambazo walikuwa wanalipa za cooperate tax zitaanza kupungua.

Sasa naomba Serikali au contract firming mtu anataka kujenga barabara anakuja anachukua mkopo anapewa anajenga barabara TRA wanakwenda TANROADS huyo mtu huyo tunamdai kabla hujamlipa kule benki tupe hela zetu kabisa, so the priority now is TRA kwa maana ya revenue ni jambo jema, lakini tusisahau kama hizi financial institutions zisipochangamka biashara haitochangamka.

Mheshimiwa Spika, mimi nasema kwa sababu ndiyo maana leo BOT wameshusha treasury bills rate, lakini bado kama unajua interest rate hazijashuka za mikopo kwa sababu gani? Risk bado ni kubwa na ni kwa sababu ya sera hizitunajichanganya. Kwa hiyo, mimi naomba jamani biashara ndiyo itakayofanya nchi hii twende kwa kasi .

Mheshimiwa Spika, kwa mfano mwaka 2015/2016 fedha iliyokuwa inakopwa kwa ajili ya agriculture ilikuwa asilimia 11.2, mwaka 2018 ikashuka to negative four, 2019 kumetokea jambo zuri na ningependa baadaye Waziri atuambie tumepanda kwa asilimia 45. Je, tumepanda 45% kwenye sekta moja hiyo ya korosho tu au na mazao mengine?

Mheshimiwa Spika, personal lending mwaka 2015/ 2016 ilikuwa asilimia 37.2; leo hii personal lending imeshuka kwa asilimia 17.5 maana yake ni nini? Kuna retrenchment watu hawaaminiki, kwa hiyo hawakopesheki. Waziri wa Uwekezaji anisikie mwaka 2015 investment kwa GDP ratio ilikuwa asilimia tano, leo investment imeshuka kwa 2.3 to ratio.

Mheshimiwa Spika, kwa nini nayasema haya maana environment ya biashara ndiyo itafanya kodi iongezeke, ndiyo itafanya tuweze kupata ajira. So lazima tunapotenga policy zetu tulinde biashara na Waziri amesema vizuri sana nimemsikia leo anasema katika sekta ambazo zimekua sana ya Mwakyembe na nyingine, lakini kilimo hakijakua sana, lakini kilimo ni 80% yaani population yetu wanaolima ni asilimia 80 hawa asilimia 80 growth yake asilimia tano sababu ni nini?

Mheshimiwa Spika, sababu ya kwanza tumeendelea kuwa na traditional agriculture bila ku-embrace commercial farming hatuwezi, mifano ipo Zimbabwe ni mfano madhubuti kwa kiburi cha Mugabe aliua commercial farming, leo wanakufa njaa na mashamba/ardhi si wanayo tuna ardhi kubwa sana nilisema juzi, lakini lazima tuje na mkakati wa growth, tujiulize maswali kwenye tumbaku tumekuwa? Kwenye kahawa tumekua? Kwenye pamba tumekua? Kwenye korosho tumekua? Twende huko lazima Waziri wa Fedha mwambie Waziri wa Kilimo tuanze kupambana kwa growth kwamba mwaka kesho seme tumetoka tani tano tumeenda tani kumi haya ndiyo maendeleo, lakini kama hakuna growth leo pamoja Tanzania tuna ardhi kubwa tunazalisha tani 50,000 za kahawa. Uganda tani 288,000 maana yake ni nini kuna kitu hatujafanya na ndiyo narudi kule tukifanya mabenki yafanye vizuri watakopesha wakulima, watakopesha wafanyabiashara, tutapata growth kwenye biasharara na tutapata growth kwenye kilimo.

Mheshimiwa Spika, kilimo ndiyo jambo pekee litakalofanya industrialization iwezekane, maana kilimo ndiyo raw material. Sasa lazima tuulizane hapa, hivi kweli tuna ardhi kubwa tunazalisha tani 19,000 za mkonge wakati tuna capacity installed ya tani milioni moja shida ni nini tunachukua mashamba tunakwenda kuwagawia watu wadogo wadogo, na mimi nasema mimi jamani naomba leo ni- declare kama kuna jambo siliamini ni ujamaa, siamini. (Makofi)

SPIKA: Ahsante sana.

MHE. PETER J. SERUKAMBA: Baada ya kusema hayo lakini nimalizie kwa neno moja tu, jambo moja, Waziri wa Fedha mwaka jana alitoa amnesty ya watu walipe kodi ambao hawajalipa kodi za nyuma, kuna watu wamelipa asilimia 50, asilimia 70 mpaka kwenda juu, ningemuomba Waziri wa Fedha wale ambao wameonesha interest ya kulipa over 50% a-extend time kwa sababu hawa wana nia hawajamaliza kwasababu hali ya biashara ngumu.

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo naomba kuunga mkono hoja. (Makofi)