Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa fursa. Kwanza nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujalia sote afya na nguvu ya kuja kutimiza wajibu wetu.

Mheshimiwa Spika, mimi nianze kwa maneno yafuatayo; litmus paper ya sera za fedha na fiscal measures ya kwanza ni Revenue Authority, kwamba je, malengo tuliyojiwekea na mimi niingie on record, siyo sahihi na Waziri wa Fedha anajua hili, siyo sahihi kusema Watanzania hawalipi kodi. Labda tuseme ni sahihi kusema kuna Watanzania wachache hawalipi direct tax, kila Mtanzania wa nchi hii analipa kodi whether ni direct or indirect. Kwa hiyo, hii dhana naiona siyo dhana sahihi kwa sababu hakuna Mtanzania hanunui bidhaa, anaponunua bidhaa amelipa kodi. Kwa hiyo, hii ni dhana ambayo ni vizuri sana ikawa inaelezwa vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mimi mkononi hapa na hii ni Wizara ya Fedha yenye jukumu la kusimamia fiscal measures. Mkononi hapa nina takwimu za miaka kumi zinazoonesha trend ya makusanyo ya kodi ya nchi yetu. Kati ya matarajio na hali halisi, the focus error kwa kipindi cha miaka kumi kwenye Revenue Authority ni asilimia 17 yaani kwa miaka kumi asilimia 17 haijawahi kufikiwa, kila ukitenga shilingi moja kwamba ndiyo tutakusanya maana yake kuna asilimia 17 ya hiyo shilingi moja hatutafikia. Ukichukua focus error ya miaka kumi ya bajeti nzima ni asilimia 27, hizi hapa ni takwimu za Serikali za miaka kumi.

Mheshimiwa Spika, sasa kwa nini nimesema litmus paper ni TRA? Kwa sababu kule ndiko tunakoenda kukusanya mapato. Sasa unakusanya mapato kutoka wapi? Hapa ndiyo linakuja jukumu la Wizara ya Fedha kusimamia fiscal measures zake. Nataka nitoe mifano, kuna makosa ya kiutawala yanayofanyika katika nchi yetu yana-destroy economy.

Mheshimiwa Spika, ripoti ya IMF ambayo ni leaked ambayo hatupendi kuisikia imezungumzia jambo moja, business environment. Tunapozungumzia business environment ni hatua tunazochukua ambazo nyingi zinakwenda kuathiri TRA function. Mfano, kuna watu wanaingiza sukari za viwandani wanapitisha kwa njia za panya kuziingiza sokoni. Tumeamua kuazisha kodi ambayo ni unconstitutional ya withholding ya 15%. Hili ni suala la administrative, ni suala la usimamizi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa nini kinachotokea, hivi kweli Waziri, Mheshimiwa Dkt. Mpango, Coca Cola ataingiza industrial sugar aipeleke Kariakoo akauze? Kwa nini wezi watatu tu wanaojulikana, wanaoingiza sukari za viwandani sokoni tunakwenda ku-destroy the entire sector, why? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, yaani mimi hili swali nimeliuliza ndani ya Kamati ya Bajeti kwa miaka miwili halipati majibu. Yaani tunawajua ambao huwa wanaingiza sukari za viwandani ambazo wanaziingiza sokoni, hawazidi watatu katika nchi, tunawajua. Lakini hatua gani tunachukua? Tunaanzisha kodi ambayo inakwenda kuua cash flow za viwanda. It is unfair. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri Dkt. Mpango, tunakubebesha dhambi nyingi katika nchi hii, malawama mengi, because you are the one, be bold kaka. Walazimishe polisi, walazimishe Wizara ya Mambo ya Ndani, walazimishe wengine wachukue hatua, don’t kill the sector, sector nzima ina-suffer.

Mheshimiwa Spika, kinachotokea ni hivi, anatakiwa alipe withholding tax ambayo refund yake haipo na tulipitisha kuanzisha Escrow Account na nikwambie mimi nampongeza sana Rais, Dkt. Magufuli, najua anakwenda kukutana na wafanyabiashara kila Wilaya wanakwenda watano. I swear zitakuja sheria hapa za kubadilishwa, kama ilivyokuwa kwenye madini, akienda kuwasikiliza.

Mheshimiwa Spika, mimi nasikitika, it is very painful. The business sector is suffering. Nataka nikupe mfano mwingine, these are administrative issues ambaye anakwenda kuathirika ni Wizara ya Fedha, TRA, kuna kiwanda kinakwenda kupigwa mnada kinaitwa Salahi Company Limited kiko Iringa. Angalia hii movie ya kihindi, kile kiwanda kiko kwenye eneo la EPZA, anazalisha pipi na biscuit, kapata certificate zote na kila kitu input yake mojawapo ni sukari kwa ajili ya pipi na biscuit. Document zote zimeenda amezipeleka Bodi ya Sukari unajua Bodi ya Sukari wamewajibu nini? Sisi hatutambui EPZA hizo incentive wanazokupa, kwa hiyo hatukupi kibali.

Sasa nini kimetokea? Kiwanda hiki kilifunguliwa for trial mwaka 2016 for trial for two months kwa ajili ya watu EPZA kujiridhisha quality na TBS na kila kitu baada ya hapo wakazima wame-importraw material ngano yao sasa hivi iko under bounded warehouse ya TRA imeoza. Sukari waliyo import kwasababu hawajapata kibali cha Bodi ya Sukari angalia bureaucracy hii sukari wamezuiliwa mpaka ime- expire bandarini angalia hili, wananchi 120 wa Iringa mjini waliokuwa wameajiriwa wamerudishwa nyumbani. Benki ya Amana leo ina-recall mkopo, asset zao zinapigwa mnada, he is a Tanzanian ame-invest two billion shillings atapata wapi kodi TRA atapata wapi? (Makofi)

Sasa ushauri wangu, Dkt. Mpango leta kasheria humu mimi sijui procedure. Economic Intelligence Unit iliyoko chini ya TRA ipewe mamlaka makubwa ya kisheria kufanya analysis na kukuletea ripoti na kukupa mamlaka ya kum-summon Waziri yeyote anaye-hinder your productivity ili tuondoke kwenye haya matatizo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nikupe mfano mwingine, mimi nimeamua kuongelea hii tu hebu tuulizane maswali kwa nini tumeenda na ambush na mapolisi na mabunduki kwenda kufunga Bureau de Change, why? hatuna sheria, hamna sheria inayosimamia biashara ya fedha ya nje kwa sababu ya luxity ya watu walioajiriwa kusimamia kazi yao tunatafuta shortcut we are going to destroy the sector matokeo yake tutaandikwa kwenye international news kwamba hawa watu are not friend in business inatu-take ages ku-clean that mess, it’s not because we don’t have laws, we have good laws in this country. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la tatu tumbaku hapa Waziri Mpango ametaja sekta zinazochangia zilizokua kwa haraka, mwaka huu sekta ya kilimo imekuwa kwa asilimia tano na hii imekuwa kwa kudra ya Mwenyezi Mungu, ninarudia kwa kudra ya Mwenyezi Mungu. Mvua mwaka jana zimekuwa nyingi growth yetu imetoka 3.7 to 5% ingawa marginal growth na hili ni jambo muhimu sana wachumi wawe wanafanya analysis tunasema tu sekta imekuwa, imekuwa kwa kiwango gani compared na mwaka jana marginal growth yetu is less than ourpopulation growth, ndiyou kweli sasa nini inatokea tumbaku, Zitto kataja Kampuni ya TLTC.

Mheshimiwa Spika, nataka nikwambie hivi it is a bad news again Alliance One ambaye ananunua tumbaku Mkoa wa Tabora, TLTC ndiyo wanunuzi wakubwa wa kwetu kinachotokea umeona hii karatasi ina page 14 haya yote ni mautitiri ya kodi na nini, crisis VAT returns hawarudishiwi hawa watu wa TLTC leo wanafunga Waziri amejitahidi wa- investment mwezi Aprili amekutana nao, lakini mimi najua hawajafikia muafaka wala kutatua tatizo kwahiyo mwaka huu tumbaku tuliyozalisha mwaka juzi ilikuwa kilo milioni 1.2 imeshuka mpaka 370,000 uzalishaji wa tumbaku unashuka….

SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Bashe.

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Spika, moja tunimalize nataka niombe kwa heshima kabisa Waziri Mpango unaweza ukawa unaweza ukawa unafanya kazi kubwa tutajenga Stigler’s, tutajenga TRC, tutajenga everything if hatu-encourage productivity na kufanya biashara katika nchi hii miradi mikubwa yote inayoifanya haiwezi kusaidia kukua kwa uchumi, ni lazima Serikali watu, wabadilike TRA rudisheni VAT mna-suffocate economy ya watu na cash flow za wafanyabiashara. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nashukuru na naunga mkono hoja. (Makofi)