Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Albert Ntabaliba Obama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buhigwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. ALBERT O. NTABALIBA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kunipa nafasi hii niweze kuchangia hii Wizara, kwanza kabisa nimpongeze Waziri, Naibu Waziri na Makatibu Wakuu na Wakuu wa Vitengo vyote vya ndani ya Wizara hii, kwa kweli wameendelea kutupa ushirikiano ndani ya Kamati ya Bajeti, naomba niwapongeze sana. Lakini niendelee kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa kuendelea kuwapa mwongozo mzuri katika usimamizi wa fedha ambayo ni jambo zuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba kabisa nipongeze Kamishna Mkuu wa TRA, kwa taarifa zake za ukusanyaji wa mapato hasa ukiangalia kule kwenye jedwali la makusanyo ukurasa wa 180 utaona kwamba average yake imekuwa ni asilimia 87 ambayo ni nzuri, kwa hiyo nampongeza sana. Lakini niendelee kumpongeza Magavana wote wa Benki Kuu kwa kazi nzuri wanayoendelea kutoa miongozi ya fedha katika nchi hii.

Mheshimiwa Spika, nilitaka tu kumuuliza Mheshimiwa Waziri ukiangalia page yake 178 Ofisi ya Msajili wa Hazina imepewa asilimia 17 ya fedha za OC, sasa nilitaka kujua ni kitu gani kinawafanya wakati Wizara zako na Taasisi zako zilizoko kwako zina asilimia 70, 60 hao wana asilimia 17 na wanasimamia mashirika ya umma. Ni kitu gani wamefanya makosa au ni shughuli gani hawaifanyi mpaka sasa wasiweze kupata fedha? Hilo nilitaka Mheshimiwa Waziri uweze kutupa ufafanuzi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini lingine ni uhakiki, Wizara ya Fedha imechukua majukumu ya kuhakiki fedha, sasa wito wito kwamba speed ya kuhakiki imekuwa ni ndogo na kama kuna timu za uhakiki basi muweze ku-recruit watu wengine kutoka kwenye Wizara nyingine kwa sababu kwa kweli malipo ya wazabuni, wakandarasi yamechelewa sana na halafu hatuna deadline ya kuona ni lini tutaweza kuhakiki. Lakini feedback kwa wale ambao hawakufanikiwa hakuna utaratibu ambao mmeuleza kwenye Kamati ambao unawapa feedback wale ambao madai yao hayakupita qualification zenu, kwa hiyo kule wanaendelea kubaki wanakijua wanadai kumbe ninyi mmeshayatupa pembeni.

Mheshimiwa Spika, lakini la pili kuna sheria hii ya asilimia 15 kama wanazo-deposit hawa wenye viwanda vya sukari, hebu tunaomba maana yake wanakuja kwenye Kamati zetu, wanaonesha mitaji yao imeyumba. Sasa Serikali inahimiza viwanda lakini inachukua fedha zao, lakini haiwarudishii sasa unachohimiza ni nini na unachotaka kufanya ni nini.

Mheshimiwa Spika, ukiangalia Mheshimiwa Waziri kwenye hotuba yako yote ni control, hakuna mahali kwenye Wizara hapa unachosema kwamba nitahamasisha wafanyabiashara wafanye hivi, nitahamasisha wakulima wafanye hivi. Sasa ni mambo umejaza mambo ya kodi tu ambayo kwa kweli ni vizuri huko mbele style hii na wanaposikia hotuba yako wapate faraja wafanyabiashara, wachimbaji waone faraja. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lingine nipongeze BOT kwa hatua yao kwa kupitia Sheria hii ya Bureau De Change sisi tuwape nguvu tuwaombe waendelee walete kanuni na wale wanafanya biashara ya Bureau De Change ambao hawana makosa basi waweze kufunguliwa waweze kwenda vizuri.

Mheshimiwa Spika, lingine ni kuchelewa kwa madai ya wastaafu. Wastaafu wanadai, wastaafu inachukua mwaka mzima bado hajalipwa fedha zake, hebu tunakuomba hicho kitengo kinachoshughulikia wastaafu kwa sababu ile database ya watu wanaostaafu Mheshimiwa Waziri mnayo kila Idara na kila sekta. Kwa hiyo, ni vizuri nayo hii iweze kuangaliwa vizuri iweze kwenda haraka.

Mheshimiwa Spika, lakini la mwisho ni mambo ya business license. Sasa hivi Watanzania wote hatuwezi kuajiriwa, watu wanatafuta namna ya kujiajiri, lakini bureaucracy iliyopo unapotaka leseni mpaka unaambiwa uende kwenye TRA ukapate tax clearance; tax clearance unaipataje na hujaanza biashara?

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ni vizuri huu mfumo uliopo hebu tuurahisishe mtu akienda kutafuta leseni siku hiyohiyo au siku ya pili aweze kuipata, lakini kuliko kuzunguka aende TRA kumbe hajaanza biashara na akifika kule anaanza kukadiriwa biashara, unataka kufanya biashara gani? Unaanza kukadiriwa kodi na huku biashara haujaanza, kwa hiyo, ni vizuri sana muweze kuiangalia hiyo, ili tuweze kwenda vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nisiseme mengi. Mengi tumeyasema kwenye Kamati yetu ya Bajeti na nisipende kuyarudia kwa sababu tumeyaandika na Wabunge wote wameyaona. Nakushukuru sana. (Makofi)