Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nianze mchango wangu na Sekta ya Ualimu. Mtiririko mzima wa kuandaa Walimu una kasoro kubwa sana hasa tangu kuchafuliwa kwao kwenda kwenye Vyuo vya Walimu kwa kuwachagua watu wenye ufaulu wa chini kuingia kwenye Vyuo vya Ualimu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile kitendo cha wahitimu kukaa mwaka mzima wakisubiri ajira kinavunja moyo Walimu wetu. Hata hivyo, kitendo cha Walimu kushindwa kuwapandisha madaraja kwa muda mrefu na pale wanapopanda kushindwa kuwapa stahiki zao, nako ni kuvuruga kiwango cha elimu nchini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Walimu kufanya kazi nje ya ajira yao, mara nyingi Walimu wamekuwa wakitumikia kwenye kazi kama vile sensa, kusimamia uchaguzi, kuwa Watendaji wa Vijiji nakadhalika. Mwalimu anaposimamia uchaguzi na Chama Tawala kikianguka kwenye Kituo husika, basi huyuo Mwalimu Mwalimu ajira yake huwa hatarini. Ninayo majina ya walimu waathirika na hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye Jimbo langu la Liwale ambako CCM ni Chama cha Upinzani, ushauri wangu ni kwamba tuwaache Walimu wabaki madarasani. Pamoja na changamoto nyingi tunazokabiliana nazo ili kujikwamua kutokana na umasikini uliokithiri mahitaji ya Chuo cha VETA Liwale ni muhimu sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na Chuo cha Walimu, kwani Walimu wanaotoka nje ya Mkoa wetu wa Lindi wanashindwa kukaa Liwale. Vilevile tunaomba Kituo cha Chuo cha Utalii ili kukuza utalii Kusini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Shule za Jimbo la Liwale hazina Wakaguzi na wale wachache waliopo hawana vitendea kazi. Hawana gari hata moja la ukaguzi wala pikipiki. Tunawezaje kuwa na elimu bora, elimu ambayo haisimamiwi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kupanda kwa madaraja ya Walimu kuzingatie kiwango cha elimu. Hakuna utendaji ulio bora kama Mratibu Kata ni Form IV, Mwalimu Mkuu Degree au Mkuu wa Shule Diploma, Mwalimu Degree, hapo hakuna uwiano wowote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Sera ya Elimu imeshusha kiwango cha elimu nchini. Leo watoto hawana mitihani ya Mid-term, mitihani ya wiki, Mock – Kata, Mock – Wilaya, wala Mock – Mkoa. Sasa hivi mtoto hupimwa mara moja tu kwa mwaka mzima. Utajuaje maendeleo ya mtoto anayefanya mtihani mmoja tu kwa mhula?
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.