Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

Hon. Agnes Mathew Marwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

MHE. AGNESS M. MARWA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii ili nami nichangie Wizara hii.

Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa nimpongeze sana Mheshimiwa wangu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuunda Tume ya Mawaziri nane; Waziri wa TAMISEMI, Ardhi, Maji, Ulinzi, Kilimo, Maliasili, Ofisi ya Makamu wa Rais ambayo ni Mazingira; kwa lengo tu la kuhakikisha kwamba matatizo ya ardhi yanashughulikiwa ipasavyo. Kwa kweli Mheshimiwa Rais anafanya kazi nzuri sana na ndiyo maana imefikia hatua wananchi wamekaa kimya. Wale wanaosema wao wanataka Katiba mpya mambo yote yametendwa, mambo yote Mheshimiwa Rais anayafanya sasa yale waliyokuwa wanahitaji wao yafanywe katika Katiba mpya.

Mheshimiwa Spika, lakini haitoshi hiyo, mimi niwe kidogpo tofauti na wenzangu badala ya bomoabomoa namshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa jenga jenga. Kakijenga Chama chetu Chama cha Mapinduzi, kaijenga Tanzania kwa ujumla na ndiyo maana bomoabomoa imebadilika imebomoa vyama vya upinzani.

Mheshimiwa Spika, lakini pia nimpongeze sana Mheshimiwa wetu Waziri Lukuvi, Mheshimiwa Waziri wetu hongera sana kwa kweli kwa kazi nzuri unayoifanya ya kutembelea wanachi na kushughulikia migogoro yao wewe pamoja na Dada yangu Mheshimiwa Angelina Mabula; na ndiyo maana badala ya kuzeeka sasa mnakuwa vijana kwa ajili ya kutembea sana na kushughulikia kero za wananchi.

Mheshimiwa Spika, Wizara hii ni nyeti sana katika hali halisi ya uchumi wa Watanzania. Kwetu Serengeti Mkoa wa Mara kumekuwa na shida na migogoro mingi sana; katika Wilaya ya Tarime na Wilaya ya Bunda lakini yote haya Mheshimiwa Waziri na Naibu wake wameyashughulikia kwa undani zaidi na kwa uzuri; kwa kweli Mheshimiwa Waziri hongera sana. Tunawashukuru sana kwa kusababisha ile ardhi iliyokuwa inatuletea shida, sasa mmeiweka katika mipango mizuri, kwamba sasa iwe katika matumizi bora ya ardhi. Mimi niwaombe tu mfanye haraka ili wale wananchi waliokuwa wanapata shida kutokana na ugomvi au migogoro ya ardhi sasa waweze kuitumia ardhi yao. Migogoro yote iliyokuwepo sasa imekwisha hivyo tunaomba wagawiwe ili waweze kuitumia vizuri.

Mheshimiwa Spika, kule kwetu Tarime wanawake tulikuwa haturuhusiwi kumiliki ardhi; kumiliki ardhi ilikuwa ni kama kosa la jinai, lakini kutokana na utendaji mzuri na upendo wa Mheshimiwa Rais na Mawaziri wake kwa wananchi wake wa hali ya chini sasa tunaweza kumiliki ardhi ambazo wanawake pia tunakwenda kuchukua hati, tena tunachukua hati kwa muda. Kwahiyo ninamshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa kuona kwamba hata sisi watu wa hali ya chini na haswa wanawake wa Mkoa wa Mara sasa wanaweza kuimiliki hii ardhi.

Mheshimiwa Spika, niombe Wizara hii; pamoja na mambo yote kuna changamoto ambazo bado wanatakiwa wazishughulikie. Kuna baadhi ya wafanyakazi au watendaji wa Wizara hii ambao hawaoni kwamba wao wanapaswa kuendana na kasi ya Mheshimiwa Rais; bado wamekuwa ni wasumbufu sana katika Wizara hii. Wamekuwa bado wakiowaomba rushwa wananchi bila kujali kwamba wananchi wana hali mbaya au hali ngumu, lakini pia wamekuwa hawafanyi kazi ipasavyo na kwa muda; na ni wachache tu wanaosababisha hii Wizara ionekane kama vile bado ina matatizo matatizo. Mheshimiwa Waziri Lukuvi Mungu akikubariki hebu ingia sasa na kwa hao wafanyakazi warudishe tu angalau na wao vijijini wakalime ili kusudi wale wanaoweza kufanyakazi; kuna wananchi wengi sana ambao hawana kazi; nao wapate kazi za kufanya.

Mheshimiwa Spika, katika utendaji wa Mheshimiwa Lukuvi kuna maeneo ambayo yamepakana na hifadhi ambapo ni Wilaya ya Bunda, maeneo ya Nyatwali. Ni muda mrefu sasa hilo eneo…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)

SPIKA: Ahsante Mheshimiwa Agness.

MHE. AGNESS M. MARWA: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja asilimia mia kwa mia.