Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

Hon. Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

MHE. DKT. STEVEN L. KIRUSWA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa niwezeuwa wa kwanza kuchangia alasiri hii kwenye hoja hii yetu muhimu ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.

Mheshimiwa Spika, mimi ni mjumbe wa kamati ya Wizara hii, ninakiri na kuungana na wezangu wote wanaowapongeza watendaji wakuu wa Wizara hii kwa kazi nzuri wanayoifanya. Mheshimiwa William Lukuvi, Mheshimiwa Angelina Mabula, Waheshimiwa Katibu Mkuu, Doroth Mwanyika na Naibu Mathias Kagundugulu, kazi mnayoifanya pamoja na watendaji wengine wote wa idara mbalimbali, tukiwa nyuma yenu ni kazi iliyotukuka, nawapongeza sana. (Makofi)

Pamoja na hayo kazi yenu ni kubwa, haijafika hata nusu, bado mna kazi kubwa sana mbele yetu na nifananishe kazi mnayoifanya na uhalisia kwamba ninyi ni Wizara ya Ardhi au sisi ni Wizara ya Ardhi; na ardhi ni kitu cha kipekee sana katika masha ya mwanadamu na uumbaji. Kwa wale wanaosoma Biblia, mnaweza mkarejea katika kitabu cha Mwanzo kwanza Mungu alioiumba hii dunia, akaweka vitu vyote na mwishoni akamweka mwanadamu alimpa wajibu wa kuitunza, akamweka katika Bustani ya Edeni aitunze.

Mheshimiwa Spika, na baada ya watu kuongezeka, tukatawanyika duniani kote; na sasa nasema mwenyewe siyo kwenye Msahafu tena; tulijikuta kwamba kila sehemu ya dunia ni sehemu ya hiyo bustani na sisi Watanzania tukajikuta tuko Tanzania ndiyo bustani yetu ya edeni ambayo tuna wajibu wa kuitunza. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, katika muda mufupi ambao nimetumikia kwenye kamati ya Wizara hii na nikiwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nimeweza kutembea maeneo mbalimbali nikashuhudia jinsi ambavyo watanzania tumejisahau katika suala zima la kutunza hii bustani yetu ya edeni, nchi yetu ya Tanzania. Mipaka yake imeingilia kuanzia mpaka wa Uganda, Rwanda, Burundi, Kenya, kila moja ina mgogoro kwa sababu imeingiliwa, na ni kwa sababu watanzania sijui tulifikiri kwamba ardhi haina ukomo, tukaachia mpaka majirani zetu wakaingilia mpaka kwenye mipaka yetu.

Mheshimiwa Spika, mimi naiomba Serikali, kwa sababu sasa tumezinduka na tumeoa Sera nzuri ya Ardhi tuliyonayo, ielekeze nguvu ya kipekee katika kuiwezesha Wizara hii kupanga, kupima na kumilikisha kila kipande cha ardhi ya nchi yetu, ipewe nguvu sana inayopewa sekta ya ukuzaji wa viwanda, uchumi wa kati. Namuomba Mheshimiwa Rais aibebe Wizara hii, aifanye moja ya Wizara mahsusi ya kushughulikiwa ili tuweze kuipima hii ardhi yetu na tuondokana na hii migogoro ambayo itazidi kuongezeka tusipochukua jukumu. Mipaka inagombaniwa katika ngazi za vijiji, kata, tarafa, wilaya, kati ya mkoa na mkoa na sasa hata katika ngazi ya nchi na nchi.

Mheshimiwa Spika, nafikiri tukiendelea kuiona Tanzania iliyojaa migogoro isiyowahikuisha ya ardhi.

Nashukuru sana kazi nzuri aliyofanya Mheshimiwa Rais ya kuteua Wizara za kushughulika na migogoro ya ardhi. Nimeona umeshika ile dossier ya Mheshimiwa Waziri, likitabu ambalo umesema ni mwarobaini wa hizo kero zetu. Ninakwenda kuamini kwamba itakwenda kutumalizia kero ya migogoro tuliyonayo ya muda mrefu.

Mheshimiwa Spika, kwa mfano sisi Longido kule wasiwasi kuna migogoro ya miaka 20, kijiji na kijiji tu, kata na kata, Matale na Gelai Lumbwa. Mipaka yetu na Mwonduli upande wa Engaruka, mipaka yetu na Arumeru upande wa Oldonyo Sambu na Engikaret, mipaka yetu na NARCO Ranch na kila sehemu. Hii basi ifanyike sera; ambayo hata katika bajeti hii mimi ningeomba Wizara na Serikali kwa ujumla tengeni mafungu muwape Halmashauri na ofisi za ma-DC ili hii migogoro ya ngazi ya wilaya waimalize wao wenyewe na muwape deadline. Wakati mwingine wanakwama kwa sababu zinahitaji resources kwenda kuhakiki, kupima na kushirikisha pande zote.

Mheshimiwa Spika, naomba hilo lizingatiwe ili tuondokane na hii kero ya migogoro ya ndani, na tukiwa kuendelea kurasimisha makazi yale ambayo yalishavamiwa zamani tulipokuwa hatujijui nayo iweze kuendelea. Tumejiachia mpaka mabonde yasiyofaa kuishi watu wakaishi, milima isiyofaa kuishi watu wakaishi na ndiyo maana leo tuna sera ya urasimishaji.

Mheshimiwa Spika, naomba pia nielekeze kauli mbiu yangu katika kuishauri Serikali. Ukienda kule katika mwisho wa Wilaya ya Longido inapopakana na Rombo, kuna kamwanya ka nchi kali mwisho wa mpaka wa Tanzania na Kenya pale na Rombo kuna watu, nina orodha yao hapa, watu 196 bao waliorodhesha mwaka 2016 ambao wameishi hapo miaka nenda miaka rudi, wamezaliana, hawana pa kwenda. Zoezi la kuhakiki mipaka lilipopita wakaonekana hawastahili kuwa pale, wameiandikia Serikali barua kuomba watafutiwe mahali pa kwenda kuishi. Walikuwa 196 mwaka 2016, sasa hivi wameendelea kuongezeka na ninaamini watakuwa zaidi ya 200. Wengine wamezaliwa palepale, hawajuwi pa kwenda, hawana ardhi, wanaishi kwenye strip ya no man’s land. Wanakodisha mashamba ya kulima Kenya na wakati mwingine idara ya misitu upande wa Mlima Kilimanjaro wanapovuna misitu, ndiyo wanakwenda kulima pale. Wananchi wale hawana ardhi na hivyo wanaililia Serikali kwamba watafutiwe mahali pa kwenda kuishi.

Mheshimiwa Spika, vilevile nipende tu kuiasa Serikali, kwamba tunapokwenda kupanga, kupima na kumilikisha kila kipande cha ardhi ya nchi yetu tuzingatie suala la kuweka benki ya ardhi; kila kijiji iwekwe benki ya ardhi kwa ajili ya matumizi ya baadaye ya vizazi vijavyo na maendeleo yatakayozidi kujitokeza. Sambamba na hilo, kwa sababu naona kama tunasubiri mpaka mazingira ya mahali paive, sijui idadi ya watu ifikie watu wangapi, ndipo tunapoingia kufanya mipango miji; tuanze kupanga miji yetu mpaka ile inayotarajiwa baadaye, maeneo ya wazi yasiyo na migogoro yapimwe, Serikali iwe na kazi moja tu ya kumuonyesha kila mtu sehemu iliyopimwa anapokuwa tayari kuhitaji eneo la kujiendeleza na kujenga makazi yake.

Mheshimiwa Spika, kwa ajili hiyo basi niangalize kwamba sisi wafugaji wa Wilaya ya Longido, tulishabainisha mpaka nyanda zetu za malisho, zinafika 27 kwa sasa hivi. Tunaomba mkono wa Serikali katika kutusaidia kupima, kurasimisha, tuweze kusimamia kama maeneo ya malisho na benki yetu ya ardhi ya vizazi vijavyo; na kwa ajili hiyo wakati huo tutakuwa tunaingezea Serikali mapato maana najua kila ardhi iliyopimwa, tunalipia kodi. Tuko tayari, tunakata ku-secure ardhi yetu na Watanzania wote wanahimiza waweke benki ya ardhi, maeneo ya malisho na kilimo na makazi ya watu na tufuate sera hiyo hiyo.

Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa muda huu mfupi ulionipa, mawazo yangu ni hayo pamoja na kuungana na maoni yetu ya Kamati ambayo tumeyaandika na kubainisha na yamewasilishwa leo asubuhi. Naunga mkono hoja asilimia 100. (Makofi)