Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

Hon. Hawa Abdulrahiman Ghasia

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mtwara Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

MHE. HAWA A. GHASIA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Nikushukuru sana kwa kunipa nafasi niweze kuchangia katika bajeti ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.

Mheshimiwa Spika, kwanza nianze kuwapongeza sana Mheshimiwa Waziri na Naibu wake kwa kazi kubwa sana wanayoifanya. Wote ni mashahidi, tunafahamu tulikotoka kwa kiasi gani Wizara hii ilikuwa na changamoto nyingi sana na kwa kiasi gani wameweza kuzifanyia kazi changamoto nyingi ambazo zilikuwa zinaikabili Wizara ya Ardhi.

Mheshimiwa Spika, kuna mageuzi makubwa sana ambayo Wizara imeyafanya. Sasa hivi karibu maeneo mengi master plan au mipango kabambe ya ardhi inaandaliwa mpaka katika ngazi za halmashauri kwa hiyo, napenda sana. Wamekuwa wakiandaa mipango ya makazi na vijiji, wamekuwa wakisimamia udhibiti na uendelezaji wa miji. Pia niwapongeze kwa kutwaa baadhi ya maeneo ambayo kwa kiasi kikubwa yalikuwa ni mashamba pori.

Mheshimiwa Spika, nishukuru sana kwa sababu haiwezekani mtu anachukua eneo anasema anataka kuwekeza, kufanya shamba, anachukua zaidi ya miaka 17 hajaotesha mti hata mmoja, hajaendeleza, hajafanya hilo shamba na bado tuendelee kumuangalia. Kwa kweli ninaipongeza sana hii Wizara.

Mheshimiwa Spika, pia, ninapongeza hasa ukizingatia taarifa ya Kamati, kamati wameipongeza sana Wizara yao na wamesema katika mapendekezo yale mengi ambayo waliipa Wizara yamefanyiwa kazi. Sioni kwanini Wizara hii ijadiliwe siku mbili, haki yake ilikuwa tujadili leo, ifike jioni tumalize tuangalie yajayo ambayo ni kukaribisha Eid na wale wanaoenda mbali waweze kwenda lakini vinginevyo kazi kubwa sana Wizara imefanya kikubwa ni kuishauri Serikali iendelee kuipatia fedha Wizara iweze kufanya kazi ambazo zinatakiwa.

Mheshimiwa Spika, jingine ambalo nilitaka kushauri. Wizara inajenga nyumba nyingi sana kupitia National Housing na mfuko wa watumishi wa umma lakini zile nyumba zenyewe pia waziweke kwa makundi, tusiweke tu za gharama nafuu. Kuna nyumba zingine zinajengwa karibu karibu hata ukikohoa jirani yako anakusikia. Watakapojenga nyingine basi waziweke kwa tabaka, waweke zile za bei nafuu lakini pia waweke na daraja la kati na wale wa juu pia wawafikirie kwa sababu unaweza hizi za gharama nafuu ukajenga asilimia 60, zile nyingine asilimia 20.

Mheshimiwa Spika, mwisho nirudie tena kuwaomba Waheshimiwa Wabunge wenzangu ikiwezekana hii bajeti leo basi tuibariki kwa sababu kazi kubwa wameifanya na wanaendelea kuifanya Waheshimiwa Wabunge.

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, naomba kutoa hoja kwamba bajeti hii tuimalize leo. (Makofi)