Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Dr. Adelardus Lubango Kilangi

Sex

Male

Party

Ex-Officio

Constituent

None

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MWENASHERIA MKUU WA SERIKALI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa muda na mimi niweze kuchangia hitimisho la hoja ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati.

Mheshimia Spika, katika mchango wangu nitajielekeza moja kwa moja kwa hoja aliyoitoa Mheshimiwa Hawa Ghasia katika mchango wake ambapo alizungumza kwamba katika mazingira ya sasa hivi inaonekana kama hakuna leseni mpya ambazo Mheshimiwa Waziri amezitoa katika sekta hii ya gesi. Pengine sababu mojawapo ya kutokuwa na leseni mpya zinatolewa ni kwa sababu hii mikataba iliyopo ya utafutaji na uchimbaji wa gesi iko kwa AG; na akaniomba kama ninaweza kwa sababu nipo, nizungumzie suala hili ili kuweza kumuepusha Mheshimiwa Waziri na kuondolewa shilingi yake; nami napenda nilizungumzie hili kwa kifupi.

Mheshimiwa Spika, kama unafahamu uliunda Kamati ya kuangalia sekta ndogo ya gesi pamoja na uvuvi. Kamati ile ilikuja na taarifa yake na ilikuja pia na mapendekezo yaliyokuwa katika taarifa ile. Mojawapo ya mapendekezo kama mnavyofahamu vizuri kabisa ilikuwa kwamba iko haja ya kurejea hii mikataba ya utafutaji na uchimbaji wa gesi (production sharing agreements), na kazi hiyo ikapewa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Kwa hiyo ni kweli kabisa kwamba mikataba hiyo anaishughulikia Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Mheshimiwa Spika, sasa naomba nichukue nafasi hii kueleza tu tumefika wapi katika zoezi hilo. Tulianza kazi na zoezi la kuipitia hiyo mikataba yote, tuliunda timu ilipata wataalam kutoka Wizara mbalimbali na sekta mbalimbali za Serikali; na tukaanza hiyo kazi. Ilitulazimu tuanze kwanza kwa kuwajengea uwazo hii timu ili iweze kufahamu ni kitu gani inakifanyia review. Hilo zoezi lilikamilika, baada ya zoezi hilo lilifuata sasa zoezi la kuipitia mikataba yenyewe; na timu hii imekaa kwa karibu kipindi cha miezi miwili na imefanya kazi ya kupitia ile mikata yote kumi na moja ambayo inahusika na utafiti na uchimbaji wa gesi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya kufanya zoezi hilo tuligundua kwamba kuna kitu ambacho ni muhimu sana kukiangalia, kwa kiingereza wanaita economic and financial modeling. Kwa sababu hapo ndipo siri nzima ilipolala, kama mnapoteza au kama mnafaidika au kama mnapata iko kwenye economic and financial modeling. Kwa hiyo tukaweka tena awamu nyingine ili timu hii ikae na ikafanya kazi hiyo kwa kipindi cha takriban mwezi mmoja. Ninavyozungumza timu hiyo imemaliza hiyo kazi ya kuangalia economic and financial modeling. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, walichokifanya katika zoezi hili ilikuwa ni kuangalia financial na economic modeling gani ilitumika katika hizi PSAs.

Kwa hiyo, baada ya hiyo kazi wakagundua kwamba ni lazima turudi tena tuangalie sisi kama nchi tunapendekeza economic na financial modeling ipi. Sasa katika hilo zoezi la tatu ambalo nimelitaja, timu hii inakutana tena kuanzia tarehe 6 Juni, na itamaliza kazi yake tarehe 25 Juni.

Mheshimiwa Spika, niseme tu kwa ufupi kwa sababu mambo mengi bado yapo kwenye taarifa hii, zoezi hili limetufanya tuelewe matatizo mengi yaliyo kwenye mikataba hii na mapungufu ambayo tunahitaji tuyafanyie kazi. Pia, kikubwa kabisa tutakachokipata kwenye zoezi hili litatufahamisha yaani lita-inform tunapoanza majadiliano ya LNG, kwa sababu hii mikataba mingi ilisukwa kwa namna ambayo baadae ingekuja ku-influence chochote ambacho tungekubaliana kwenye LNG.

Mheshimiwa Spika, ni hayo tu niliyokuwa napenda kushirikisha na kwa ujumla ninaunga mkono hoja, ahsante sana. (Makofi)