Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Dr. Haji Hussein Mponda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. DKT. HADJI H. MPONDA: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja na kuwapongeza Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na team yote ya Wizara kwa utekelezaji wa majukumu yao pamoja na changamoto ya ufinyu wa bajeti. Pongezi pia kwa TANESCO kwa uendelezaji mzuri wa taasisi kufikia matokeo chanya hadi 2019 kutoa gawio kwa Serikali.

Mheshimiwa Spika, Mkoa wa Morogoro kama hatua za dharura hazitachukuliwa dhidi ya mkandarasi wa REA III, M/S State Grid mradi huu hautokamilika kutokana na uwezo hafifu wa mkandarasi huyo Mkoani Morogoro katika REA III.

Mheshimiwa Spika, mkandarasi huyu State Grid alishindwa kumaliza mradi wa REA II katika Mkoa wa Lindi (2012 - 2016). Hata hivyo la ajabu bado mkandarasi huyu anaendelea kupewa kazi tena katika Mkoa huohuo wa Lindi na Morogoro, licha ya mapungufu makubwa katika utendaji kazi katika miradi ya umeme.

Mheshimiwa Spika, Mkandarasi ameonesha waziwazi kushindwa kazi kwa sababu zifuatazo; uwezo finyu kiufundi, fedha, vifaa vya kufabyia kazi na usafiri.

Mheshimiwa Spika, nashauri Serikali aidha itengue mkataba au wamlazimishe mkandarasi aweke wakandarasi wadogo (sub- contracting) au wasaidiane na timu ya ufundi TANESCO Mkoa wa Morogoro.

Mheshimiwa Spika, mradi wa kuzalisha umeme wa Stiegler’s Gorge Power Project katika kutengeneza masuala ya mazingira/huduma kwa jamii imeelekeza zaidi katika upande wa Lower Rufiji kwa kuweka miradi kama ya mabwawa, skimu za umwagiliaji n.k. Mradi huu umesahau/ umeacha kabisa upande wa Upper Rufiji ambapo ndiko kunakozalisha maji kwa kuendesha mradi wote mfano Mto Kilombero na bonde lake linazalisha adilimia 65 ya maji yote ya mradi.

Mheshimiwa Spika, Serikali ni muhimu wangepima upya mradi na kuona namna gani wanaweka miradi ya kijamii na mazingira katika maeneo ya Upper Rufiji (Wilaya ya Malinyi, Ulanga, Kilombero) kutekeleza miradi ya skimu za umwagiliaji n.k ili kuwezesha kulinda mazingira wezeshi kuweka uendelevu wa Mto Kilombero.