Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

Hon. Ally Seif Ungando

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Nishati

MHE. ALLY S. UNGANDO: Mheshimiwa Spika, napenda kuchangia hotuba hii ya Waziri wa Nishati kwa maandishi. Napenda kuwapongeza Waziri na Naibu wake kwa kazi nzuri wanayoifanya ya kuhakikisha wanazima vibatali nchi nzima na kuwasha umeme maeneo yote ya vijijini na mijini.

Mheshimiwa Spika, katika Jimbo langu la Kibiti tunashukuru sana Serikali yetu ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais wetu mpendwa Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa kazi nzuri.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo hadi leo vipo vijiji ambavyo havina umeme ambavyo nguzo na waya tayari kwa muda mrefu lakini cha kushangaza hadi leo umeme bado haujawaka kutokana na tatizo la transfomer. Vijiji hivyo ni Nyamatanga, Kikale na Ruaruke; naomba vijiji hivyo viangaliwe kwa jicho la huruma.

Mheshimiwa Spika, Jimbo la Kibiti lina jumla ya Kata 16, vijiji 58 vitongoji 42 vipo katika visiwa vya Bahari ya Hindi kama Mfisini, Kivimbuni, Salale, Msala, Mbwera na maeneo mengine ambayo hadi leo havina umeme kabisa. Naomba Serikali yangu sikivu ituangalie kwa jicho la kipekee katika visiwa vyetu vya Kibiti.

Mheshimiwa Spika, sambamba na hivyo, Wilaya ya Kibiti ina Mji Mdogo Kibiti ambapo ina jumla ya vitongoji 39 ambavyo baadhi ya vitongoji havina umeme kabisa; kama vile Makina, Zimwini, Nyambangala, Mroso, Bumba, Ugezi, Kikota, Penda Miwaga, Penda na Kimbuga.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.